Skip to main content

WAHUKUMIWA JELA KIFUNGO CHA MAISHA KWA KOSA LA UBAKAJI













Na Mwandishi Wetu







Katavi
 Mahakama ya Hakimu  Mkazi Katavi imewahukumu watu wawili  Swalehe Idd(29( Mkazi wa Mtaa wa Ilembo na  Mess Ntinka (23)mkazi wa Mtaa wa Kasimba tumikia kfungo cha maisha  jela baada ya kupatikana na hatia  ya kumbaka kwa kushirikiana zamu zamu msiichana mwenye   umri wa miaka 15 kwenye stendi ya mabasi ya Manispaa ya Mpanda ya Mizengo Pinda   

  Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu MkazI mfawidhii wa Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Katavi Emanuel  Ngigwana baada ya Mahakama kuridhika na ushahidi uliotplewa mahakamani hapo na upande wa  mashitaka ulikuwa ukiongozwa na mwendesha mashitaka wa kutoka ofisi ya  mwendesha mashitaka Mkoa wa Katavi   Lungano Mwasubila

 Washitakiwa hao wote wawili wamehukumu kutumikia kifungo hicho cha maisha jela kuanzia jana baada ya kupatikana na hatia ya kutenda kosa la kifungu cha sheria namba 131 (1) (131A)   (2) sura ya 16 cha shereria ya majejeo ya mwaka 2002

  Awali kwenye kesi hiyo mwendesha mashitaka huyo alidai kuwa washitakiwa hao walitenda kosa hilo hapo  januari  24 mwaka huu   majira ya saa   huko katika eneo la stendi kuu ya mabasi ya Mkoa wa Katavi Mizengo Pinda iliyoko katika Mtaa wa Ilembo Manispaa ya Mpanda

 Siku hiyo ya tukio msichana huyo alikuwa akitokea Mkoani Songwe kama abiria akiwa anaelekea Mkoani Kigoma chini ya uangalizi wa Kondakta wa basi hilo alilokuwa akisafiria .

 Mwendesha mashita MwasubIla alieleza kuwa baada ya msichana huyo kuwa amefika kwenye stendi ya Mizengo Pinda walijitokeza washitakiwa hao ambao walikuwa ni  maajenti wa mabasi yaendayo Mikoani na kumweleza  kondakta huyo kuwa wao ni maafisa wa usalama wa stendi hiyo hivyo wanamwomba binti huyo awe mikononi mwao kwani atakuwa yuko kwenye mikono salama hadi hapo siku ilifuata ambayo wangemsafirisha kwenda kwao kigoma kwa mabasi yaendayo huko .

  Baada ya kuwa wamekabidhi  binti huyo washitakiwa hao walimchukua na kumpeleka hadi kwenye chumba kimoja kilichopo kwenye stendi hiyo na kisha walianza kumbaka kwa zamu zamu hadi hapo walipomaliza  haja yao .

 Mwendesha mashitaka alidai kuwa baada ya kuwa wamemfanyia kitendo hicho walimtolea  maneno ya vitisho kuwa asiwaambie watu vinginevyo watamuuwa hata hivyo baada ya kuwa amefika Mkoani Kigoma kwa wazazi wake aliwaeleza  jinsi alivyofanyiwa kitendo hicho kwa kubakwa ndipo taarifa zilitolewa polisi na watuhumiwa walianza kusakwa na kukamatwa.

 Upande wa mashitaka kwenye kesi hiyo ulikuwa na mashahidi wanne akiwemo daktari  aliyemfanyia uchunguzi msichana huyo pamoja na muhanga mwenyewe wa tukio hilo.

 Kabla ya kutowa hukumu hiyo hakimu Mkazi  Mfawidhi wa Mahakama ya  Hakimu Mkazi  Katavi  Emanuel Ngigwana alitowa nafasi kwa watuhumiwa kuweza kujitetea kama wanayosababu ya msingi ya kuwafanya wapunguziwe adhabu .

 Katika utetezi wao waliiomba mahakama iwapunguzie adhabu kwa kile walchodai kuwa  wanafamilia ambayoinawategemea na pia umri wao ni mdogo  maombi hayo ambayo yalipingw na mwendesha mashitaka Mwasubila ambae aliiomba mahakama itowe adhabu kali kwa washitakiwa 

 Hakimu  Ngiwana baada ya kusikiliza utetezi huo aliiambia Mahakama kuwa kosa walilopatikanalo watumiwa kifungo chake ni cha kutumikia kwenda jela maisha


Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja