Skip to main content

DC Mhando agoma Watendaji wa VIjiji kupewa uhamisho kabla hawajafanyiwa uchunguzi.

Baadhi ya Wananchi wakifatilia Mkutano wa hadhara.

Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Salehe Mbwana Mhando,akiongea jambo mbele ya Wananchi katika Mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Shukura.


Na Zainab Mtima,Tanganyika-Katavi

Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Mkoani, Katavi  Saleh Mhando  ameagiza watendaji wote wa vijiji katika halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika  wanaoomba uhamisho,wasipewe uhamisho wowote  na badala yake warudi katika vituo vyao vya kazi na kufanyiwa uchunguzi kama kuna deni lolote la kijiji analodaiwa.

Mhando ametoa agizo hilo alipokutana na Uongozi wa Kijiji cha Shukura ambapo Viongozi hao wamedai kuwepo na changamoto ya uhamishwaji wa ghafla kwa Watendaji wa Vijiji jambo linalowaachia madeni yasiyo ya lazima,kufuatia Watendaji hao kuondoka na michango ya Wananchi kwa ajili ya maendeleo ya Kijiji.

Katika hatua nyingine Mhando ametoa Siku Saba kwa Uongozi wa Kijiji hicho kuhakikisha wanamaliza mgogoro wa eneo la ujenzi wa Shule ya Msingi Shukura na kuanza Ujenzi wa Shule hiyo mara  moja.

Hata hivyo Mhando  amewataka Serikali ya Kijiji cha Shukura pamoja na Watendaji wake,kufanya harambee ya kuilipa mifuko 50 ya saruji  iliyotolewa na Mkuu wa Wilaya hiyo kwa ajili ya ujenzi wa Shule hiyo ambayo imeharibika.

Kijiji cha Shukura kilianzishwa Mwaka 2014 na ni Kijiji pekee katika Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika ambacho hakina Taasisi yoyote ya Serikali ikiwemo Shule wala Zahanati.

                               MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja