Skip to main content

Posts

Showing posts from July, 2020

TASAF KIPINDI CHA PILI CHA AWAMU YA TATU YAANZA RASMI UTEKELEZAJI WA AGIZO LA MH.RAIS MAGUFULI

Na Swaum Katambo,Site Tv Nsimbo-Katavi Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) umeanza utekelezaji wa wa kipindi cha Pili cha awamu ya tatu ya TASAF ambapo ruzuku kwa walengwa zitafanyika kwa njia ya Mtandao nchi nzima. Akitoa Hotuba kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF,Bw.Ladislaus Mwamanga wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha wakuu wa Idara na mafunzo ya wawezeshaji wa Halmashauri kuhusu Utekelezaji wa Kipindi cha Pili cha Awamu ya Tatu ya TASAF na uhakiki wa Kaya za walengwa wa Mpango wa kunususru Kaya Masikini uliofanyika katika Halmashauri ya Nsimbo Wilaya ya Mpanda Mkoani Katavi Bi Josephine Pupia alisema kipindi hiki cha pili kitatekelezwa katika Halmashauri zote 185 za Tanzania Bara na Wilaya zote za Zanzibar. "Utekelezaji huo utafanyika kwenye Vijiji/Mitaa/Sehia zote nchini na kujumuisha maeneo ya Vijiji/Mitaa/Sehia ambayo hayakupata Fursa hiyo katika kipindi cha kwanza cha utekelezaji wake ambacho kimekamilika." Alisema Bi.Rupia Kulia (aliyevaa nguo ya ...

Serikali yatoa bilioni 16 kutekeleza miradi ya maji Ruvuma

Miradi ya maji wilaya ya Nyasa SERIKALI ya awamu ya tano imetoa zaidi ya shilingi bilioni 16 kutekeleza miradi mbalimbali ya maji mkoani Ruvuma hali iliyoweza wananchi 1,149,867 kupata maji safi na salama hadi kufikia mwakahuu. Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amesema idadi ya wananchi wanaopata huduma ya maji safi na salama katika Mkoa wa Ruvuma hivi sasa ni asilimia 63.9 ya wakazi wote wa Mkoa idadi ambayo imeongezeka kutoka asilimia 57 ya wananchi waliokuwa wakipata huduma hiyo mwaka 2015. Hata hivyo Mndeme amewataja wananchi wanaoishi maeneo ya vijijini wanaopata huduma ya maji safi na salama wanakadiriwa kuwa 888,005 ambao ni sawa na asilimia 61.6,ambao wanapata maji kupitia vituo vyakuchotea maji 5,631 . “Katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji safi na salama na kufikia malengo ya kitaifa, Mhe, Rais ameendelea kuwezesha ukarabati na ujenzi wa miradi mipya ya maji, kuanzisha na kusajili kisheria jumuiya za watumia maji vijijini kwa ajili ya kusimamia ...

JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA LINAWASHIKILIA WATUHUMIWA TISA KWA TUHUMA MBALIMBALI.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi wa Polisi SEBASTIAN MBUTA Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia JUSTINE SADIQ [18] Fundi rangi na mkazi wa Ndola katika Mji Mdogo Mbalizi akiwa na mali mbalimbali za wizi mnamo tarehe 20/07/2020 majira ya saa 15:30 Alasiri katika Kijiji na Kitongoji cha Mwampalala, Kata ya Iwindi, Tarafa ya Usongwe, Wilaya ya Mbeya Vijijini. Akitoa taarifa hizo Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi wa Polisi SEBASTIAN MBUTA alisema walimkamata mtuhumiwa huyo akiwa mali za wizi ambazo TV moja aina ya “Sansan” nyeusi,Deki moja aina ya “Singsung”,Remote control mbili,na Tarakishi Mpakato aina ya Compac moja pamoja na “adapter” yake zikiwa kwenye mfuko wa sandarusi ambapo thamani ya mali hizo bado haijajulikana na ufuatiliaji unaendelea. Jeshi la Polisi pia linamshikilia ZUENA SELEMAN [48] Mfanyabiashara, na Mkazi wa Uyole akiwa na vipodozi vilivyopigwa marufuku nchini vyenye viambata sumu. "Mtuhumiwa alikamatwa mna...

HALMASHAURI YA MJI MBINGA ILIVYOFANIKIWA KUJENGA NYUMBA NANE ZA WATUMISHI KWA MILIONI 650

Mradi wa nyumba saba za wakuu wa Idara wenye thamani ya shilingi milioni 350 ambao unatekelezwa katika Halmashauri ya Mji Mbinga,ujenzi wake umefikia zaidi ya asilimia 75 HALMASHAURI ya Mji wa Mbinga Mkoani Ruvuma, imetumia shilingi milioni 650 kwa ajili ya kutekeleza mradi wa ujenzi wa nyumba saba za wakuu wa Idara na nyumba moja ya Mkurugenzi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Grace Quintine amesema Halmashauri yake katika kipindi cha mwaka 2019/2020 ilipokea kiasi cha sh.milioni 350 kwa ajili ya nyumba saba za wakuu wa Idara na kwamba shughuli za utekelezaji zilianza Machi 26 ambapo hadi sasa mradi umefikia asilimia 75. “Jumla ya shilingi milioni 284.374 zimetumika hadi sasa kati ya milioni 350,vifaa vyote vya viwandani kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo vimenunuliwa’’ ,alisema Quintine. Amesema mradi ulitarajiwa kukamilika Juni mwaka huu,hata hivyo kutokana na changamoto ya kuchelewa kupokea bati ambazo ziliagizwamoja kwa moja kiwandani ALAF ilisababisha mradi kus...

MRADI WA MITI KUKIINGIZIA CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA CHA MBIFACU MILIONI 553

Chama kikuu cha ushirika MBIFACU mjini Mbinga CHAMA Kikuu cha Ushirika cha Wilaya za Mbinga na Nyasa(MBIFACU) kimeanzisha shamba la miti la Kitelea mjini Mbinga lenye ukubwa wa hekari 39 lililopo kando kando ya barabara iendayo Mbambabay wilayani Nyasa. Kaimu Meneja wa MBIFACU Henrick Ndimbo amesema chama hicho kimeanzisha shamba hilo kwa lengo la kujiongezea mapato na kuimarisha ushirika kutokana na maelekezo ya serikali ya awamu ya Tano yenye lengo la kufufua ushirika nchini. Ndimbo amesema kupitia shamba hilo,katika msimu wa mwaka 2019/2020 MBIFACU imefanikiwa kuuza miti 118 yenye thamani ya shilingi 2,360,000/= na kwamba fedha hizo ziliingizwa kwenye mapato ya chama ili kuweza kusaidia uendeshaji wa shughuli mbalimbali za chama. “Mpango mkakati wa mwaka 2020/2021 ni uvunaji wa miti kwa hekari 30 na uchanaji wa mbao ambazo zinatarajia kutuingizia kipato cha shilingi milioni 553,630,000/= baada ya kutoa gharama zote za uendeshaji,ikiwa ni moja ya juhudi za kuongeza mapato...

AMCOS ya Kimuli Mbinga yatoa milioni 100 kuchangia miradi ya maendeleo

Ofisi cha chama cha Ushirika cha msingi Kimuli Mbinga CHAMA cha Ushirika cha msingi kimuli,kilichopo kijiji cha Utiri, kata ya Utiri Wilayani Mbinga mkoani Ruvuma, kimetoa sh. milioni 100, kwa kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika kata ya Kitanda, Utiri na Kihangi mahuka. Hayo yamesemwa na Meneja wa Chama hicho Ernest Komba, wakati akisoma Taarifa ya utendaji kazi wa Chama hicho, Katika Ziara ya kukagua Shughuli za Chama hicho cha Msingi iliyofanywa na Viongozi wa Chama kikuu cha Ushirika Mbinga (MBIFACU) na viongozi wa ushirika ngazi ya Mkoa wa Ruvuma. Komba amesema kuwa fedha hizo zilizotolewa na Chama cha kimuli, zilitokana na mapato ya premium na ziada, za Ndani na kusaidia ukarabati wa majengo ya Taasisi za elimu na Afya, zilizomo katika maeneo yanayohudumiwa na Chama cha kimuli. Ameitaja miradi iliyopewa fedha na chama hicho kuwa ni Zahanati ya Lipumba sh. milioni 14 ,Zahanati ya Kitanda milioni 9.5, Zahanati ya Utiri milioni saba na S...

UKIWA NA MSAIDIZI MWEUPE HATA UKIWA NA STRESS ZINAPUNGUA-JPM

Na Mwandishi Wetu,Site Tv Dodoma,Tanzania Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Taifa, wamempitisha Ndugu John Pombe Magufuli kuwa mgombea Urais 2020-2025 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM kwa kura 1,822. Mkutano huo umefanyika Julai 11,2020 kwenye ukumbi wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma na kuhudhiriwa na wajumbe wa kamati kuu pamoja na wageni mbalimbali waalikwa kutoka nje na ndani ya Nchi. Akitangaza matokeo ya kura hizo Mmoja wa wasimamizi wa uchaguzi Ndg. Job Ndugai amesema idadi ya wajumbe waliohudhuri ni 1,822 na hakuna kura iliyoharibika hivyo ameshinda kwa asilimia 100. Hivyo,rasmi CCM imekamilisha mchakato wa kupata wagombea kwa ngazi ya Urais ambapo kwa Zanzibar atasimama Hussein Mwinyi na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atasimama Rais Magufuli anayeingia katika awamu yake ya pili. Aidha, Dkt. John Pombe Magufuli amemchagua Mama Samia Suluhu Hassan kuwa mgombea mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ...

SHULE YA SEKONDARI ISACK KAMWELWE YAJA NA MFUMO WA KUTATUA UHABA WA WALIMU WA MASOMO YA SAYANSI,TANESCO KUMALIZA TATIZO LA UMEME KATA YA NSENKWA.

Na Aidan Felson,Site Tv Mlele,Katavi. Wizara ya Nishati kupitia Shirika la Umeme TANESCO Mkoa wa Katavi,inatarajia kumaliza tatizo la Umeme kwa kuhakikisha Wananchi wa Kata ya Nsenkwa iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mlele wanaunganishiwa Umeme. Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa Nishati Mh. Subira Mgalu katika ziara yake kikazi ya Siku Mbili Mkoani Katavi,alipokuwa katika Kata hiyo katika zoezi la kuwasha Umeme rasmi katika baadhi ya Kaya katika Kata hiyo. "Na Mimi naomba nikutaarifu,Vijiji vyako vilivyosalia pamoja na Vitongoji vyake,tunatarajia kupata Wakandarasi Mwezi wa Nane,Mwezi wa Tisa utakapokuja kunadi Ilani ya Uchaguzi ya 2020/2025,we jimwage Mzee kwa raha zako"-Naibu Waziri wa Nishati Mh. Subira Mgalu akimhakikishia Waziri Kamwelwe kumletea Umeme katika Vijiji vyote vya Kata ya Nsenkwa. Naibu Waziri wa Nishati Mh. Subira Mgalu akihutubia. Mh. Mgalu pia amewaomba wawekezaji kuwekeza katika Mkoa wa Katavi kwa kuwa ni Mkoa ambao umefunguliwa na neem...

UGOMVI BAINA YA WATEULE WA RAIS INAVYOMHUZUNISHA RAIS-JAFO.

Nteghenjwa Hosseah, OR- TAMISEMI WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Selemani Jafo amewataka wateule wa Rais kuwa na mahusiano mazuri kazini na kusisitiza kuwa Rais John Magufuli anahuzunishwa na wateule wake kugombana badala ya kufanya kazi.  Jafo ametoa rahi hiyo kwa wateule 22 wa Rais, wakiwamo wakuu wa mikoa wawili, katibu tawala wa mkoa mmoja, wakuu wa wilaya 10 na wakurugenzi wa halmashauri nane ambao wameteuliwa na kuapishwa juzi Ikulu ya Chamwino Dodoma wakati wa kuwakabidhi nyenzo za kufanyia kazi.  Alisema suala la kuimarisha mahusiano kazini kati ya wateule na watumishi walio chini yao na kuwa Rais hafurahishwi na namna wanavyogombana badala ya kufanya kazi.  “Haipendezi kukuta, mkuu wa mkoa anagombana na mkuu wa wilaya, au mkurugenzi  na mkuu wa wilaya kazi haziendi kwasababu ya ugomvi wenu, kusema ukweli sitarajii viongozi nyinyi ambao Rais amewateua ili msaidie majukumu kuwaita kwenye vikao kwa...

NAIBU WAZIRI WA NISHATI ASHITUSHWA NA GHARAMA ZA UENDESHAJI WA SHIRIKA LA TANESCO MKOA WA KATAVI.

Na Aidan Felson,Site Tv Mpanda,Katavi. Serikali ya Tanzania kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) awamu ya Tatu Mzunguko wa Kwanza,inatarajia kuwaunganishia Wateja wa Umeme wapatao 10,665 katika Vijiji 113 vya Wilaya zote Tatu za Mkoa wa Katavi. Akisoma taarifa kwa Naibu Waziri wa Nishati Mh. Subira Khamis Mgalu (MB),Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mh. Rachel Kasanda alisema,Mradi huo kabambe wa Umeme unaotekelezwa na Kampuni ya CHINA RAILWAY CONSTRUCTION ELECTRIFICATION BUREAU GROUP (CRCEBG) ulianza Mwezi Februali,2019 kwa Gharama ya Tsh. Bilioni 43.1 na umefikia Asilimia 58.35. Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mh. Rachel Kasanda (Mkuu wa Wilaya ya Mlele). "Na mpaka sasa hivi kazi inaendelea na ipo Asilimia 58.35,Jumla ya Mawanda wa mradi njia ndogo wenye Kilomita 551.2 na Jumla ya Mawanda Scop ya njia kubwa ni Kilomita 586.34 kulingana na Mawanda ya mradi wa REA awamu ya Tatu Mzunguko wa Kwanza ulivyoainisha"-Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mh. Rachel Kasanda. Kwa...

MBIFACU KUKARABATI HOTELI WILAYANI MBINGA KUFIKIA VIWANGO VYA KIMATAIFA.

Muonekano wa hoteli ya MBICU utakapokamilika ukarabati wake ambao unafanyika kwa miaka mitatu. CHAMA Kikuu cha Ushirika Wilaya ya Mbinga Nyasa (MBIFACU) Mkoani Ruvuma kimeanza  mradi wa ukarabati wa  hoteli ya MBICU ambayo inamilikiwa na chama hicho ili iweze kuwa na  viwango vya kimataifa. Alisema ukarabati wa hoteli hiyo ambao umeanza mwaka wa fedha wa 2019/2020 unatarajia kukamilika baada ya miaka mitatu na kwamba katika kutekeleza mradi huo zaidi ya shilingi bilioni moja zitatumika. Hata hivyo alisema ukarabati wa hoteli hiyo unafanyika kwa awamu ambapo katika awamu ya kwanza yanajengwa majengo sita na kujenga uzio ambao utazunguka eneo lote la hoteli hiyo. “Eneo hili litakuwa majengo 15 pamoja na jengo la hoteli,majengo yote yataezuliwa na kuezekwa katika mtindo wa kisasa  ili kukidhi viwango vya kimataifa na kuvutia wageni wa ndani na nje ya nchi’’,alisisitiza  Ndimbo. Kaimu Meneja wa MBIFACU Henerick Ndimbo akitoa maelezo ya ukarabati wa hoteli...

KANISA LA FPCT KATAVI LATOA MAFUNZO KWA WALEMAVU JUU KUJIKINGA NA VIRUSI VYA CORONA.

Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mpanda-Katavi. Watu wenye ulemavu Mkoani Katavi,wamelishukuru kanisa la FPCT kwa kuwapatia mafunzo ya Elimu Jumuishi dhidi ya kujikinga na Virusi vya Corona yaliyotolewa kwa viongozi wanaosimamia watu wenye ulemavu kupitia vyama vyao  yaani TAS, CHAVITA, CHAWATA,TLB na TAMS. Wakizungumza baadhi ya viongozi hao baada ya kupata mafunzo Ndg. Isack Lukas Mlela (Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Wasioona Mkoani Katavi (SHIVYAWATA) amesema mafunzo hayo yatawasaidia Watu wenye ulemavu huku akiyashukuru mashirika kwa kuanza kutambua uwepo wa Walemavu na amesema changamoto yao kubwa ilikuwa ni kujua namna ya kujikinga na maradhi hayo. "Katika Mafunzo haya ya Leo yametusaidia Sana sisi walemavu kuyafahamu ili yaweze kuwasaidia pia familia zetu na wenye ulemavu wengine kutoka katika mafunzo haya kadri ya uelimishaji tutakapofanya huko tunapoishi pamoja na wenzetu,lakini hili ni jambo muafaka kabisa ambalo kweli mashirika yameanza kututambua wat...

WAZIRI MKUU ATANGAZA NEEMA KWA VIJANA MKOANI KATAVI,BANDARI YA KAREMA KUFUNGUA MILANGO YA FURSA.

Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa ameagiza hadi kufikia Julai 25 Mwaka huu Shirika la Bandari,Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),Idara ya Uhamiaji,Jeshi la Polisi,Wizara ya Madini na Tasac wahakikishe wanajenga Mabanda eneo la Karema Wilayani Tanganyika Mkoani Katavi inapojengwa Bandari. Maagizo hayo ameyatoa Julai 4,2020 wakati akihutubia Wananchi wa Kata ya Karema baada ya kuzindua kwa kuweka jiwe la msingi Ujenzi wa Bandari ya Karema ambayo inajengwa na Serikali kwa kiasi cha zaidi ya Tsh. Bilioni 47. Waziri Mkuu amesema,Mabanda hayo ni kwa lengo la kujiweka tayari kwaajili ya kupokea wageni kutoka Nchi jirani ya Congo ambayo ndiyo Nchi washirika wakubwa wa Bandari hiyo,ili watakapo wasili eneo hilo taratibu zote zifuatwe zikiwemo za kikodi na kiusalama. "Hamtaweza kuanza kwa maagizo haya kujenga jengo la matofali,lakini jenga Mabanda yale,ya wakandarasi yale pale,myapange vizuri ili wageni wetu wooote kutoka Congo wakifika,anafika kwanza Uhamiaji,akishama...