Skip to main content

SHULE YA SEKONDARI ISACK KAMWELWE YAJA NA MFUMO WA KUTATUA UHABA WA WALIMU WA MASOMO YA SAYANSI,TANESCO KUMALIZA TATIZO LA UMEME KATA YA NSENKWA.


Na Aidan Felson,Site Tv

Mlele,Katavi.

Wizara ya Nishati kupitia Shirika la Umeme TANESCO Mkoa wa Katavi,inatarajia kumaliza tatizo la Umeme kwa kuhakikisha Wananchi wa Kata ya Nsenkwa iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mlele wanaunganishiwa Umeme.

Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa Nishati Mh. Subira Mgalu katika ziara yake kikazi ya Siku Mbili Mkoani Katavi,alipokuwa katika Kata hiyo katika zoezi la kuwasha Umeme rasmi katika baadhi ya Kaya katika Kata hiyo.

"Na Mimi naomba nikutaarifu,Vijiji vyako vilivyosalia pamoja na Vitongoji vyake,tunatarajia kupata Wakandarasi Mwezi wa Nane,Mwezi wa Tisa utakapokuja kunadi Ilani ya Uchaguzi ya 2020/2025,we jimwage Mzee kwa raha zako"-Naibu Waziri wa Nishati Mh. Subira Mgalu akimhakikishia Waziri Kamwelwe kumletea Umeme katika Vijiji vyote vya Kata ya Nsenkwa.
Naibu Waziri wa Nishati Mh. Subira Mgalu akihutubia.

Mh. Mgalu pia amewaomba wawekezaji kuwekeza katika Mkoa wa Katavi kwa kuwa ni Mkoa ambao umefunguliwa na neema imeingia,huku akiwataka Wananchi ambao hawajaunganishiwa Umeme kuwa wavumilivu kwa kuwa zoezi hilo linafanyika kwa awamu.

"Naomba niwaombe wawekezaji wote,Mkoa wa Katavi ni Mkoa ambao umefunguliwa,Mkoa wa Katavi ni Mkoa ambao Neema imeingia,neema ya miundombinu ya Barabara,neema ya Miundombinu ya anga,Mi mwenyewe nimefurahi,nimefika na Ndege hapa"-Mh. Mgalu,Naibu Waziri wa Nishati.

Kwa upnde wake Mbunge wa Jimbo la Katavi na Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Aloyce Kamwelwe alisema Vijiji ambavyo havijapata Umeme ni Mapili,Ilunde,Isegenezya na Masiko na ameishukuru Wizara ya Nishati kwa kukubali kuleta Nguzo 40 katika Kijiji cha Mgombe ambazo zinafika Mwezi ujao.

Pichani ni Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Aloyce Kamwelwe  na Naibu Waziri wa Nishati Mh. Subira Mgalu akitoa ufafanuzi kuhusu Mfumo unaofungwa katika Shule ya Sekondari Isack Kamwelwe utakavyokuwa.

Aidha,katika kuhakikisha Nishati inapatikana ili Wanafunzi wapate muda wa kujisomea muda wote,Mh. Kamwelwe amechangia Tsh. Milioni Moja kwa ajili ya kufanya Wiring katika Shule ya Sekondari Isack Kamwelwe,na alisema hadi sasa Shule hiyo inafungwa Mtambo wa Teleconference utakao tatua tatizo la ukosefu wa Walimu wa Masomo ya Sayansi kwa kuwa Mfumo huo utaunganishwa na Walimu wa masomo hayo.

"Huyu Bwana (Meneja wa TTCL) ndiye anayetuletea Teleconference hapa,ameshanunua vifaa vyote,na ile Optic fiber amenunua,ilikuwa wafunge upande wa TANESCO lakini sasa conectivity ime fail,kwasababu lazima tuje na hii Barabara ya Lami,kwahiyo wanaleta nguzo 150,ukikamilika tunafunga sceen hapa,tunaanza kufanya E-Education,kwahiyo itaondoa changamoto ya Walimu wa Sayansi hawapo,Walimu wa Hesabu hawapo,Moja tutaunganisha na Dar Es Salaam Institute Of Technology"-Mhandisi Kamwelwe,Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano.

Pichani ni Naibu Waziri wa Nishati Mh. Subira Mgalu akiwa na Waziri wa  Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Aloyce Kamwelwe wakifurahia jambo.
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Isack Kamwelwe.
Wananchi wakifatilia Mkutano wa Naibu Waziri wa Nishati.

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...