Skip to main content

KAMATI YA SIASA CCM RUVUMA YAKAGUA CHUO CHA VETA NYASA.



KAMATI ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma imekagua mradi wa ujenzi wa  chuo cha ufundi stadi VETA Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma ambao unagharimu zaidi ya shilingi bilioni mbili.

Akisoma taarifa ya mradi huo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nyasa,Jimson Mhagama  amesema mradi unahusisha majengo 16 na kwamba fedha za mradi zimepokelewa kwa awamu ambapo katika awamu ya kwanza zimepokelewa zaidi ya bilioni moja.

Amesema mradi huo unatekelezwa  na mafundi mawili wakiwemo SUMA JKT ambaye anajenga majengo 14 na Simon Chiwanga ambaye anajenga vyumba viwili vya madarasa na kwamba mradi umetoa jumla ya ajira 123.

                         Moja ya majengo ya karakana katika chuo cha VETA Nyasa

Mhagama amesema mradi huo unatekelezwa kwa kutumia mtindo wa force account ambapo wananchi kutoka Kata ya Kilosa ambako mradi unatekelezwa wanashiriki  na kwamba mradi ulianza Februari 21,2020 na unaarajiwa kukamilika Julai 31 mwaka huu.

Hata hivyo amesema mradi umefikia katika hatua tofauti za utekelezaji ambapo majengo saba yamefikia zaidi ya asilimia 80 ambayo ni nyumba ya Mkuu wa Chuo,kibanda cha mlinzi,vyumba viwili vya madarasa ,karakana na vyoo.

“Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa kwa kushirikiana na wananchi tunaishukuru serikali ya awamu ya tano kwa kusimamia na kutekeleza kwa vitendo Ilani ya CCM kupitia mradi huu ambao utawanufaisha vijana wa Nyasa’’,alisisitiza Mhagama.

Akizungumza mara baada ya kukagua mradi huo Katibu wa CCM Mkoa wa Ruvuma Nuru Ngeleja amewapongeza wananchi wa Wilaya ya Nyasa kwa kusimamia utekelezaji wa mradi huo ambao amesema utachochea wananchi kukiamini Chama Tawala kuendelea kutawala.


                                 Jengo la  utawala katika chuo cha VETA Nyasa

Hata hivyo Ngeleja ameushauri uongozi wa Halmashauri ya Nyasa kuhakikisha miradi yote inayotekelezwa na serikali kuhakikisha  inatangazwa na kufahamika kwa wananchi ili kutambua kazi nzuri zinazofanywa na serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo.

Naye Mjumbe wa Halmashauri Kuu  ya CCM Taifa Musa Homera ameipongeza Kampuni ya SUMA JKT kwa kutekeleza mradi huo  ambapo amesema wananchi wa Nyasa wameonesha moyo wa kujitolea katika utekelezaji wa mradi huo.

“Naomba serikali iendelee kuwaamini zaidi SUMA JKT kutokana na kutekeleza vema miradi ambayo mnapewa ,wilaya ya Nyasa inafanya vizuri katika utekelezaji miradi,inagawa,imezipita wilaya nyingine kongwe katika Mkoa wa Ruvuma’’,alisisitiza Homera.

Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma inafanya ziara ya siku tano kupita katika wilaya zote za Mkoa wa Ruvuma  kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali.

Imeandikwa na Albano Midelo
Afisa Habari wa Mkoa wa Ruvuma
Juni 30,2020

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja