Skip to main content

TANGA YAJIDHATITI NA MAPAMBANO DHIDI YA COVID 19



 
Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martin Shigella akipokea Matanki matano kutoka wa wadau wa mapambano ya COVID 19 jijini humo


Na Mwandishi Wetu
      Tanga

MKUU wa Mkoa wa Tanga Martin Shigella amepokea vifaa vya kujikinga na ugongwa wa COVID 19 ikiwa sambamba na kuwataka wafanyabiashara wengine kuguswa na kuchangia vifaa vya usafi ili kuhakikisha wanadhibiti na kuchukua hatadhati za kujikinga na ugonjwa huo.

Kauli hiyo ameitoa wakati akipokea msaada wa mataki matano ya ujazwa wa lita mia tano kila moja kutoka kampuni ya vifaa vya ujenzi ya Hussain Plastic Industry ya jijini hapa.

Shigella amasema bado kunauhitaji mkubwa wa vifaa kwa ajili ya kusabazwa  kwenye maeneo mengine ya mkoani Tanga ili wananchi waweze kujikinga na COVID 19 kupitia kunawa mikono kwa maji safi yanyotiririka .

Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Hussein Yusuph amesema kuwa wameamua kutoa msaada huo ili kuuga juhudi juhudiza serikali katika mapambano katika kukabiliana na ugonjwa huo

Hata hivyo ametoa wito kwa wananchi wengine wenye uwezo wa kuguswa na tatizo hilo wapatwe na msukumo wa kutoa msaada ili kuenndelea kujikinga virusi vya Corona visivyo na mashika.

“Sisi kama sehemu ya jamii ya Tanga tumeona tuugane na serikali katika kuhakikisha tunashirikiana kuchukua tahadhari dhidi ya COVID 19”alisisitiza Yusuph.

Aidha baadhi ya wakazi wa Jiji hilo Athony Charles na Aisha Ramadhani wameipongeza serikali ya Mkoa kwa kuendelea na juhudi za kuwaelimisha wananchi kujikinga na ugojwa huo hatari. 

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja