Skip to main content

KAMATI YA SIASA CCM RUVUMA YAKAGUA CHUO CHA VETA NYASA.



KAMATI ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma imekagua mradi wa ujenzi wa  chuo cha ufundi stadi VETA Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma ambao unagharimu zaidi ya shilingi bilioni mbili.

Akisoma taarifa ya mradi huo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nyasa,Jimson Mhagama  amesema mradi unahusisha majengo 16 na kwamba fedha za mradi zimepokelewa kwa awamu ambapo katika awamu ya kwanza zimepokelewa zaidi ya bilioni moja.

Amesema mradi huo unatekelezwa  na mafundi mawili wakiwemo SUMA JKT ambaye anajenga majengo 14 na Simon Chiwanga ambaye anajenga vyumba viwili vya madarasa na kwamba mradi umetoa jumla ya ajira 123.

                         Moja ya majengo ya karakana katika chuo cha VETA Nyasa

Mhagama amesema mradi huo unatekelezwa kwa kutumia mtindo wa force account ambapo wananchi kutoka Kata ya Kilosa ambako mradi unatekelezwa wanashiriki  na kwamba mradi ulianza Februari 21,2020 na unaarajiwa kukamilika Julai 31 mwaka huu.

Hata hivyo amesema mradi umefikia katika hatua tofauti za utekelezaji ambapo majengo saba yamefikia zaidi ya asilimia 80 ambayo ni nyumba ya Mkuu wa Chuo,kibanda cha mlinzi,vyumba viwili vya madarasa ,karakana na vyoo.

“Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa kwa kushirikiana na wananchi tunaishukuru serikali ya awamu ya tano kwa kusimamia na kutekeleza kwa vitendo Ilani ya CCM kupitia mradi huu ambao utawanufaisha vijana wa Nyasa’’,alisisitiza Mhagama.

Akizungumza mara baada ya kukagua mradi huo Katibu wa CCM Mkoa wa Ruvuma Nuru Ngeleja amewapongeza wananchi wa Wilaya ya Nyasa kwa kusimamia utekelezaji wa mradi huo ambao amesema utachochea wananchi kukiamini Chama Tawala kuendelea kutawala.


                                 Jengo la  utawala katika chuo cha VETA Nyasa

Hata hivyo Ngeleja ameushauri uongozi wa Halmashauri ya Nyasa kuhakikisha miradi yote inayotekelezwa na serikali kuhakikisha  inatangazwa na kufahamika kwa wananchi ili kutambua kazi nzuri zinazofanywa na serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo.

Naye Mjumbe wa Halmashauri Kuu  ya CCM Taifa Musa Homera ameipongeza Kampuni ya SUMA JKT kwa kutekeleza mradi huo  ambapo amesema wananchi wa Nyasa wameonesha moyo wa kujitolea katika utekelezaji wa mradi huo.

“Naomba serikali iendelee kuwaamini zaidi SUMA JKT kutokana na kutekeleza vema miradi ambayo mnapewa ,wilaya ya Nyasa inafanya vizuri katika utekelezaji miradi,inagawa,imezipita wilaya nyingine kongwe katika Mkoa wa Ruvuma’’,alisisitiza Homera.

Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma inafanya ziara ya siku tano kupita katika wilaya zote za Mkoa wa Ruvuma  kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali.

Imeandikwa na Albano Midelo
Afisa Habari wa Mkoa wa Ruvuma
Juni 30,2020

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...