Skip to main content

Posts

Katavi: Watoto Wachanga 631 walifariki Dunia na Vifo 56 vitokanavyo na Uzazi 2020.

Baadhi ya Wadau wakisikiliza jambo kwa makini katika Kikao Kazi cha Wadau wa Afya kilichofanyika Mei 20,2021 katika Ukumbi wa Mpanda Manispaa. Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Katavi Bi. Crecensia Joseph akiwahutubia Wadau wa Afya,katika Kikao Kazi cha Wadau wa Afya. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mpanda-Katavi. Mkoa wa Katavi umeweka Mkakati wa Miaka Mitano wa kupunguza Vifo vya Mama na Mtoto ambapo jumla ya Watoto Wachanga 631 walifariki Dunia kwa kipindi cha Januari hadi Desemba 2020 na 93 walifariki kipindi cha Januari hadi Machi 2021. Akitoa hotuba Jana Mei 20,2021 mbele ya Wadau mbalimbali wa Afya Mkoani Katavi katika kikao Kazi cha Wadau wa Afya,Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Katavi Crecensia Joseph amesema Vifo 56 vilivyotokana na Uzazi vilisababishwa na kutokwa na Damu nyingi kabla na baada ya kujifungua Vifo 22,Kifafa cha Mimba Vifo 6 na Upungufu mkubwa wa Damu wakati wa Ujauzito Vifo 5. Aidha,amezitaja sababu zingine kuwa ni uambukizo mkali baada ya kujifungua Vifo 10 na Magonjwa mengine...

Taasisi 14 za kutana haraka kujadili Vifo vya Mama na Mtoto//Watoto wach...

Madaktari waeleza sababu kubwa za Vifo vya Mama na Mtoto.

WAONYWA KUTUMIA MAJINA YA VIONGOZI VIBAYA.

Na Swaum Katambo Tanganyika-Katavi Wafugaji wa Wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi wameonywa tabia ya kutumia vibaya majina ya viongozi ili kujificha katika kichaka cha uharibifu wanaofanya wa kupeleka mifugo katika mashamba ya wakulima na kuharibu mazao. Hatua hiyo inakuja mara baada ya wakulima wa Kijiji cha Majalila kulalamika na kuhoji kwa Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Salehe Mhando juu ya kero ya majibu mabaya wanayoyapata kutoka kwa wafugaji pindi wanapo wakamata wafugaji wakilisha mifugo yao kwenye mazao na kujibiwa "Hata mfanye nini hamna pa kutupeleka kwanza mifugo hii ni ya Mkuu wa Wilaya". Ili kuondoa Mgogoro huo baina ya Wakulima na Wafugaji DC Mhando amewaagiza Mtendaji wa Kijiji na Mtendaji wa Kata kuwatambua kwa majina wafugaji wote waliopo Tanganyika pamoja na mifugo yao ili kuwapangia maeneo ya vitalu kwa ajili ya kulisha mifugo yao. Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Salehe Mhando akizungumza na wakulima wa  wa Kijiji cha Majalila. Katika hatua nyingine wakulima wa ...

WAKAGUZI WA NYAMA WANATUZINGUA.

Na Zainabu Mtima, Site Tv-Mlele Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi wamekutana kujadili shughuli za maendeleo katika robo Tatu ya Mwaka wa Fedha 2021. Miongoni mwa mambo yaliyojadiliwa ni pamoja na utekelezaji wa miradi mbalimbali katika Kata zote Sita za Halmashauri hiyo. Akizungumza katika Baraza hilo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mlele Soud Mbogo amesema kumekuwa na changamoto ya uchache wa Wataalamu wa ukaguzi wa Nyama jambo lililomfanya atoe azimio la kuwatoa kwenye huduma ya ukaguzi wa nyama wataalamu wote waliopo sasa na kutafutwa wengine watakaofanya kazi kwa uweledi. Akitolea ufafanuzi changamoto hiyo Afisa Mifugo na Uvuzi wa Wilaya,Livingstone Mandari amesema Idara ya Mifugo   na Uvuvi inaupungufu mkubwa wa Watumishi jambo linalowafanya waelemewe na kazi ya ukaguzi wa Nyama. Aidha Livingstone ameongeza kuwa ukaguzi wa Nyama unatakiwa ufanywe na mtaalam aliyesomea Afya ya Wanyama ambapo kwa Halmshauri nzima ya Wilaya ya Mlele yuko Mtaa...

Aliyekodi watu na kumuua baba yake ahukumiwa kunyongwa.

Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga, imemhukumu Seni Lisesi adhabu ya kunyongwa hadi kufa baada ya kumtia hatiani kuhusika na mauaji ya baba yake mzazi. Lisesi (33) mkazi wa Kijiji cha Mwadui wilayani Sumbawanga, alidaiwa kuhusika kwenye mauaji ya baba yake Lisesi Magadula (50) ili arithi mali. Hukumu hiyo imetolewa jana Jumanne ya Mei 18, 2021 na Jaji wa Mahakama hiyo Dustan Ndunguru baada ya kuridhika na ushahidi uliowasilishwa na upande wa mashitaka ukiongozwa na mawakili wa Serikali, Njoloyota Mwashubila na Irene Mwabeza. Kwa mujibu wa hati ya mashitaka iliyowasilishwa mahakamani hapo, inaeleza kuwa Lisesi alitenda kosa la mauaji ya Magadula kwa kushirikiana na kikundi cha watu. Ilidaiwa kuwa Liseni alikodisha kikundi hicho kwa ajili ya kufanya mauaji hayo mnamo Desemba 4, 2016 nyumbani kwa marehemu huko Kijiji cha Mwadui. Ilidaiwa na waendesha mashitaka wa Serikali kwamba muuaji akiwa na wenzake walivamia nyumbani kwa Liseni nyakati za usiku wakiwa silaha aina ya mapanga na kumkataka...

RAIS DK.MWINYI AMEFANYA ZIARA MAENEO YA MRADI WA MANGAPWANI.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amefanya ziara katika eneo linalotarajiwa kujengwa bandari mpya ya Magapwani na kueleza kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itatoa maamuzi yenye tija kwa ajili ya muendelezo wa eneo hilo. Rais Dk. Mwinyi aliyasema hayo jana Mei 18,2021, mara baada ya kufanya ziara ya kulitembelea eneo linalotarajiwa kujengwa bandari mpya ya Mangapwani, Wizaya ya Kaskazini B,Mkoa wa Kaskazini Unguja ambapo pia, alitembelea miradi ambayo imeanza kabla ya ujenzi huo mpya. Katika maelezo yake Rais Dk. Mwinyi alisema kuwa Serikali itakuja na maamuzi yenye tija ambayo yatasaidia kwa pande sote mbili ikiwemo upande wa wawekezaji ambao walianza kuekeza kwa muda mrefu katika eneo hilo pamoja na kwa upande wa Serikali kwa ujumla huku akiwataka wawekezaji hao kuwa na subira . Rais Dk. Mwinyi alisema kuwa Serikali imeridhishwa na ukubwa wa eneo pamoja na hatua ya awali iliyofikiwa na kuelez ajambo kubwa lililompelekea kufanya ziara h...