Skip to main content

WANANCHI WA NAMTUMBO KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJI WA BILIONI MBILI.


Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ChristinaMndeme  akikagua mradi wa maji wa Mkongogulioni Wilayani ya Namtumbo.

SERIKALI ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt.John Magufuli imetoa zaidi ya Tsh. Bilioni Mbili ili kutekeleza mradi wa Maji wa Mkongogulioni na Nakahimba Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma.

Kaimu Meneja wa RUWASA Wilaya ya Namtumbo David Mkondya akitoa taarifa ya mradi huo kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme,amesema mradi huo ulisainiwa  Juni 12 mwaka 2013 na utekelezaji wake ulianza mwaka 2017 na ulitarajiwa kukamilika Februari 2020 chini ya Mkandarasi Kipera Contractors.

Mkondya alisema mradi huo unatarajia kuhudumia watu zaidi ya 8000 katika vijiji vya Mkongogulioni na Nahimba na kwamba kazi ambazo zimepangwa kufanyika kwenye mradi huo ni ujenzi wa tanki la lita 25,000 katika kijiji cha Nahimba na ukarabati wa matanki mawili yenye ujazo wa lita 150,000 katika kijiji cha Mkongo.

Hata hivyo alizitaja kazi ambazo zimefanyika kulingana na mkataba kuwa ni uchimbaji wa mtaro katika kijiji cha Nakahimba ambao umefikia zaidi ya asilimia 83,ujenzi na ukarabati wa matanki ya kuhifadhia maji,ujenzi wa chanzo,ulazaji wa mabomba na ujenzi wa vituo 46 vya kuchotea maji.

Akizungumza mara baada ya kukagua mradi huo Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amesema ameridhishwa na mradi huo na kusisitiza kuwa serikali imetoa zaidi ya shilingi bilioni 30 kutekeleza miradi ya maji katika Mkoa wa Ruvuma.

Ali

waasa wananchi hao kuhakikisha kuwa wanalinda miundombinu ya maji na kutochoma moto au kuharibu kwenye vyanzo vya maji ili maji yaweze kutumika kwa muda mrefu bila kuwa na maji ya mgawo.

Imeandikwa na Albano Midelo
Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma
Juni 28,2020

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...