Skip to main content

WAKAMATWA KWA KUJIHUSISHA NA MATUKIO YA MAUAJI,KUJERUHI.

 


Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watuhumiwa 5 kwa tuhuma za kujihusisha na matukio ya mauaji,kujeruhi na kuingiza bidhaa Nchini bila kulipia ushuru.


Kuhusu taarifa za Mauaji,Jeshi la Polisi Mkoani humo limesema Watuhumiwa Watatu ambao ni Lusajo Mwaijobelo (32),Naboti Sanga (44) na Christina Chaula (50) wote wakazi wa Kisyosyo-Matema Wilaya ya Kyela,wanashikiliwa kwa tuhuma za tukio la mauaji ya Mwanamke aitwaye Elizabeth Mwaike (22) Mkazi wa Kisyosyo.

Watuhumiwa wamekamatwa Mei 28,2021 majira ya saa 18:30 jioni katika Kijiji cha Kisyosyo,Kata ya Matema,Tarafa ya Ntebela,Wilaya ya Kyela,Mkoani Mbeya,ambapo katika Machimbo ya Kokoto ya kampuni ya Kichina,Marehemu alikutwa eneo hilo akiwa ameuawa kwa kupigwa kitu kizito kichwani umbali wa mita 500 kutoka Nyumbani kwake.

Chanzo cha tukio hilo kimeelezwa kuwa ni wivu wa kimapenzi na upelelezi wa shauri hili unaendelea na mara baada ya kukamilika watuhumiwa watafikishwa mahakamani.

Katika tukio lingine,Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya linamshikilia Furaha Shipindi (37) Mkazi wa DDC-Mbalizi kwa tuhuma za kujihusisha na matukio ya kujeruhi.

Mtuhumiwa alikamatwa Mei 28,2021 majira ya saa 21:00 usiku,mtaa wa DDC katika Mji Mdogo wa Mbalizi,Kata ya Utengule,Tarafa ya Usongwe,Mkoa wa Mbeya. 

Katika upekuzi,Mtuhumiwa alikutwa na shoka dogo,nondo iliyochongwa mbele na begi dogo lenye nguo anazobadilisha kuvaa kila baada ya tukio.

Aidha,Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Mfanyabiashara aitwae Philip Peter (49) mkazi wa Jijini Mbeya kwa tuhuma za kuingiza bidhaa Nchini bila kulipia ushuru pamoja na kuingiza bidhaa zilizopigwa marufuku.

Mtuhumiwa alikamatwa Mei 28,2021 majira ya saa 05:00 alfajiri Kijiji cha Bujinga, Kata ya Bagamoyo, Wilaya ya Rungwe,Mkoani Mbeya akiwa na Gari yenye namba za usajili T.259 BLA aina ya Toyota Hilux Pickup akiingiza bidhaa mbalimbali Nchini akitokea Nchini Malawi bila kulipia ushuru.

Bidhaa alizokamatwa nazo ni pamoja na Sukari katoni 30,Uyoga mifuko 20,Mafuta ya kula ndoo 10 kila moja lita 20 na Pombe kali zilizopigwa marufuku Nchini aina ya Fighter Vodka katoni 60 na taratibu za kiforodha zinaendelea. 

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja