Skip to main content

UKIWA NA MSAIDIZI MWEUPE HATA UKIWA NA STRESS ZINAPUNGUA-JPM


Na Mwandishi Wetu,Site Tv

Dodoma,Tanzania

Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Taifa, wamempitisha Ndugu John Pombe Magufuli kuwa mgombea Urais 2020-2025 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM kwa kura 1,822.

Mkutano huo umefanyika Julai 11,2020 kwenye ukumbi wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma na kuhudhiriwa na wajumbe wa kamati kuu pamoja na wageni mbalimbali waalikwa kutoka nje na ndani ya Nchi.

Akitangaza matokeo ya kura hizo Mmoja wa wasimamizi wa uchaguzi Ndg. Job Ndugai amesema idadi ya wajumbe waliohudhuri ni 1,822 na hakuna kura iliyoharibika hivyo ameshinda kwa asilimia 100.

Hivyo,rasmi CCM imekamilisha mchakato wa kupata wagombea kwa ngazi ya Urais ambapo kwa Zanzibar atasimama Hussein Mwinyi na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atasimama Rais Magufuli anayeingia katika awamu yake ya pili.

Aidha, Dkt. John Pombe Magufuli amemchagua Mama Samia Suluhu Hassan kuwa mgombea mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama hicho.

Magufuli amesema katika kipindi cha miaka mitano alichofanya kazi na Mama Samia kama makamu wa Rais amejifunza mengi na ameamua kuendelea naye katika awamu ya pili.

"Nilipomteua Mama Samia kuwa Makamu wa Rais mwaka 2015 sikuujua utendaji kazi wake vizuri lakini ni mchapakazi,anajituma pia ni mzuri,Wasukuma tunapenda weupe,ukiwa na Msaidizi mweupe hata ukiwa na stress zinaisha,nimeamua awe tena Mgombea mwenza"-Dkt. JPM kwenye Mkutano Mkuu Dodoma leo Julai 11,2020.

''Kwa kipindi nilichofanya kazi na Mama Samia nimejifunza mambo mengi sana na kupitia yeye nawahikikishia nitakuwa mtetezi mzuri wa wanawake. Nimekuwa nikimtuma popote hakatai kama na nyie kina Mama mkitumwa hamkatai"-Amesema JPM

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja