Skip to main content

Posts

Showing posts from May, 2021

Madiwani Tutengeneze Mshikamano//Tusionyane kwa Kukomoana.

Fedha za Stakabadhi Ghalani zajenga Kituo cha Afya.

Cheyo aeleza Utekelezaji Mradi wa Maabara//DC-"Biashara Asubuhi"

Mradi wa Maji wakamilika//Umeme kikwazo Wananchi kuanza kutumia.

"Niwepo nisiwepo,Hii Kazi ikamilike,Iwe katika Ufasaha ninaoutaka"-DC Mlele

"Serikali itaongeza ambavyo havipo,Vilivyopo tuvisimamie kwa wakati vien...

WAKAMATWA KWA KUJIHUSISHA NA MATUKIO YA MAUAJI,KUJERUHI.

  Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watuhumiwa 5 kwa tuhuma za kujihusisha na matukio ya mauaji,kujeruhi na kuingiza bidhaa Nchini bila kulipia ushuru. Kuhusu taarifa za Mauaji,Jeshi la Polisi Mkoani humo limesema Watuhumiwa Watatu ambao ni Lusajo Mwaijobelo (32),Naboti Sanga (44) na Christina Chaula (50) wote wakazi wa Kisyosyo-Matema Wilaya ya Kyela,wanashikiliwa kwa tuhuma za tukio la mauaji ya Mwanamke aitwaye Elizabeth Mwaike (22) Mkazi wa Kisyosyo. Watuhumiwa wamekamatwa Mei 28,2021 majira ya saa 18:30 jioni katika Kijiji cha Kisyosyo,Kata ya Matema,Tarafa ya Ntebela,Wilaya ya Kyela,Mkoani Mbeya,ambapo katika Machimbo ya Kokoto ya kampuni ya Kichina,Marehemu alikutwa eneo hilo akiwa ameuawa kwa kupigwa kitu kizito kichwani umbali wa mita 500 kutoka Nyumbani kwake. Chanzo cha tukio hilo kimeelezwa kuwa ni wivu wa kimapenzi na upelelezi wa shauri hili unaendelea na mara baada ya kukamilika watuhumiwa watafikishwa mahakamani. Katika tukio lingine,Jeshi la Polisi Mkoan...

Wananchi wa Kata ya Kibaoni kwa Waziri Mkuu mstaafu ni mfano wa Kuingwa ...

Wasimamishwa Kazi baada ya kulipana Posho.

Waziri Mkuu wa Tanzania,Kassim Majaliwa. Na Mwandishi Wetu Waziri mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amewasimamisha kazi mkaguzi mkuu,mkaguzi msaidizi na baadhi ya watendaji wa Wizara ya Fedha na Mipango kupisha uchunguzi wa tuhuma za matumizi mabaya ya fedha  za umma zinazowakabili. Taarifa kutoka ofisi ya waziri mkuu iliyotolewa leo Mei 28,2021 inaeleza kuwa katika kikao kazi na waziri wa fedha na mipango,katibu mkuu,manaibu katibu wakuu na watendaji waandamizi wa wizara hiyo mkoani Dodoma jana,Majaliwa amemuagiza mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa (Takukuru),Salum Hamdun kufanya uchunguzi kuhusu tuhuma hizo na ikithibitika si za kweli wahusika warejeshwe kazini. Majaliwa amezitaja tuhuma hizo kuwa ni malipo yaliyofanyika Machi 31,2021 kupitia vocha 30 ya TSh. Milioni 251 yakielezwa kuwa ni malipo maalum bila kutaja kazi maalum ni nini na nani aliifanya. Amebainisha kuwa siku hiyo hiyo pia zililipwa TSh. Milioni 198.8 kwa madai kuwa ni posho ya honoraria. ...

MKURUGENZI WA MPIMBWE APEWA MWEZI MMOJA KUREKEBISHA MILANGO YA HOSPITALI.

Mkuu wa Wilaya ya Mlele,Rachel Kasanda akitoa maelekezo ya jambo fulani. Mradi wa ujenzi wa Wodi 3 ikiwemo Wodi ya Watoto,Wanawake na Wanaume. Zahanati ya Mirumba inayojengwa. Nyumba ya Mkurugenzi inayojengwa. Nyumba za Wakuu wa Idara.  Picha na Swaum Katambo. Na Swaum Katambo,Mpimbwe-Katavi. Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda Jana Mei 27,2021 amefanya ziara ya kutembelea Miradi ya Ujenzi wa Zahanati ya Mirumba iliyopo Kata ya Kibaoni,Ujenzi wa Wodi Tatu ya Watoto,Wanawake na Wanaume katika Hospitali ya Halmashauri na Ujenzi wa Nyumba Saba za Wakuu wa Idara na Vitengo na Uzio. Katika Ziara yake ya kukagua Ujenzi wa Zahanati ya Mirumba iliyogharimu kiasi cha Tsh. 46,953,000/- ambapo ndani yake kiasi cha Tsh.26,953,000/- zilitokana na michango ya nguvu za Wananchi ambapo DC Rachel Kasanda ametumia fursa hiyo kuwapongeza Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe kwa ushiriano wanao utoa kwa Serikali katika utekelezaji wa Miradi mbalimbali. "Huu ni mfano wa kuigwa hata katika H...

RAIA WA BURUNDI AMBAO NI WAFUGAJI WAMEVAMIA ARDHI YA TANZANIA WILAYANI KAKONKO MKOANI KIGOMA.

Raia wa Burundi waliokamatwa. Na Jastin Cosmas,Kakonko-Kigoma. Raia wa Burundi ambao ni Wafugaji,wamevamia ardhi ya Tanzania Wilayani Kakonko Mkoani Kigoma kwa kuweka Mifugo ya Ng’ombe kama sehemu ya kuchunga kitendo ambacho kimeleta sintofahamu kwa Wananchi wa Kata ya Gwanumpu. Sintofahamu hiyo imeibuka wakati Wananchi walipohoji katika mkutano wa hadhara ulio fanyika katika Kijiji cha Rusenga Kata ya Gwanumpu Wilayani Kakonko,ambapo wamelaani kitendo cha Mashamba yao kuvamiwa na Wafugaji kutoka Nchi ya Burundi huku mazao yao yakiharibiwa na Ng’ombe. Wananchi hao wamesema kuwa,Mwnyekiti wa Kijiji cha Rusenga Evarist Ndumiwe alitoa ardhi kwa Wafugaji wa Burundi bila kushirikisha Wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji hicho cha Rusenga.ambapo Wajumbe wa Kijiji hicho wamesema hawana imani na Mwenyekiti huyo. Nae mwenyekiti wa Kijiji hicho Evarist Ndumiwe ametupilia mbali lawama hizo, akisema kuwa ameingia kwenye uongozi Ng’ombe hao wakiwepo hivyo haja ruhusu Ng’ombe hao kuingia Tanzania. Kwa u...

"Ningekuwa na Uwezo ningewajengea Nyumba Waandishi wa Habari"-RC Homera,...

Madiwani wametakiwa kutoingilia Mfumo wa Usajili wanufaika wa TASAF.

Pichani ni Washiriki wa  kikao kazi cha kujenga uelewa wa Wadau juu ya awamu ya 3 ya Kipindi cha Pili cha Shughuli za TASAF,kikao kilicho wakutanisha Madiwani,Wataala,Wana Habari na Wawezeshaji. Picha na Elias Mlugala. Judith Woiso,Afisa Ufuatiliaji-TASAF,akitoa elimu kwa washiriki wa Semina. Zacharia Ngoma,Mwakilishi wa Mkurungenzi Mtendaji wa TASAF akitoa neno. Na Mwandishi Wetu,Site Tv. Madiwani wa Halimashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi wametakiwa kutoingilia mfumo wa usajili wa Wanufaika wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) ili kuondoa uingizaji wa Wanaufaika wasio na sifa. Wito huo umetolewa na Zacharia Ngoma,Mwakilishi wa Mkurungenzi Mtendaji wa TASAF katika kikao kazi cha Madiwani,Timu ya Wataalam kutoka TASAF Makao Makuu,Wana Habari na Wawezeshaji cha kujenga uelewa wa Wadau juu ya Sehemu ya Pili ya awamu ya 3 ya Shughuli za TASAF,kikao kilichofanyika katika Ukumbi wa Mtakatifu Mathias,uliopo Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi. "Vipo vigezo vya kuziingiza Kaya mas...

