Skip to main content

WANANCHI WA NAMTUMBO KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJI WA BILIONI MBILI.


Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ChristinaMndeme  akikagua mradi wa maji wa Mkongogulioni Wilayani ya Namtumbo.

SERIKALI ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt.John Magufuli imetoa zaidi ya Tsh. Bilioni Mbili ili kutekeleza mradi wa Maji wa Mkongogulioni na Nakahimba Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma.

Kaimu Meneja wa RUWASA Wilaya ya Namtumbo David Mkondya akitoa taarifa ya mradi huo kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme,amesema mradi huo ulisainiwa  Juni 12 mwaka 2013 na utekelezaji wake ulianza mwaka 2017 na ulitarajiwa kukamilika Februari 2020 chini ya Mkandarasi Kipera Contractors.

Mkondya alisema mradi huo unatarajia kuhudumia watu zaidi ya 8000 katika vijiji vya Mkongogulioni na Nahimba na kwamba kazi ambazo zimepangwa kufanyika kwenye mradi huo ni ujenzi wa tanki la lita 25,000 katika kijiji cha Nahimba na ukarabati wa matanki mawili yenye ujazo wa lita 150,000 katika kijiji cha Mkongo.

Hata hivyo alizitaja kazi ambazo zimefanyika kulingana na mkataba kuwa ni uchimbaji wa mtaro katika kijiji cha Nakahimba ambao umefikia zaidi ya asilimia 83,ujenzi na ukarabati wa matanki ya kuhifadhia maji,ujenzi wa chanzo,ulazaji wa mabomba na ujenzi wa vituo 46 vya kuchotea maji.

Akizungumza mara baada ya kukagua mradi huo Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amesema ameridhishwa na mradi huo na kusisitiza kuwa serikali imetoa zaidi ya shilingi bilioni 30 kutekeleza miradi ya maji katika Mkoa wa Ruvuma.

Ali

waasa wananchi hao kuhakikisha kuwa wanalinda miundombinu ya maji na kutochoma moto au kuharibu kwenye vyanzo vya maji ili maji yaweze kutumika kwa muda mrefu bila kuwa na maji ya mgawo.

Imeandikwa na Albano Midelo
Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma
Juni 28,2020

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja