Skip to main content

SIMANZI KATAVI,MTOTO WA MIAKA MITANO AZAMA KWENYE MAJI.




Mtoto mmoja aliyefahamika kwa majina ya Trifon Filbert Kanoni (5) amefariki Dunia kwa kuzama kwenye bwawa la kufyatulia tofali lililopo Eneo la mnazi mmoja E,kata ya uwanja wa ndege tarafa ya kashauriri manispaa ya Mpanda mkoani katavi.

Wakizungumza kwa masikitiko baadhi ya mashuhuda wa tukio Hilo wamesema tukio limetokea Juni 24,2020 majira ya saa 7 mchana wakati alipokwenda kumtembelea baba yake mdogo anaejihusisha na shughuli za uchomaji Matofali.

Dada wa Marehemu huyo,Anasitazia Martin amesema,Mdogo wake huyo hakuwa anasoma huku Baba wa Marehemu, Filbert Kanoni akieleza kuwa alipata taarifa majira ya saa Sita mchana na kufika eneo la tukio lakini alikukuta Mtoto wake ameshafariki Dunia tayari. 

Nae Mjumbe wa Serikali ya Mtaa huo Juma Gogomoka amewaasa wazazi kutowaruhusu watoto wao kujishughulisha na shughuli za Matofali huku akiwaasa wachomaji kuacha tabia za kuwapa ajira watoto ili kuwalipa pesa ndogo ambayo ni sh 5 kwa Kila tofali.

Kwa upande wake Afisa Oparesheni wa zima Moto Paul Masungwa ametoa ushauri kwa wananchi kuwa na utaratibu wa kutoa taarifa kwa wakati kwa kupiga simu ya bure 114 na kuwaomba viongozi wa serikali ya Mtaa kuwasimamia wafyatuaji matofali wafukue madimbwi ambayo ni hatarishi.

Aidha,amesema Jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Katavi linaendelea kutoa elimu kwa Jamii ili kujua namna ya kujiepusha na majanga kama hayo ikiwemo utoaji taarifa mapema.

Taarifa zaidi,tembelea YouTube channel yetu @sitetvtz


        Anasitazia Martin,Dada wa Marehemu


        Filbert Kanoni,Baba wa Marehemu


     Afisa Oparesheni wa zima Moto,Paul Masungwa


      Mjumbe wa Serikali ya Mtaa,Juma Gogomoka


           Mashuhuda wakiwa eneo la tukio


         Bwawa lililopelekea kifo cha Mtoto huyo







Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja