Skip to main content

WAKAMATWA KWA KUJIHUSISHA NA MATUKIO YA MAUAJI,KUJERUHI.

 


Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watuhumiwa 5 kwa tuhuma za kujihusisha na matukio ya mauaji,kujeruhi na kuingiza bidhaa Nchini bila kulipia ushuru.


Kuhusu taarifa za Mauaji,Jeshi la Polisi Mkoani humo limesema Watuhumiwa Watatu ambao ni Lusajo Mwaijobelo (32),Naboti Sanga (44) na Christina Chaula (50) wote wakazi wa Kisyosyo-Matema Wilaya ya Kyela,wanashikiliwa kwa tuhuma za tukio la mauaji ya Mwanamke aitwaye Elizabeth Mwaike (22) Mkazi wa Kisyosyo.

Watuhumiwa wamekamatwa Mei 28,2021 majira ya saa 18:30 jioni katika Kijiji cha Kisyosyo,Kata ya Matema,Tarafa ya Ntebela,Wilaya ya Kyela,Mkoani Mbeya,ambapo katika Machimbo ya Kokoto ya kampuni ya Kichina,Marehemu alikutwa eneo hilo akiwa ameuawa kwa kupigwa kitu kizito kichwani umbali wa mita 500 kutoka Nyumbani kwake.

Chanzo cha tukio hilo kimeelezwa kuwa ni wivu wa kimapenzi na upelelezi wa shauri hili unaendelea na mara baada ya kukamilika watuhumiwa watafikishwa mahakamani.

Katika tukio lingine,Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya linamshikilia Furaha Shipindi (37) Mkazi wa DDC-Mbalizi kwa tuhuma za kujihusisha na matukio ya kujeruhi.

Mtuhumiwa alikamatwa Mei 28,2021 majira ya saa 21:00 usiku,mtaa wa DDC katika Mji Mdogo wa Mbalizi,Kata ya Utengule,Tarafa ya Usongwe,Mkoa wa Mbeya. 

Katika upekuzi,Mtuhumiwa alikutwa na shoka dogo,nondo iliyochongwa mbele na begi dogo lenye nguo anazobadilisha kuvaa kila baada ya tukio.

Aidha,Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Mfanyabiashara aitwae Philip Peter (49) mkazi wa Jijini Mbeya kwa tuhuma za kuingiza bidhaa Nchini bila kulipia ushuru pamoja na kuingiza bidhaa zilizopigwa marufuku.

Mtuhumiwa alikamatwa Mei 28,2021 majira ya saa 05:00 alfajiri Kijiji cha Bujinga, Kata ya Bagamoyo, Wilaya ya Rungwe,Mkoani Mbeya akiwa na Gari yenye namba za usajili T.259 BLA aina ya Toyota Hilux Pickup akiingiza bidhaa mbalimbali Nchini akitokea Nchini Malawi bila kulipia ushuru.

Bidhaa alizokamatwa nazo ni pamoja na Sukari katoni 30,Uyoga mifuko 20,Mafuta ya kula ndoo 10 kila moja lita 20 na Pombe kali zilizopigwa marufuku Nchini aina ya Fighter Vodka katoni 60 na taratibu za kiforodha zinaendelea. 

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...