Skip to main content

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO





Na Swaumu Katambo, Katavi

Wafanyabiashara wadogo katika stendi ya mabasi Mizengo Pinda wameiomba Serikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuepukana na adha ya kulipa ushuru wa Halmashauri ambao una gharama kubwa.

Wakizungumza na Site Tv wajasiriamali Mjini Mpanda wameilalamikia Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Mpanda Michael Nzyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kucheleweshwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki.

Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote.

MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja

Katavi Yakemea Vikali Ushoga,Mauaji "Wanaume Msiwazuie Wake Zenu Kufanya...