Skip to main content

SHULE YA SEKONDARI ISACK KAMWELWE YAJA NA MFUMO WA KUTATUA UHABA WA WALIMU WA MASOMO YA SAYANSI,TANESCO KUMALIZA TATIZO LA UMEME KATA YA NSENKWA.


Na Aidan Felson,Site Tv

Mlele,Katavi.

Wizara ya Nishati kupitia Shirika la Umeme TANESCO Mkoa wa Katavi,inatarajia kumaliza tatizo la Umeme kwa kuhakikisha Wananchi wa Kata ya Nsenkwa iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mlele wanaunganishiwa Umeme.

Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa Nishati Mh. Subira Mgalu katika ziara yake kikazi ya Siku Mbili Mkoani Katavi,alipokuwa katika Kata hiyo katika zoezi la kuwasha Umeme rasmi katika baadhi ya Kaya katika Kata hiyo.

"Na Mimi naomba nikutaarifu,Vijiji vyako vilivyosalia pamoja na Vitongoji vyake,tunatarajia kupata Wakandarasi Mwezi wa Nane,Mwezi wa Tisa utakapokuja kunadi Ilani ya Uchaguzi ya 2020/2025,we jimwage Mzee kwa raha zako"-Naibu Waziri wa Nishati Mh. Subira Mgalu akimhakikishia Waziri Kamwelwe kumletea Umeme katika Vijiji vyote vya Kata ya Nsenkwa.
Naibu Waziri wa Nishati Mh. Subira Mgalu akihutubia.

Mh. Mgalu pia amewaomba wawekezaji kuwekeza katika Mkoa wa Katavi kwa kuwa ni Mkoa ambao umefunguliwa na neema imeingia,huku akiwataka Wananchi ambao hawajaunganishiwa Umeme kuwa wavumilivu kwa kuwa zoezi hilo linafanyika kwa awamu.

"Naomba niwaombe wawekezaji wote,Mkoa wa Katavi ni Mkoa ambao umefunguliwa,Mkoa wa Katavi ni Mkoa ambao Neema imeingia,neema ya miundombinu ya Barabara,neema ya Miundombinu ya anga,Mi mwenyewe nimefurahi,nimefika na Ndege hapa"-Mh. Mgalu,Naibu Waziri wa Nishati.

Kwa upnde wake Mbunge wa Jimbo la Katavi na Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Aloyce Kamwelwe alisema Vijiji ambavyo havijapata Umeme ni Mapili,Ilunde,Isegenezya na Masiko na ameishukuru Wizara ya Nishati kwa kukubali kuleta Nguzo 40 katika Kijiji cha Mgombe ambazo zinafika Mwezi ujao.

Pichani ni Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Aloyce Kamwelwe  na Naibu Waziri wa Nishati Mh. Subira Mgalu akitoa ufafanuzi kuhusu Mfumo unaofungwa katika Shule ya Sekondari Isack Kamwelwe utakavyokuwa.

Aidha,katika kuhakikisha Nishati inapatikana ili Wanafunzi wapate muda wa kujisomea muda wote,Mh. Kamwelwe amechangia Tsh. Milioni Moja kwa ajili ya kufanya Wiring katika Shule ya Sekondari Isack Kamwelwe,na alisema hadi sasa Shule hiyo inafungwa Mtambo wa Teleconference utakao tatua tatizo la ukosefu wa Walimu wa Masomo ya Sayansi kwa kuwa Mfumo huo utaunganishwa na Walimu wa masomo hayo.

"Huyu Bwana (Meneja wa TTCL) ndiye anayetuletea Teleconference hapa,ameshanunua vifaa vyote,na ile Optic fiber amenunua,ilikuwa wafunge upande wa TANESCO lakini sasa conectivity ime fail,kwasababu lazima tuje na hii Barabara ya Lami,kwahiyo wanaleta nguzo 150,ukikamilika tunafunga sceen hapa,tunaanza kufanya E-Education,kwahiyo itaondoa changamoto ya Walimu wa Sayansi hawapo,Walimu wa Hesabu hawapo,Moja tutaunganisha na Dar Es Salaam Institute Of Technology"-Mhandisi Kamwelwe,Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano.

Pichani ni Naibu Waziri wa Nishati Mh. Subira Mgalu akiwa na Waziri wa  Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Aloyce Kamwelwe wakifurahia jambo.
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Isack Kamwelwe.
Wananchi wakifatilia Mkutano wa Naibu Waziri wa Nishati.

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja