Skip to main content

MANISPAA YA MPANDA KUTOA ELIMU YA KILIMO CHA NCHI KAVU.


Shamba la Mfano likiwa na Mazao mbalimbali ikiwemo Mpunga wa Nchi kavu,Mahindi,Zao la strawberry, Bamia, Alizeti, Ufuta na mazao mengine ya Bustani kama Mchicha,chainizi,spinachi n.k. PICHA NA Swaum Katambo

Mkuu wa Idara ya Kilimo,Umwagiliaji na  Ushirika Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Laurent Munyu akifafanua jambo.

Na Swaum Katambo,Mpanda-Katavi

Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda inatarajia kutenga bajeti kwa ajili ya kuanzisha mashamba ya mfano ya kilimo cha kisasa ambayo yatasaidia kutoa Elimu kwa jamii juu ya namna bora ya kufanya kilimo cha kisasa hasa maeneo yaliyopo mjini.

Akizungumza leo Mei 21,2020 katika hitimisho la hatua ya utoaji wa Elimu ya Kilimo kwa wakulima wa Manispaa ya Mpanda na Mkoa wa Katavi kwa ujumla,Mkuu wa Idara ya Kilimo,Umwagiliaji na  Ushirika Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Laurent Munyu amesema pamoja na kuishi maeneo ya Mjini,Wananchi wanaweza kuandaa Mashamba na kulima Kilimo chenye tija.

Munyu ameongeza kuwa wanachokifanya wanajaribu kuonesha wadau wa Kilimo namna bora za uzalishaji wa mazao ya aina mbalimbali kama Mpunga wa Nchi kavu,Mahindi,Zao la strawberry, Bamia, Alizeti, Ufuta na mazao mengine ya Bustani kama Mchicha,chainizi,spinachi n.k

"Kitu tunachokifanya leo ni moja ya majukumu mazito sana ambayo Idara ya Kilimo inapaswa kufanya,sisi wataalamu wa Kilimo tunaamini jambo moja kwamba kuona ni kuamini..,tunachokifanya ni kufanya sisi kwa mfano mpaka tunafikia matokeo,yale matokeo sasa ndio tunakuja kumuonesha Mkulima na kumuelekeza njia ya kuyafikia yale matokeo" Alisema Munyu.

Kwa upande wao baadhi ya wadau wa Kilimo walionufaika na Elimu ya Kilimo hicho cha kisasa wameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda kwa kuandaa mafunzo hayo ambapo wamesema walizoea kulima Kilimo cha maeneo ya bondeni ili kufuata maji hivyo Elimu hiyo imewapa mwanga kuwa wanaweza kulima hata maeneo ya nchi kavu yaliyopo mjini na kupata mazao yenye tija.


Baadhi ya Wadau wakieleza namna watakavyoitumia Elimu waliyoipata kujikwamua katika Kilimo.

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...