Skip to main content

UKIWA NA MSAIDIZI MWEUPE HATA UKIWA NA STRESS ZINAPUNGUA-JPM


Na Mwandishi Wetu,Site Tv

Dodoma,Tanzania

Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Taifa, wamempitisha Ndugu John Pombe Magufuli kuwa mgombea Urais 2020-2025 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM kwa kura 1,822.

Mkutano huo umefanyika Julai 11,2020 kwenye ukumbi wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma na kuhudhiriwa na wajumbe wa kamati kuu pamoja na wageni mbalimbali waalikwa kutoka nje na ndani ya Nchi.

Akitangaza matokeo ya kura hizo Mmoja wa wasimamizi wa uchaguzi Ndg. Job Ndugai amesema idadi ya wajumbe waliohudhuri ni 1,822 na hakuna kura iliyoharibika hivyo ameshinda kwa asilimia 100.

Hivyo,rasmi CCM imekamilisha mchakato wa kupata wagombea kwa ngazi ya Urais ambapo kwa Zanzibar atasimama Hussein Mwinyi na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atasimama Rais Magufuli anayeingia katika awamu yake ya pili.

Aidha, Dkt. John Pombe Magufuli amemchagua Mama Samia Suluhu Hassan kuwa mgombea mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama hicho.

Magufuli amesema katika kipindi cha miaka mitano alichofanya kazi na Mama Samia kama makamu wa Rais amejifunza mengi na ameamua kuendelea naye katika awamu ya pili.

"Nilipomteua Mama Samia kuwa Makamu wa Rais mwaka 2015 sikuujua utendaji kazi wake vizuri lakini ni mchapakazi,anajituma pia ni mzuri,Wasukuma tunapenda weupe,ukiwa na Msaidizi mweupe hata ukiwa na stress zinaisha,nimeamua awe tena Mgombea mwenza"-Dkt. JPM kwenye Mkutano Mkuu Dodoma leo Julai 11,2020.

''Kwa kipindi nilichofanya kazi na Mama Samia nimejifunza mambo mengi sana na kupitia yeye nawahikikishia nitakuwa mtetezi mzuri wa wanawake. Nimekuwa nikimtuma popote hakatai kama na nyie kina Mama mkitumwa hamkatai"-Amesema JPM

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...