Skip to main content

UGOMVI BAINA YA WATEULE WA RAIS INAVYOMHUZUNISHA RAIS-JAFO.


Nteghenjwa Hosseah, OR- TAMISEMI

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Selemani Jafo amewataka wateule wa Rais kuwa na mahusiano mazuri kazini na kusisitiza kuwa Rais John Magufuli anahuzunishwa na wateule wake kugombana badala ya kufanya kazi. 

Jafo ametoa rahi hiyo kwa wateule 22 wa Rais, wakiwamo wakuu wa mikoa wawili, katibu tawala wa mkoa mmoja, wakuu wa wilaya 10 na wakurugenzi wa halmashauri nane ambao wameteuliwa na kuapishwa juzi Ikulu ya Chamwino Dodoma wakati wa kuwakabidhi nyenzo za kufanyia kazi. 

Alisema suala la kuimarisha mahusiano kazini kati ya wateule na watumishi walio chini yao na kuwa Rais hafurahishwi na namna wanavyogombana badala ya kufanya kazi. 

“Haipendezi kukuta, mkuu wa mkoa anagombana na mkuu wa wilaya, au mkurugenzi  na mkuu wa wilaya kazi haziendi kwasababu ya ugomvi wenu, kusema ukweli sitarajii viongozi nyinyi ambao Rais amewateua ili msaidie majukumu kuwaita kwenye vikao kwa mambo ambayo ninyi wenyewe mnaweza kumaliza. “ 

Jueni kuwa mmechaguliwa si kwa upendeleo bali kwa uwezo wenu wa kufanya kazi na mmepewa kipande cha kumsaidia Rais kuwatumikia wananchi hivyo mkafanye kazi, kumbukeni kuwa mheshimiwa Rais (John Magufuli) hafurahishi na hali ya migogoro baina ya wateule wake au na watumishi.” 

Jafo alisema ili kuondokana na migongano baina yao wanayopaswa  kufanya ni kuzingatia na kuheshimu mipaka yao ya kazi. “ 

Kila mtu akafanye kazi katika mipaka yake ya kazi, sio muende huko mkuu wa mkoa anawaza kumfunika mkuu wa wilaya, au mkuu wa wilaya anataka kumfunika mkuu wa mkoa, na matatizo haya yako sana kwenye maeneo ya mijini na ndio maana unaona hata kufungua choo kimoja anataka kwenda Mkuu wa mkoa, mkaheshimu na kuzingatia mipaka yenu ya kazi.”-Alisema Waziri Jafo
Aidha, Jafo amewataka viongozi hao kuwa na nidhamu na kuhakikisha watumishi walio chini yao wanafanyia kazi kwa nidhamu katika nyanja zote na kusisitiza kuwa ufanyaji kazi kwa mazoea halikubaliki. 

Pia amewataka kuzingatia maadili ya viongozi wa umma  katika nyanja zote na kuwahimiza wanapofika kwenye maeneo yao ya kazi wasiende kutengeneza maadui bali marafiki ambao watafanya kazi kwa ushirikiano.

Mhe. Jafo pia amesisitiza viongozi hao kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika vita ya kupambana na dawa za kulevya katika maeneo yao

“Serikali haitaki kuona wananchi wake badalaya ya kufanya kazi wanajikita katika matumizi ya dawa za kulevya, ushiriki wa wananchi katika kufanya kazi pia kumechangia Tanzania kufika kwenye uchumi wa kati hata kabla ya muda tuliojiowekea, hivyo vita ya dawa za kulevya ni ya viongozi katika ngazi zote, hakikisheni mnalisimamia hilo.”-Alisema Mh. Jafo

Jafo pia alisema viongozi hao wanapaswa kuhakikisha hoja za ukaguzi za CAG zinajibiwa kwa wakati na kusisitiza kuwa hataki kusikia halmashauri inakuwa na hati chafu hasa ikizingatia kuwa kazi kubwa imefanyika mpaka kufanya taarifa ya cag ya hivi karibuni inaonesha kuwa asilimia 95 Ni hati safi na asilimia 5 zinamashaka.

Jafo wamewasisitizs viongozi hao katika kuhakikisha wanasimamia mkusanyo ya mapato na matumizi ya fedha za ndani.

Pia amewataka kuhakikisha asilimia 10 zinazopelekwa kwa vijana, wanawake na wenye ulemvu zinawafikia walengwabna kuwa kinyume chake ni kukiuka Sheria kwasababu suala liko kisheria.

 (Mwisho)

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...