Na George Mwigulu
Katavi .
Serikali
ya Wilaya ya Mpanda Mkoani Katavi imetangaza vituo 65
vitakavyo tumika kwa ajiri ya ununuzi wa mazao mbalimbali katika msimu huu wa
kilimo wa 2019/ 2020 na vituo 16 vya mazao ya stakabadhi gharani ili
kumfanya mkulima asiibiwe na kuzifanya Halmashauri za Wilaya hiyo kudhibiti
mapato yake na pia imepiga marufuku mfanya biashara yeyote kununua mazao bila
kuwa na leseni
Vituo
hivyo vilitangazwa hapo Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Lilian Charles Matinga
wakati alipokuwa akiongea na wandishi wa Habari wa vyombo mbalimbali
vilivyopo katika Mkoa huu kikao ambacho kilihudhuliwa pia na Wakurugenzi wa
Halmashauri za Manispaa ya Mpanda na Halmashauri ya Wilaya ya
Nsimbo
Alisema
Halmashauri mbili zilizopo katika Wilayah ii wamekuwa wakipoteza mapato
yao kutokana na wafanya biashara wanao nunua mazao kwenye
Halmashauri hizo kuwa wadanganyifu na kuzifanya Halmashauri kupoteza
mapato pia mkulima amekuwa akipunjika bei kutokana na wafanya
biashara kununua mazao bila kuwa na vipimo halali vya mizani.
Lengo
la kuweka vituo hivyo ni kutataka Halmashauri ziweze
kukusanya mapato vizuri pamoja na fedha za maendeleo na kumsaidia
mkulima asipunjwe kwenye bei na vipimo ambapo apo awali wafanya biashara
walikuwa wakinunua mazao kwa kutumia ndoo ambazo sio vipimo halisi
.
Matinga
alifafanua kuwa jumla ya vituo 53 vimeandaliwa kwa ajiri ya ununuzi wa
mazao ya Mahindi , Karanga , Mpunga na muhogo
katika Halmashauri hizo mbili ambapo Manispaa ya Mpanda itakuwa na
vituo 26 na Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo itakuwa na vituo 27.
Pia
wameweka vituo 16 kwa ajiri ya mazao ya yatakayo uzwa kwa
stakabadhi gharani kwenye Halmashauri hizo ambapo mazao hayo
yatahusu ufuta na alizeti .
DC
Matinga alisisitiza kuwa hakuna mfanyabiashara yeyote ambae ataruhusiwa
kununa mazao kwenye Wilaya hiyo bila kuwa na leseni ya biashara kutoka kwenye
Halmashauri husika pia amepiga marufuku wafanya biashara
kununua mazao kwa kutumia ndoo za plasitiki wala kutumia mizani ambayo
haija kaguliwa.
Amepiga
marufuku kwenye maeneo hayo watu ambao wamekuwa wakijifanya wao kuwa ni
madalali wa kuwanunulia wafanya biashara mazao kuwepo kwenye vituo hivyo kwani
wamekuwa wakisababisha mkulima kuibiwa
Mkurugenzi wa Manispaa ya Mpanda
Michael Nzyungu alisema Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda imeweka
utaratibu wa mtu kwa wafanya biashara anae taka kununu mazao ni lazima
awe na leseni ya biashara ya kununua mazao hayo ambayo atakuwa analipia
leseni tshs 100,000 .
Alifafanua
kuwa mazao ambayo yatakuwa ni ya mkulima ambayo hayazidi tani
moja hawata yatoza ushuru kama ambavyo Rais alivyoagiza isipokuwa kwa
mfanyabiashara yeyote atakae nunua atatozwa ushuru hata kama mazao hayazidi
tani moja .
Aliwaonya
wafanya biashara ambao watafanya ujanja wa kufanya biashara bila kuwa na leseni
watambue kuwa endapo watakamatwa mazao yao yote yatataifishwa.
Alisema
kwa wale wafanya biashara watakao kuwa wamenunua mazao kwenye Halmashauri hiyo
na kutaka kuyasafirisha nje ya Mkoa wa Katavi ni lazima wawe na kibali ambacho
kitakuwa kinatolewa na Mkuu wa Wilaya

Comments
Post a Comment