Skip to main content

Mwenyekiti na Mtendaji wasimamishwa ili kupisha uchuguzi kwa tuhuma za ubadhilifi wa Fedha.

Pichani ni Mwenyekiti wa Kijiji cha Shukura Peter Colomery (Alie shika Shavu) na Mtendaji wa kijiji hicho Mesamo Megama.

Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Salehe Mbwana Mhando.


Na Zainab Mtima,Tanganyika-Katavi.

Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika  Mkoani Katavi,Saleh Mhando amewasimamisha kazi Mwenyekiti wa Kijiji cha Shukura Peter Colomery na Mtendaji wa Kijiji hicho Mesamo Megama ili kupisha uchuguzi kufuatia tuhuma za ubadhilifi wa Fedha zilizochangwa na Wanakijiji kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Msingi Shukura.

Mhando ametoa maagizo hayo katika mkutano wa hadhara na wakazi wa Kijiji hicho,ambapo awali walitoa kero zao mbele ya Mkuu wa Wilaya huyo na kuzipatia ufumbuzi na kuongeza kuwa  Watumishi hao watachunguzwa na taasisi ya kupambana na Rushwa TAKUKURU Wilayani Tanganyika. .

Katika mkutano huo pia Mhando ameagiza Uongozi wa Kijiji hicho kuhakikisha ujenzi wa Shule ya Msingi Shukura kuanza kujengwa kuanzia June Mosi Mwaka huu.

Hata hivyo ametoa tahadhali kwa Wananchi waishio pembezeni mwa Ziwa Tanganyika,kuepuka kujenga makazi ya kudumu maeneo ya mwambao wa ziwa .

Aidha amewataka Wenyeviti wa Vijiji vyote katika Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika kusoma mapato na matumizi kwa Wananchi kila baada ya Miezi Mitatu.

MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Katavi Yakemea Vikali Ushoga,Mauaji "Wanaume Msiwazuie Wake Zenu Kufanya...

Watu kula dagaa,Mchicha na Maharage wanaona ni Umasikini/Lishe ajenda ya...