Skip to main content

"Kwa Miaka hii takribani 9 sidhani kuna jipya kujiita Mkoa mpya"-RC Katavi.


Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Hoza Mrindoko katika Kikao na Watumishi wa Umma Mkoani Katavi cha kusalimiana na kufahamiana leo Mei 24,2021.

Katibu Tawala Mkoa wa Katavi,Abdallah Mohammed Malela.

Baadhi ya Watumishi wa Umma wakifatilia Hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi wakati wa Kikao cha kusalimiana na kufahamiana katika ukumbi wa Mpanda Manispaa.


Na Mwandishi Wetu,Site Tv
Mpanda-Katavi.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi Ndg. Abdallah Malela amemweleza Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi.Mwanamvua Hoza Mrindoko kuwa Watumishi wa Mkoa wa Katavi wanafanya kazi kwa kujituma bila kujali Siku za Kazi na hawana changamoto zozote isipokuwa Mkoa unatatizo kubwa la Lishe na Matundu bora ya Vyoo.

Ameyasema hayo wakati akimkaribisha Mkuu wa Mkoa huo Bi.Mwanamvua Hoza Mrindoko katika kikao na Watumishi wa Umma wa Mkoa wa Katavi,Kikao cha kusalimiana na kufahamiana kilichofanyika katika Ukumbi wa Mpanda Manispaa leo Mei 24,2021.

Kwa upande wake RC Mrindoko ametumia nafasi hiyo kuwashukuru Watumishi wenzake kwa mapokezi na kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe,Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini huku akisema atahakikisha anatimiza yale yote yanayotarajiwa na Rais kwa Wanakatavi kutoka kwake na kuwataka Watumishi kuendelea kujituma kwa kufanya kazi vizuri kwa manufaa ya Wananchi.

"Nimeona cha Kwanza kabisa nikutane na nyie,kwa sababu naamini kwamba hii ndiyo timu ya ushindi,lakini kwa Miaka hii takribani 9 sidhani kuna jipya kujiita Mkoa mpya,kwa hiyo sioni sababu ya kujiita Mkoa mpya kwa sababu tayari zipo hatua kubwa ambazo tumeshapiga Sisi kwama Mkoa wa Katavi"-RC Katavi,Mwanamvua Mrindoko.

RC Mwanamvua amesema kila nafasi katika Uongozi inaumuhimu wake katika kusimamia miradi kwa ukamilifu hivyo ni wito wake kuona mipango yote inatekelezwa kwa mujibu wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ikiwemo kuisoma na kujua nini kinatakiwa kufanyika katika kila Sekta.

Aidha,amesema ni jukumu la kila Mmoja kuhakikisha usalama wa Mkoa,na amewasihii Watumishi kutoa taarifa pale wanapoona hali ya uvunjifu wa Amani ili hatua zichukuliwe kabla ya madhara kutokea huku akiwataka kuzitunza Mali za Umma kama wanavyotunza Mali zao.

Kadhalika amewaomba Watumishi wote Kutenda haki katika kuwahudumia Wananchi ikiwa ni pamoja na kuepuka ubaguzi kwa Maslahi yao Binafsi na badala yake kuwahudumia Wananchi kwa haraka na kutatua changamoto zao huku akiikemea sentensi ya "rudi kesho" na kusema kuwa asingependa kuisikia.


Kwa upande wao baadhi ya Watumishi wa Umma wamemhakikishia Mkuu wa Mkoa kuwa watafanya kazi kwa ushirikiano.

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...