Skip to main content

DC Mhando agoma Watendaji wa VIjiji kupewa uhamisho kabla hawajafanyiwa uchunguzi.

Baadhi ya Wananchi wakifatilia Mkutano wa hadhara.

Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Salehe Mbwana Mhando,akiongea jambo mbele ya Wananchi katika Mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Shukura.


Na Zainab Mtima,Tanganyika-Katavi

Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Mkoani, Katavi  Saleh Mhando  ameagiza watendaji wote wa vijiji katika halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika  wanaoomba uhamisho,wasipewe uhamisho wowote  na badala yake warudi katika vituo vyao vya kazi na kufanyiwa uchunguzi kama kuna deni lolote la kijiji analodaiwa.

Mhando ametoa agizo hilo alipokutana na Uongozi wa Kijiji cha Shukura ambapo Viongozi hao wamedai kuwepo na changamoto ya uhamishwaji wa ghafla kwa Watendaji wa Vijiji jambo linalowaachia madeni yasiyo ya lazima,kufuatia Watendaji hao kuondoka na michango ya Wananchi kwa ajili ya maendeleo ya Kijiji.

Katika hatua nyingine Mhando ametoa Siku Saba kwa Uongozi wa Kijiji hicho kuhakikisha wanamaliza mgogoro wa eneo la ujenzi wa Shule ya Msingi Shukura na kuanza Ujenzi wa Shule hiyo mara  moja.

Hata hivyo Mhando  amewataka Serikali ya Kijiji cha Shukura pamoja na Watendaji wake,kufanya harambee ya kuilipa mifuko 50 ya saruji  iliyotolewa na Mkuu wa Wilaya hiyo kwa ajili ya ujenzi wa Shule hiyo ambayo imeharibika.

Kijiji cha Shukura kilianzishwa Mwaka 2014 na ni Kijiji pekee katika Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika ambacho hakina Taasisi yoyote ya Serikali ikiwemo Shule wala Zahanati.

                               MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...