Skip to main content

RAIA WA BURUNDI AMBAO NI WAFUGAJI WAMEVAMIA ARDHI YA TANZANIA WILAYANI KAKONKO MKOANI KIGOMA.


Raia wa Burundi waliokamatwa.


Na Jastin Cosmas,Kakonko-Kigoma.


Raia wa Burundi ambao ni Wafugaji,wamevamia ardhi ya Tanzania Wilayani Kakonko Mkoani Kigoma kwa kuweka Mifugo ya Ng’ombe kama sehemu ya kuchunga kitendo ambacho kimeleta sintofahamu kwa Wananchi wa Kata ya Gwanumpu.


Sintofahamu hiyo imeibuka wakati Wananchi walipohoji katika mkutano wa hadhara ulio fanyika katika Kijiji cha Rusenga Kata ya Gwanumpu Wilayani Kakonko,ambapo wamelaani kitendo cha Mashamba yao kuvamiwa na Wafugaji kutoka Nchi ya Burundi huku mazao yao yakiharibiwa na Ng’ombe.


Wananchi hao wamesema kuwa,Mwnyekiti wa Kijiji cha Rusenga Evarist Ndumiwe alitoa ardhi kwa Wafugaji wa Burundi bila kushirikisha Wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji hicho cha Rusenga.ambapo Wajumbe wa Kijiji hicho wamesema hawana imani na Mwenyekiti huyo.


Nae mwenyekiti wa Kijiji hicho Evarist Ndumiwe ametupilia mbali lawama hizo, akisema kuwa ameingia kwenye uongozi Ng’ombe hao wakiwepo hivyo haja ruhusu Ng’ombe hao kuingia Tanzania.


Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Gwanumpu Toyi Butono amesema kuwa Ng'ombe hao waondolewe,sheria na  taraibu zifatwe na ardhi irudishwe kwa Wananchi.


Ntarabe Mvulugu,ni miongoni mwa Wananchi ambao Mashamba yao yamevamiwa ambapo amesema kuwa tayari Mazao yake yameharibiwa na Ng’ombe,na hana sehemu nyingine yakulima kwani alikuwa anategemea sehemu hiyo kwa shughuli ya Kilimo.


Site Blog imemtafuta Mwenyekiti wa Ulinzi na Usalama ambae ni Mkuu wa Wilaya Kakonko,Kanali Hosea Ndagala ambapo amesema kuwa hajapata taarifa kuhusu kuwepo kwa Ng’ombe hao hivyo suala hili atalifuatilia kwa kina.


Msikilize hapa chini Diwani wa Kata ya Gwanumpu Toyi Butono.


Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja