Mahakama
ya Hakimu Mkazi Katavi imewahukumu watu wawili Swalehe Idd(29(
Mkazi wa Mtaa wa Ilembo na Mess Ntinka (23)mkazi wa Mtaa wa Kasimba
tumikia kfungo cha maisha jela baada ya kupatikana na hatia ya
kumbaka kwa kushirikiana zamu zamu msiichana mwenye umri wa miaka
15 kwenye stendi ya mabasi ya Manispaa ya Mpanda ya Mizengo Pinda
Hukumu
hiyo imetolewa na Hakimu MkazI mfawidhii
wa Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Katavi Emanuel Ngigwana baada ya
Mahakama kuridhika na ushahidi uliotplewa mahakamani hapo na upande wa
mashitaka ulikuwa ukiongozwa na mwendesha mashitaka wa kutoka ofisi ya
mwendesha mashitaka Mkoa wa Katavi Lungano Mwasubila
Washitakiwa
hao wote wawili wamehukumu kutumikia kifungo hicho cha maisha jela kuanzia
jana baada ya kupatikana na hatia ya kutenda kosa la kifungu cha sheria namba
131 (1) (131A) (2) sura ya 16 cha shereria ya
majejeo ya mwaka 2002
Awali
kwenye kesi hiyo mwendesha mashitaka huyo alidai kuwa washitakiwa hao
walitenda kosa hilo hapo januari 24 mwaka huu majira
ya saa huko katika eneo la stendi kuu ya mabasi ya Mkoa wa Katavi
Mizengo Pinda iliyoko katika Mtaa wa Ilembo Manispaa ya Mpanda
Siku
hiyo ya tukio msichana huyo alikuwa akitokea Mkoani Songwe kama abiria akiwa
anaelekea Mkoani Kigoma chini ya uangalizi wa Kondakta wa basi hilo alilokuwa
akisafiria .
Mwendesha
mashita MwasubIla alieleza kuwa baada ya msichana huyo kuwa amefika kwenye
stendi ya Mizengo Pinda walijitokeza washitakiwa hao ambao walikuwa ni
maajenti wa mabasi yaendayo Mikoani na kumweleza kondakta huyo kuwa wao
ni maafisa wa usalama wa stendi hiyo hivyo wanamwomba binti huyo awe mikononi
mwao kwani atakuwa yuko kwenye mikono salama hadi hapo siku ilifuata ambayo
wangemsafirisha kwenda kwao kigoma kwa mabasi yaendayo huko .
Baada
ya kuwa wamekabidhi binti huyo washitakiwa hao walimchukua na kumpeleka
hadi kwenye chumba kimoja kilichopo kwenye stendi hiyo na kisha walianza
kumbaka kwa zamu zamu hadi hapo walipomaliza haja yao .
Mwendesha
mashitaka alidai kuwa baada ya kuwa wamemfanyia kitendo hicho
walimtolea maneno ya vitisho kuwa asiwaambie watu vinginevyo watamuuwa
hata hivyo baada ya kuwa amefika Mkoani Kigoma kwa wazazi wake
aliwaeleza jinsi alivyofanyiwa kitendo hicho kwa kubakwa ndipo taarifa
zilitolewa polisi na watuhumiwa walianza kusakwa na kukamatwa.
Upande wa mashitaka kwenye kesi hiyo ulikuwa na mashahidi wanne akiwemo
daktari aliyemfanyia uchunguzi msichana huyo pamoja na muhanga mwenyewe
wa tukio hilo.
Kabla
ya kutowa hukumu hiyo hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu
Mkazi Katavi Emanuel Ngigwana alitowa nafasi kwa watuhumiwa
kuweza kujitetea kama wanayosababu ya msingi ya kuwafanya wapunguziwe adhabu
.
Katika utetezi wao waliiomba mahakama iwapunguzie adhabu kwa kile walchodai
kuwa wanafamilia ambayoinawategemea na pia umri wao ni mdogo
maombi hayo ambayo yalipingw na mwendesha mashitaka Mwasubila ambae
aliiomba mahakama itowe adhabu kali kwa washitakiwa
Hakimu
Ngiwana baada ya kusikiliza utetezi huo aliiambia Mahakama kuwa kosa
walilopatikanalo watumiwa kifungo chake ni cha kutumikia kwenda jela maisha
|
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Comments
Post a Comment