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Rais wa Zanzibar atamani Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kushirikiana na SKAUTI.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi akiwa na  Mkuu wa Chama cha SKAUTI Tanzania Mwantumu Bakari Mahiza. Na Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar. RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ameeleza haja kwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali ya Zanzibar kushirikiana vyema na Chama cha SKAUTI Tanzania ili kuwajengea vijana uwezo mzuri wa stadi za maisha pamoja na uzalendo. Rais Dk. Mwinyi aliyasema hayo leo, Ikulu Jijini Zanzibar wakati alipokutana na Uongozi wa Chama cha SKAUTI Tanzania ukiongozwa na kiongozi wake Mkuu Hajjat Mwantumu Bakari Mahiza akiwa amefuatana na viongozi kutoka Zanzibar. Alisema kuwa kuna vijana wengi wa SKAUTI waliohamasika katika chama hicho hapa Zanzibar hivyo, ni vyema Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali ikashirikiana na chama hicho katika kuhakikisha vijana hao wanatekelezewa mahitaji yao kutokana na shughuli wanazozifanya. Rais Dk. Mwinyi alieleza kuwa programu za vijana ambazo tayari z...

"Kwa Miaka hii takribani 9 sidhani kuna jipya kujiita Mkoa mpya"-RC Katavi.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Hoza Mrindoko katika Kikao na Watumishi wa Umma Mkoani Katavi cha kusalimiana na kufahamiana leo Mei 24,2021. Katibu Tawala Mkoa wa Katavi,Abdallah Mohammed Malela. Baadhi ya Watumishi wa Umma wakifatilia Hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi wakati wa Kikao cha kusalimiana na kufahamiana katika ukumbi wa Mpanda Manispaa. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mpanda-Katavi. Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi Ndg. Abdallah Malela amemweleza Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi.Mwanamvua Hoza Mrindoko kuwa Watumishi wa Mkoa wa Katavi wanafanya kazi kwa kujituma bila kujali Siku za Kazi na hawana changamoto zozote isipokuwa Mkoa unatatizo kubwa la Lishe na Matundu bora ya Vyoo. Ameyasema hayo wakati akimkaribisha Mkuu wa Mkoa huo Bi.Mwanamvua Hoza Mrindoko katika kikao na Watumishi wa Umma wa Mkoa wa Katavi,Kikao cha kusalimiana na kufahamiana kilichofanyika katika Ukumbi wa Mpanda Manispaa leo Mei 24,2021. Kwa upande wake RC Mrindoko ametumia nafasi hiyo kuwashukuru Watumishi wenzake k...

Kwa kazi Bora ya Video na Picha wasiliana nasi SITE DIGITAL MEDIA - 0765...

RC Mbeya Juma Homera atema Cheche//Ni wakati akikabidhiwa Ofisi.

JANE GOODALL YAWAJENGEA UWEZO WA ELIMU YA KUJITEGEMEA WANAFUNZI WILAYANI TANGANYIKA.

Mratibu wa Jane Goodall's Roots & Shoots Erasto Njavike akifafanua jamno. Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Salehe Mbwana Mhando akiwakabidhi Wanafunzi Mche wa Nanasi. Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika akisisitiza jambo. Na Swaum Katambo, Tanganyika-Katavi Taasisi ya Jane Goodall kupitia Mradi wa Roots & Shoots imetoa Mizinga ya Nyuki 135 na Mbegu za Matunda Tani 1 pamoja na Miche ya Matunda ya Nanasi,Papai,Machungwa na Limao kwenye Shule za Msingi na Sekondari zilizopo Wilayani Tanganyika Mkoani Katavi. Akizungumza mara baada ya kutoa Mizinga,Mbegu pamoja na Miche hiyo Mratibu wa Jane Goodall's Roots & Shoots Erasto Njavike kupitia mradi wa Roots & Shoots amesema,walipoadhimisha miaka 60 ya utafiti wa Jane Goodall Mwaka Jana 2020,Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Salehe Mhando alitamani kuona kila Shule iliyopo Wilayani humo inakuwa na Miradi hivyo mradi huo umetimiza kilio cha DC Mhando. Njavike Ameongeza kuwa wanaamini Vijana wataisimamia vizuri Miradi hiyo ya ufugaji wa Ny...

Afukuzwa Kazi kwa tuhuma za Wizi wa Dawa na Vifaa Tiba.

Mwenyekiti Mtata akutana na Maswali magumu

Maajabu,Karne hii Kijiji hakina Shule//Mpango wa haraka waanza.

