Skip to main content

MANISPAA YA MPANDA KUTOA ELIMU YA KILIMO CHA NCHI KAVU.


Shamba la Mfano likiwa na Mazao mbalimbali ikiwemo Mpunga wa Nchi kavu,Mahindi,Zao la strawberry, Bamia, Alizeti, Ufuta na mazao mengine ya Bustani kama Mchicha,chainizi,spinachi n.k. PICHA NA Swaum Katambo

Mkuu wa Idara ya Kilimo,Umwagiliaji na  Ushirika Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Laurent Munyu akifafanua jambo.

Na Swaum Katambo,Mpanda-Katavi

Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda inatarajia kutenga bajeti kwa ajili ya kuanzisha mashamba ya mfano ya kilimo cha kisasa ambayo yatasaidia kutoa Elimu kwa jamii juu ya namna bora ya kufanya kilimo cha kisasa hasa maeneo yaliyopo mjini.

Akizungumza leo Mei 21,2020 katika hitimisho la hatua ya utoaji wa Elimu ya Kilimo kwa wakulima wa Manispaa ya Mpanda na Mkoa wa Katavi kwa ujumla,Mkuu wa Idara ya Kilimo,Umwagiliaji na  Ushirika Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Laurent Munyu amesema pamoja na kuishi maeneo ya Mjini,Wananchi wanaweza kuandaa Mashamba na kulima Kilimo chenye tija.

Munyu ameongeza kuwa wanachokifanya wanajaribu kuonesha wadau wa Kilimo namna bora za uzalishaji wa mazao ya aina mbalimbali kama Mpunga wa Nchi kavu,Mahindi,Zao la strawberry, Bamia, Alizeti, Ufuta na mazao mengine ya Bustani kama Mchicha,chainizi,spinachi n.k

"Kitu tunachokifanya leo ni moja ya majukumu mazito sana ambayo Idara ya Kilimo inapaswa kufanya,sisi wataalamu wa Kilimo tunaamini jambo moja kwamba kuona ni kuamini..,tunachokifanya ni kufanya sisi kwa mfano mpaka tunafikia matokeo,yale matokeo sasa ndio tunakuja kumuonesha Mkulima na kumuelekeza njia ya kuyafikia yale matokeo" Alisema Munyu.

Kwa upande wao baadhi ya wadau wa Kilimo walionufaika na Elimu ya Kilimo hicho cha kisasa wameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda kwa kuandaa mafunzo hayo ambapo wamesema walizoea kulima Kilimo cha maeneo ya bondeni ili kufuata maji hivyo Elimu hiyo imewapa mwanga kuwa wanaweza kulima hata maeneo ya nchi kavu yaliyopo mjini na kupata mazao yenye tija.


Baadhi ya Wadau wakieleza namna watakavyoitumia Elimu waliyoipata kujikwamua katika Kilimo.

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja