Skip to main content

TANGA YAJIDHATITI NA MAPAMBANO DHIDI YA COVID 19



 
Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martin Shigella akipokea Matanki matano kutoka wa wadau wa mapambano ya COVID 19 jijini humo


Na Mwandishi Wetu
      Tanga

MKUU wa Mkoa wa Tanga Martin Shigella amepokea vifaa vya kujikinga na ugongwa wa COVID 19 ikiwa sambamba na kuwataka wafanyabiashara wengine kuguswa na kuchangia vifaa vya usafi ili kuhakikisha wanadhibiti na kuchukua hatadhati za kujikinga na ugonjwa huo.

Kauli hiyo ameitoa wakati akipokea msaada wa mataki matano ya ujazwa wa lita mia tano kila moja kutoka kampuni ya vifaa vya ujenzi ya Hussain Plastic Industry ya jijini hapa.

Shigella amasema bado kunauhitaji mkubwa wa vifaa kwa ajili ya kusabazwa  kwenye maeneo mengine ya mkoani Tanga ili wananchi waweze kujikinga na COVID 19 kupitia kunawa mikono kwa maji safi yanyotiririka .

Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Hussein Yusuph amesema kuwa wameamua kutoa msaada huo ili kuuga juhudi juhudiza serikali katika mapambano katika kukabiliana na ugonjwa huo

Hata hivyo ametoa wito kwa wananchi wengine wenye uwezo wa kuguswa na tatizo hilo wapatwe na msukumo wa kutoa msaada ili kuenndelea kujikinga virusi vya Corona visivyo na mashika.

“Sisi kama sehemu ya jamii ya Tanga tumeona tuugane na serikali katika kuhakikisha tunashirikiana kuchukua tahadhari dhidi ya COVID 19”alisisitiza Yusuph.

Aidha baadhi ya wakazi wa Jiji hilo Athony Charles na Aisha Ramadhani wameipongeza serikali ya Mkoa kwa kuendelea na juhudi za kuwaelimisha wananchi kujikinga na ugojwa huo hatari. 

Comments

Popular posts from this blog

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja

Katavi Yakemea Vikali Ushoga,Mauaji "Wanaume Msiwazuie Wake Zenu Kufanya...