Shuhudia Kilimo cha Nchi Kavu kinavyofanyika//Wananchi sasa kutajirika.

Mwenyekiti na Mtendaji wasimamishwa ili kupisha uchuguzi kwa tuhuma za ubadhilifi wa Fedha.

Pichani ni Mwenyekiti wa Kijiji cha Shukura Peter Colomery (Alie shika Shavu) na Mtendaji wa kijiji hicho Mesamo Megama . Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Salehe Mbwana Mhando. Na Zainab Mtima,Tanganyika-Katavi. Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika   Mkoani Katavi,Saleh Mhando amewasimamisha kazi Mwenyekiti wa Kijiji cha Shukura Peter Colomery na Mtendaji wa Kijiji hicho Mesamo Megama ili kupisha uchuguzi kufuatia tuhuma za ubadhilifi wa Fedha zilizochangwa na Wanakijiji kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Msingi Shukura. Mhando ametoa maagizo hayo katika mkutano wa hadhara na wakazi wa Kijiji hicho,ambapo awali walitoa kero zao mbele ya Mkuu wa Wilaya huyo na kuzipatia ufumbuzi na kuongeza kuwa   W atumishi hao watachunguzwa na taasisi ya kupambana na Rushwa TAKUKURU Wilayani Tanganyika. . Katika mkutano huo pia Mhando ameagiza Uongozi wa Kijiji hicho kuhakikisha ujenzi wa Shule ya Msingi Shukura kuanza kujengwa kuanzia June Mosi Mwaka huu. Hata hivyo ametoa tahadhali kwa Wananchi wais...

MANISPAA YA MPANDA KUTOA ELIMU YA KILIMO CHA NCHI KAVU.

Shamba la Mfano likiwa na Mazao mbalimbali ikiwemo  Mpunga wa Nchi kavu,Mahindi,Zao la strawberry, Bamia, Alizeti, Ufuta na mazao mengine ya Bustani kama Mchicha,chainizi,spinachi n.k. PICHA NA Swaum Katambo Mkuu wa Idara ya Kilimo,Umwagiliaji na  Ushirika Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Laurent Munyu akifafanua jambo. Na Swaum Katambo, Mpanda-Katavi Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda inatarajia kutenga bajeti kwa ajili ya kuanzisha mashamba ya mfano ya kilimo cha kisasa ambayo yatasaidia kutoa Elimu kwa jamii juu ya namna bora ya kufanya kilimo cha kisasa hasa maeneo yaliyopo mjini. Akizungumza leo Mei 21,2020 katika hitimisho la hatua ya utoaji wa Elimu ya Kilimo kwa wakulima wa Manispaa ya Mpanda na Mkoa wa Katavi kwa ujumla,Mkuu wa Idara ya Kilimo,Umwagiliaji na  Ushirika Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Laurent Munyu amesema pamoja na kuishi maeneo ya Mjini,Wananchi wanaweza kuandaa Mashamba na kulima Kilimo chenye tija. Munyu ameongeza kuwa wanachokifanya wanajar...

DC Mhando agoma Watendaji wa VIjiji kupewa uhamisho kabla hawajafanyiwa uchunguzi.

Baadhi ya Wananchi wakifatilia Mkutano wa hadhara. Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Salehe Mbwana Mhando,akiongea jambo mbele ya Wananchi katika Mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Shukura. Na Zainab Mtima, Tanganyika-Katavi Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Mkoani, Katavi   Saleh Mhando   ameagiza watendaji wote wa vijiji katika halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika   wanaoomba uhamisho,wasipewe uhamisho wowote   na badala yake warudi katika vituo vyao vya kazi na kufanyiwa uchunguzi kama kuna deni lolote la kijiji analodaiwa. Mhando ametoa agizo hilo alipokutana na Uongozi wa Kijiji cha Shukura ambapo Viongozi hao wamedai kuwepo na changamoto ya uhamishwaji wa ghafla kwa Watendaji wa Vijiji jambo linalowaachia madeni yasiyo ya lazima,kufuatia Watendaji hao kuondoka na michango ya Wananchi kwa ajili ya maendeleo ya Kijiji. Katika hatua nyingine Mhando ametoa Siku Saba kwa Uongozi wa Kijiji hicho kuhakikisha wanamaliza mgogoro wa eneo la ujenzi wa Shule ya Msingi Shuk...