Skip to main content

Posts

DC TANGANYIKA AWAOMBA WANANCHI KUCHUKUA HATUA KUJILINDA NA EBOLA KAMA WANANVYO JILINDA NA CORONA

Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Mbwana Saleh Mhando akizungumza na waadishi wa habari ofisini kwake huku akihimiza wananchi kujikinga na ugonjwa wa COVID 19 pamoja na EBOLA. Na George Mwigulu,Tanganyika. Wananchi wa   Wilaya ya   Tanganyika Mkoani Katavi wametakiwa kuendelea kuchukua hatua madhubuti za kupambana na kujikinga na ugonjwa wa COVID 19 pamoja na Ebola wawapo sehemu za mikusanyiko hususani minadani. Hayo aliyasema Mkuu wa wilaya ya hiyo Mbwana Saleh Mhando wakati akizungumza na Wanahabari ofisi kwake katika kata ya Ifukutwa ambapo aliwataka wakazi hao kuwa waangalifu pamoja na   kuchukua tahadhari kubwa wakati huu ugonjwa wa corona unapoendelea kuenea hapa nchini. Mkuu wa wilaya hiyo alieleza kuwa kutokana na wilaya ya Tanganyika kupakana na nchi ya DRC Congo ambayo imeshuhudiwa pia na   maambukizi ya COVID 19 pamoja na ugonjwa wa Ebola.Hatua madhubuti zinatakiwa kuchukuliwa na wananchi za kujikinga pasipo kuiachia jukumu hilo pekee serikal...

WAHUKUMIWA JELA KIFUNGO CHA MAISHA KWA KOSA LA UBAKAJI

Na Mwandishi Wetu Katavi  Mahakama ya Hakimu  Mkazi Katavi imewahukumu watu wawili  Swalehe Idd(29( Mkazi wa Mtaa wa Ilembo na  Mess Ntinka (23)mkazi wa Mtaa wa Kasimba tumikia kfungo cha maisha  jela baada ya kupatikana na hatia  ya kumbaka kwa kushirikiana zamu zamu msiichana mwenye   umri wa miaka 15 kwenye stendi ya mabasi ya Manispaa ya Mpanda ya Mizengo Pinda      Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu MkazI mfawidhii wa Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Katavi Emanuel  Ngigwana baada ya Mahakama kuridhika na ushahidi uliotplewa mahakamani hapo na upande wa  mashitaka ulikuwa ukiongozwa na mwendesha mashitaka wa kutoka ofisi ya  mwendesha mashitaka Mkoa wa Katavi   Lungano Mwasubila  Washitakiwa hao wote wawili wamehukumu kutumikia kifungo hicho cha maisha jela kuanzia jana baada ya kupatikana na hatia ya kutenda kosa la kifungu cha sheria namba 131 (1) (131A) ...

DC MATINGA ATANGAZA VITUO VYA KUNUNULIA MAZAO HUKU ALIPIGA MARUFUKU KUFANYA BIASHARA BILA LESENI

Na   George Mwigulu              Katavi .  Serikali ya Wilaya ya Mpanda Mkoani Katavi imetangaza vituo  65 vitakavyo tumika kwa ajiri ya ununuzi wa mazao mbalimbali katika msimu huu wa kilimo wa 2019/ 2020 na vituo  16 vya mazao ya stakabadhi gharani ili kumfanya mkulima asiibiwe na kuzifanya Halmashauri za Wilaya hiyo kudhibiti mapato yake na pia imepiga marufuku mfanya biashara yeyote kununua mazao bila kuwa na leseni  Vituo hivyo vilitangazwa hapo Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Lilian Charles Matinga wakati alipokuwa akiongea na  wandishi wa Habari wa vyombo mbalimbali vilivyopo katika Mkoa huu kikao ambacho kilihudhuliwa pia na Wakurugenzi wa Halmashauri  za  Manispaa ya Mpanda na Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo  Alisema  Halmashauri  mbili zilizopo katika Wilayah ii wamekuwa wakipoteza mapato yao  kutokana na wafanya biashara wanao nunua ...

MHUBIRI AUWAWA AKITOA HUDUMA YA KUHUBIRI NJILI KWENYE CLABU CHA POMBE ZA KIENYEJI.

Na Mwandishi wetu       IRINGA MAUWAJI   ya  kinyama yafanyika   usiku  wa   ijumaa  kuu   Mkoa wa Iringa eneo la Kijiweni kata ya Kwakilosa katika Manispaa ya  Iringa  baada ya mhubiri  wa injili na mgombea ubunge mtarajiwa katika  jimbo la Kalenga   Raymond Mdota (46)  kuuwawa  kwa  kuchinjwa shingo yake akiwa katika  huduma ya kuhubiri injili kwenye  klabu  cha Pombe za kienyeji na  mwili  wake kutupwa kwenye mahindi. Mashuhuda  wa  tukio  hilo  waliozungumza na mwandishi  wa  habari hizi eneo la  tukio  walisema kuwa tukio hilo lilitokea  usiku  wa Ijumaa na  nje ya  chumba  kimoja wapo  ch...

APATWA NA MAUTI KWA KUPIGWA NA RADI AKIENDESHA PIKIPIKI BARABARANI.

 Na Mwandishi Wetu.          Katavi. MTU   mmoja   Mkazi wa Mtaa wa Mpanda Hotel  katika Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi aliyejulikana kwa jina la  Paulo  Chundu   amekufa hapo hapo baada ya kupigwa na radi akiwa anaaendesha pikipiki wakati akitokea kwenye shamba la mpunga .  Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Benjamin  Kuzaga aliwaambia wandishi wa habari kuwa tukio la kifo cha marehemu huyo  lilitokea hapo juzi majira ya saa 12  jioni katika eneo la  Kalilankuluku Tarafa ya Kabungu Wilaya ya Tanganyika .  Kuzaga alieleza kuwa kabla ya tukio hilo marehemu huyo alikuwa ameaga nyumbani kwake kuwa anapeleka chakula  kwenye shamba lake la mpunga kwa ajiri ya chakula  cha vibarua waliokuwa wakifanya kazi kwenye shamba hilo .  Baada ya kuwa ameaga nyumbani kwake marehemu huyo alipakia chakula hicho kwenye pikipiki  yake na kuelekea kwenye shamba hi...