Skip to main content

WAKAGUZI WA NYAMA WANATUZINGUA.

Na Zainabu Mtima,Site Tv-Mlele

Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi wamekutana kujadili shughuli za maendeleo katika robo Tatu ya Mwaka wa Fedha 2021.

Miongoni mwa mambo yaliyojadiliwa ni pamoja na utekelezaji wa miradi mbalimbali katika Kata zote Sita za Halmashauri hiyo.

Akizungumza katika Baraza hilo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mlele Soud Mbogo amesema kumekuwa na changamoto ya uchache wa Wataalamu wa ukaguzi wa Nyama jambo lililomfanya atoe azimio la kuwatoa kwenye huduma ya ukaguzi wa nyama wataalamu wote waliopo sasa na kutafutwa wengine watakaofanya kazi kwa uweledi.

Akitolea ufafanuzi changamoto hiyo Afisa Mifugo na Uvuzi wa Wilaya,Livingstone Mandari amesema Idara ya Mifugo  na Uvuvi inaupungufu mkubwa wa Watumishi jambo linalowafanya waelemewe na kazi ya ukaguzi wa Nyama.

Aidha Livingstone ameongeza kuwa ukaguzi wa Nyama unatakiwa ufanywe na mtaalam aliyesomea Afya ya Wanyama ambapo kwa Halmshauri nzima ya Wilaya ya Mlele yuko Mtaalamu Mmoja tu .

Hata hivyo Afisa Mifugo amesema changamoto ilipotokea kwa wachinjaji ni kutofahamu uchache wa wakaguzi wa Nyama uliopo kwani waliopo hufanya kazi zaidi ya Moja.

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...