Skip to main content

MRADI WA MITI KUKIINGIZIA CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA CHA MBIFACU MILIONI 553

Chama kikuu cha ushirika MBIFACU mjini Mbinga

CHAMA Kikuu cha Ushirika cha Wilaya za Mbinga na Nyasa(MBIFACU) kimeanzisha shamba la miti la Kitelea mjini Mbinga lenye ukubwa wa hekari 39 lililopo kando kando ya barabara iendayo Mbambabay wilayani Nyasa.

Kaimu Meneja wa MBIFACU Henrick Ndimbo amesema chama hicho kimeanzisha shamba hilo kwa lengo la kujiongezea mapato na kuimarisha ushirika kutokana na maelekezo ya serikali ya awamu ya
Tano yenye lengo la kufufua ushirika nchini.

Ndimbo amesema kupitia shamba hilo,katika msimu wa mwaka 2019/2020 MBIFACU imefanikiwa kuuza miti 118 yenye thamani ya shilingi 2,360,000/= na kwamba fedha hizo ziliingizwa kwenye mapato ya chama ili kuweza kusaidia uendeshaji wa shughuli mbalimbali za
chama.

“Mpango mkakati wa mwaka 2020/2021 ni uvunaji wa miti kwa hekari 30 na uchanaji wa mbao ambazo zinatarajia kutuingizia kipato cha shilingi milioni 553,630,000/= baada ya kutoa gharama zote za uendeshaji,ikiwa ni moja ya juhudi za kuongeza mapato ya ndani ya chama ili kiweze kujitegemea’’,alisisitiza Ndimbo.

Ndimbo ametoa rai kwa Taasisi zote kushirikiana na MBIFACU katika kutekeleza na kusimamia mfumo wa ushirika kwa sababu ndiyo mkombozi wa wakulima ambao unaweza kuwanufaisha wakulima,endapo mfumo wa ushirika utasimamiwa vizuri kupitia wataalam.

Amesisitiza kuwa ushirika utaongeza uzalishaji kwa kuongeza kipato cha wakulima moja kwa moja na kuongeza mapato ya Halmashauri ya serikali kwa ujumla.

Kwa upande wake Kaimu Mwenyekiti wa MBIFACU Winfred Lupembe
amesema shamba la miti la Kitelea ni la miti ya zamani ambapo MBIFACU imeamua kuliboresha shamba hilo kwa kuvuna miti yote kwamatumizi ya mbao na kuni na kwamba baada ya kukamilisha kazi yakuvuna,MBIFACU inatarajia kupanda miti upya kibiashara na kuingiza mapato makubwa zaidi.

Lupembe amesisitiza kuwa zoezi la uvunaji miti ya zamani na kupanda miti mipya linaendelea ambapo katika eneo hilo tayari imepandwa mitimipya 600 na kwamba shamba la miti linalomilikiwa na MBIFACU,ukitembea kwa mguu unaweza kutembea kwa saa mbili na nusu kuzunguka shamba lote.
Sehemu ya miti katika shamba la miti Kitelea Mbinga lenye ukubwa wa hekari 39 linalomilikiwa na MBIFACU

Amesema miti yote ambayo ilipandwa katika shamba la miti la Kitelea ilishavunwa na kwamba miti iliyopo hivi sasa ni michipukizi ya miti zamani ambayo pia inavunwa kwa ajili ya mbao za kuendeleza mradi wa ukarabati wa hoteli ya MBICU kuwa katika viwango vya kimataifa.

Imeandikwa na Albano Midelo
Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...