Skip to main content

Aliyekodi watu na kumuua baba yake ahukumiwa kunyongwa.

kunyongwa pcMahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga, imemhukumu Seni Lisesi adhabu ya kunyongwa hadi kufa baada ya kumtia hatiani kuhusika na mauaji ya baba yake mzazi.

Lisesi (33) mkazi wa Kijiji cha Mwadui wilayani Sumbawanga, alidaiwa kuhusika kwenye mauaji ya baba yake Lisesi Magadula (50) ili arithi mali.

Hukumu hiyo imetolewa jana Jumanne ya Mei 18, 2021 na Jaji wa Mahakama hiyo Dustan Ndunguru baada ya kuridhika na ushahidi uliowasilishwa na upande wa mashitaka ukiongozwa na mawakili wa Serikali, Njoloyota Mwashubila na Irene Mwabeza.
Kwa mujibu wa hati ya mashitaka iliyowasilishwa mahakamani hapo, inaeleza kuwa Lisesi alitenda kosa la mauaji ya Magadula kwa kushirikiana na kikundi cha watu.
Ilidaiwa kuwa Liseni alikodisha kikundi hicho kwa ajili ya kufanya mauaji hayo mnamo Desemba 4, 2016 nyumbani kwa marehemu huko Kijiji cha Mwadui.
Ilidaiwa na waendesha mashitaka wa Serikali kwamba muuaji akiwa na wenzake walivamia nyumbani kwa Liseni nyakati za usiku wakiwa silaha aina ya mapanga na kumkatakata hadi kufariki huku lengo likiwa ni kurithi mali mbalimbali ikiwemo ng'ombe na mashamba.
Hata hivyo, Polisi katika uchunguzi wao walimtia mbaroni Liseni na kumfikisha katika vyombo vya sheria.
Katika kesi hiyo, upande wa mashitaka ulipeleka mashahidi wanne huku Lisesi akiwakilishwa na Wakili wa kujitegemea Neema Charles, ambapo alijitetea kuwa hakushiriki katika mauaji hayo akiiomba mahakama kumuachia huru.
Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo, waendesha mashitaka wa Serikali waliomba mahakama kutoa adhabu kali ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia za kushiriki kukatisha uhai wa wazazi wao kwa tamaa za kurithi mali.
Akisoma hukumu hiyo, Jaji Ndunguru alisema ameridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo pasi kuacha shaka na amemkuta mtuhumiwa na hatia ya kufanya mauaji ya kukusudia hivyo kwa kutumia kifungu cha 196 cha kanuni ya adhabu sura ya 16 na kifungu cha 197 anahukumiwa kunyongwa hadi kufa.
CHANZO:GAZETI LA MWANANCHI

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...