Skip to main content

SIMANZI KATAVI,MTOTO WA MIAKA MITANO AZAMA KWENYE MAJI.




Mtoto mmoja aliyefahamika kwa majina ya Trifon Filbert Kanoni (5) amefariki Dunia kwa kuzama kwenye bwawa la kufyatulia tofali lililopo Eneo la mnazi mmoja E,kata ya uwanja wa ndege tarafa ya kashauriri manispaa ya Mpanda mkoani katavi.

Wakizungumza kwa masikitiko baadhi ya mashuhuda wa tukio Hilo wamesema tukio limetokea Juni 24,2020 majira ya saa 7 mchana wakati alipokwenda kumtembelea baba yake mdogo anaejihusisha na shughuli za uchomaji Matofali.

Dada wa Marehemu huyo,Anasitazia Martin amesema,Mdogo wake huyo hakuwa anasoma huku Baba wa Marehemu, Filbert Kanoni akieleza kuwa alipata taarifa majira ya saa Sita mchana na kufika eneo la tukio lakini alikukuta Mtoto wake ameshafariki Dunia tayari. 

Nae Mjumbe wa Serikali ya Mtaa huo Juma Gogomoka amewaasa wazazi kutowaruhusu watoto wao kujishughulisha na shughuli za Matofali huku akiwaasa wachomaji kuacha tabia za kuwapa ajira watoto ili kuwalipa pesa ndogo ambayo ni sh 5 kwa Kila tofali.

Kwa upande wake Afisa Oparesheni wa zima Moto Paul Masungwa ametoa ushauri kwa wananchi kuwa na utaratibu wa kutoa taarifa kwa wakati kwa kupiga simu ya bure 114 na kuwaomba viongozi wa serikali ya Mtaa kuwasimamia wafyatuaji matofali wafukue madimbwi ambayo ni hatarishi.

Aidha,amesema Jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Katavi linaendelea kutoa elimu kwa Jamii ili kujua namna ya kujiepusha na majanga kama hayo ikiwemo utoaji taarifa mapema.

Taarifa zaidi,tembelea YouTube channel yetu @sitetvtz


        Anasitazia Martin,Dada wa Marehemu


        Filbert Kanoni,Baba wa Marehemu


     Afisa Oparesheni wa zima Moto,Paul Masungwa


      Mjumbe wa Serikali ya Mtaa,Juma Gogomoka


           Mashuhuda wakiwa eneo la tukio


         Bwawa lililopelekea kifo cha Mtoto huyo







Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...