Skip to main content

Mwenyekiti na Mtendaji wasimamishwa ili kupisha uchuguzi kwa tuhuma za ubadhilifi wa Fedha.

Pichani ni Mwenyekiti wa Kijiji cha Shukura Peter Colomery (Alie shika Shavu) na Mtendaji wa kijiji hicho Mesamo Megama.

Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Salehe Mbwana Mhando.


Na Zainab Mtima,Tanganyika-Katavi.

Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika  Mkoani Katavi,Saleh Mhando amewasimamisha kazi Mwenyekiti wa Kijiji cha Shukura Peter Colomery na Mtendaji wa Kijiji hicho Mesamo Megama ili kupisha uchuguzi kufuatia tuhuma za ubadhilifi wa Fedha zilizochangwa na Wanakijiji kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Msingi Shukura.

Mhando ametoa maagizo hayo katika mkutano wa hadhara na wakazi wa Kijiji hicho,ambapo awali walitoa kero zao mbele ya Mkuu wa Wilaya huyo na kuzipatia ufumbuzi na kuongeza kuwa  Watumishi hao watachunguzwa na taasisi ya kupambana na Rushwa TAKUKURU Wilayani Tanganyika. .

Katika mkutano huo pia Mhando ameagiza Uongozi wa Kijiji hicho kuhakikisha ujenzi wa Shule ya Msingi Shukura kuanza kujengwa kuanzia June Mosi Mwaka huu.

Hata hivyo ametoa tahadhali kwa Wananchi waishio pembezeni mwa Ziwa Tanganyika,kuepuka kujenga makazi ya kudumu maeneo ya mwambao wa ziwa .

Aidha amewataka Wenyeviti wa Vijiji vyote katika Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika kusoma mapato na matumizi kwa Wananchi kila baada ya Miezi Mitatu.

MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja