Skip to main content

Posts

MWALIMU WA SHULE YA MSINGI MKOANI MBEYA ADAKWA KWA TUHUMA ZA WIZI KWA NJIA YA MTANDAONI KIASI CHA MILIONI 34.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya,Ulrich Matei akionyesha Pesa zilizokamatwa.                                                       TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUKAMATWA KWA MTUHUMIWA WA WIZI KWA NJIA YA MTANDAO. Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia JOSEPH SHILA [29] Mwalimu Shule ya Msingi Mwakareli na Mkazi wa Mwakareli kwa tuhuma za wizi wa fedha Tshs.Milioni 34,000,000/= mali ya mwalimu mstaafu GIDEON NGOLAKO MWALUJOBO [60] Mkazi wa Mwakareli. Mtuhumiwa alikamatwa mnamo tarehe 30.06.2020 majira ya saa 19:00 Usiku huko Kijiji na Kata ya Mwakareli, Tarafa ya Busokelo, Wilaya ya Rungwe, Mkoa wa Mbeya baada ya kupata taarifa toka kwa msiri. Mtuhumiwa alifanikiwa kuiba pesa hizo mali ya mwalimu mstaafu GIDEON NGOLAKO MWALUJOBO [60] Mkazi wa Mwakareli kupitia akaunti 6140201871 kwa kutumia “NMB Mobile” katika Tawi la NMB Mbalizi ...

KAMATI YA SIASA CCM RUVUMA YAKAGUA CHUO CHA VETA NYASA.

Kamati ya Siasa ya CCM MKoa wa Ruvuma ikikagua majengo ya mradi wa chuo cha VETA Wilaya ya Nyasa) KAMATI ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma imekagua mradi wa ujenzi wa  chuo cha ufundi stadi VETA Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma ambao unagharimu zaidi ya shilingi bilioni mbili. Akisoma taarifa ya mradi huo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nyasa,Jimson Mhagama  amesema mradi unahusisha majengo 16 na kwamba fedha za mradi zimepokelewa kwa awamu ambapo katika awamu ya kwanza zimepokelewa zaidi ya bilioni moja. Amesema mradi huo unatekelezwa  na mafundi mawili wakiwemo SUMA JKT ambaye anajenga majengo 14 na Simon Chiwanga ambaye anajenga vyumba viwili vya madarasa na kwamba mradi umetoa jumla ya ajira 123.                          Moja ya majengo ya karakana katika chuo cha VETA Nyasa Mhagama amesema mradi huo unatekelezwa kwa kutumia mtindo wa force account ambapo wananchi kutoka Kata ya Kilosa ambako mradi ...

MKOA WA KATAVI UMEJIPANGA KULETA MAPINDUZI YA KIUCHUMI KWA KUONGEZA VIWANDA,KUKUZA SEKTA YA MADINI NA KILIMO.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mh Juma Zuberi Homera. Na Swaum Katambo Mpanda-Katavi Kuelekea mwishoni mwa Mwaka wa fedha,Mkoa wa Katavi umejiandaa kuleta mapinduzi makubwa ya Kiuchumi ikiwemo kuongeza Viwanda,kuongeza Vyuo,kukuza sekta ya Madini,Kilimo na Umeme Vijijini. Akitoa mwelekeo wa Mkoa,Mkuu wa Mkoa Mh. Juma Zuberi Homera katika kikao na Waandishi wa Habari kilichofanyika Ofisini kwake Juni 24,2020 amezungumzia mwenendo wa Soko la Madini na mikakati ya kuongeza kasi ya ununuzi na uuzaji wa Madini. Kuhusu Madini Mh Homera alisema,toka Soko la Madini lianze Mei,2019 hadi Juni 2020 Mkoa umefikisha Kilogra 254 za Madini na Gram 734 zenye thamani zaidi ya Tsh. Bilioni 24 ambapo kupitia soko la Madini Mkoa umeshakusanya kiasi cha Tsh. Bilioni 1.7 huku tozo za huduma kutoka katika Sekta ya Madini ikichangia zaidi ya Milioni 66. Alisema matarajio ni kuhakikisha ongezeko la ununuzi na uuzaji wa madini,na Serikali imeshapata eneo la uchimbaji Madini la zaidi ya Hekta 1901 kutoka ...

MKOA WA KATAVI WAANDAA EKARI 221 KWAAJILI YA KUANZISHA MAONYESHO YA NANENANE.

Muonekano wa eneo linalotarajiwa kuanzishwa maonyesho ya Nanenane Mkoa wa Katavi umetenga zaidi ya Ekari 200 eneo la Kabungu Wilayani Tanganyika kwaajili ya kuanzisha Maonyesho ya Kilimo na Sherehe za Wakulima (Nanenane) za mwaka 2021 ambapo kabla ya mpango huo Wakulima kutoka Mikoa ya Nyanda za juu Kusini iliwalazimu kwenda Mkoani Mbeya. Akizungumza na Site Tv ilipokwenda kuangalia maendeleo katika eneo hilo Msanifu Majengo Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika Ndg. Iblahim Bashiru amesema hadi sasa maandalizi yako hatua ya kwanza ya kulisafisha eneo pamoja na kuchonga Barabara. "Shughuli zinazofanyika hapa,kwanza tuna eneo la Ekari 221 ambapo katika eneo hili tutakuwa na majengo ya Halmashauri,tutakuwa na maeneo kwaajili ya zana za Kilimo na Taasisi mbalimbali"-Ibrahim Bashiru,Msanifu Majengo Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika. "....hapa ni uchongaji wa Barabara za kuingia ndani ya site kwa maana ya access road pamoja na main Road,tunachokifanya kwa sasa ni a...

WANANCHI WA NAMTUMBO KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJI WA BILIONI MBILI.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ChristinaMndeme  akikagua mradi wa maji wa Mkongogulioni Wilayani ya Namtumbo. SERIKALI ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt.John Magufuli imetoa zaidi ya Tsh. Bilioni Mbili ili kutekeleza mradi wa Maji wa Mkongogulioni na Nakahimba Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma. Kaimu Meneja wa RUWASA Wilaya ya Namtumbo David Mkondya akitoa taarifa ya mradi huo kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme,amesema mradi huo ulisainiwa  Juni 12 mwaka 2013 na utekelezaji wake ulianza mwaka 2017 na ulitarajiwa kukamilika Februari 2020 chini ya Mkandarasi Kipera Contractors. Mkondya alisema mradi huo unatarajia kuhudumia watu zaidi ya 8000 katika vijiji vya Mkongogulioni na Nahimba na kwamba kazi ambazo zimepangwa kufanyika kwenye mradi huo ni ujenzi wa tanki la lita 25,000 katika kijiji cha Nahimba na ukarabati wa matanki mawili yenye ujazo wa lita 150,000 katika kijiji cha Mkongo. Hata hivyo alizitaja kazi ambazo zimefanyika kulingana na mkat...

SIMANZI KATAVI,MTOTO WA MIAKA MITANO AZAMA KWENYE MAJI.

Mtoto mmoja aliyefahamika kwa majina ya Trifon Filbert Kanoni (5) amefariki Dunia kwa kuzama kwenye bwawa la kufyatulia tofali lililopo Eneo la mnazi mmoja E,kata ya uwanja wa ndege tarafa ya kashauriri manispaa ya Mpanda mkoani katavi. Wakizungumza kwa masikitiko baadhi ya mashuhuda wa tukio Hilo wamesema tukio limetokea Juni 24,2020 majira ya saa 7 mchana wakati alipokwenda kumtembelea baba yake mdogo anaejihusisha na shughuli za uchomaji Matofali. Dada wa Marehemu huyo,Anasitazia Martin amesema,Mdogo wake huyo hakuwa anasoma huku Baba wa Marehemu, Filbert Kanoni akieleza kuwa alipata taarifa majira ya saa Sita mchana na kufika eneo la tukio lakini alikukuta Mtoto wake ameshafariki Dunia tayari.  Nae Mjumbe wa Serikali ya Mtaa huo Juma Gogomoka amewaasa wazazi kutowaruhusu watoto wao kujishughulisha na shughuli za Matofali huku akiwaasa wachomaji kuacha tabia za kuwapa ajira watoto ili kuwalipa pesa ndogo ambayo ni sh 5 kwa Kila tofali. Kwa upande wake Afisa Opare...

TANGA YAJIDHATITI NA MAPAMBANO DHIDI YA COVID 19

  Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martin Shigella akipokea Matanki matano kutoka wa wadau wa mapambano ya COVID 19 jijini humo Na Mwandishi Wetu       Tanga MKUU wa Mkoa wa Tanga Martin Shigella amepokea vifaa vya kujikinga na ugongwa wa COVID 19 ikiwa sambamba na kuwataka wafanyabiashara wengine kuguswa na kuchangia vifaa vya usafi ili kuhakikisha wanadhibiti na kuchukua hatadhati za kujikinga na ugonjwa huo. Kauli hiyo ameitoa wakati akipokea msaada wa mataki matano ya ujazwa wa lita mia tano kila moja kutoka kampuni ya vifaa vya ujenzi ya Hussain Plastic Industry ya jijini hapa. Shigella amasema bado kunauhitaji mkubwa wa vifaa kwa ajili ya kusabazwa   kwenye maeneo mengine ya mkoani Tanga ili wananchi waweze kujikinga na COVID 19 kupitia kunawa mikono kwa maji safi yanyotiririka . Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Hussein Yusuph amesema kuwa wameamua kutoa msaada huo ili kuuga juhudi juhudiza serikali katika mapambano katika kukabili...