Skip to main content

WAKAGUZI WA NYAMA WANATUZINGUA.

Na Zainabu Mtima,Site Tv-Mlele

Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi wamekutana kujadili shughuli za maendeleo katika robo Tatu ya Mwaka wa Fedha 2021.

Miongoni mwa mambo yaliyojadiliwa ni pamoja na utekelezaji wa miradi mbalimbali katika Kata zote Sita za Halmashauri hiyo.

Akizungumza katika Baraza hilo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mlele Soud Mbogo amesema kumekuwa na changamoto ya uchache wa Wataalamu wa ukaguzi wa Nyama jambo lililomfanya atoe azimio la kuwatoa kwenye huduma ya ukaguzi wa nyama wataalamu wote waliopo sasa na kutafutwa wengine watakaofanya kazi kwa uweledi.

Akitolea ufafanuzi changamoto hiyo Afisa Mifugo na Uvuzi wa Wilaya,Livingstone Mandari amesema Idara ya Mifugo  na Uvuvi inaupungufu mkubwa wa Watumishi jambo linalowafanya waelemewe na kazi ya ukaguzi wa Nyama.

Aidha Livingstone ameongeza kuwa ukaguzi wa Nyama unatakiwa ufanywe na mtaalam aliyesomea Afya ya Wanyama ambapo kwa Halmshauri nzima ya Wilaya ya Mlele yuko Mtaalamu Mmoja tu .

Hata hivyo Afisa Mifugo amesema changamoto ilipotokea kwa wachinjaji ni kutofahamu uchache wa wakaguzi wa Nyama uliopo kwani waliopo hufanya kazi zaidi ya Moja.

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja