Skip to main content

DC TANGANYIKA AWAOMBA WANANCHI KUCHUKUA HATUA KUJILINDA NA EBOLA KAMA WANANVYO JILINDA NA CORONA




Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Mbwana Saleh Mhando akizungumza na waadishi wa habari ofisini kwake huku akihimiza wananchi kujikinga na ugonjwa wa COVID 19 pamoja na EBOLA.

Na George Mwigulu,Tanganyika.
Wananchi wa  Wilaya ya  Tanganyika Mkoani Katavi wametakiwa kuendelea kuchukua hatua madhubuti za kupambana na kujikinga na ugonjwa wa COVID 19 pamoja na Ebola wawapo sehemu za mikusanyiko hususani minadani.
Hayo aliyasema Mkuu wa wilaya ya hiyo Mbwana Saleh Mhando wakati akizungumza na Wanahabari ofisi kwake katika kata ya Ifukutwa ambapo aliwataka wakazi hao kuwa waangalifu pamoja na  kuchukua tahadhari kubwa wakati huu ugonjwa wa corona unapoendelea kuenea hapa nchini.
Mkuu wa wilaya hiyo alieleza kuwa kutokana na wilaya ya Tanganyika kupakana na nchi ya DRC Congo ambayo imeshuhudiwa pia na  maambukizi ya COVID 19 pamoja na ugonjwa wa Ebola.Hatua madhubuti zinatakiwa kuchukuliwa na wananchi za kujikinga pasipo kuiachia jukumu hilo pekee serikali yao.
Mhando amefafanua kuwa hadi sasa kunawageni pekee watatu kutoka nchi ya DRC Congo ambao wote kwa pamoja wamehifadhiwa kwenye kituo cha Afya Karema kwa uagalizi wa kitabibu (Karatini)wa siku kumi na nne.
Philipo Mihayo ambaye ni Afisa Mazingira na Msimamizi wa kituo cha ukaguzi wa wageni wanao ingia kutoka Mkoa wa Kigoma na maeneo ya Mwambao wa Ziwa Tanganyika amewataka wasafiri kuendelea kuchukua hatua za kujikinga wawapo safarini  ikiwa pamoja na kunawa mikono na kutogusana.
Pamoja na hayo Philipo amewapongeza wasafiri wote kwa kuwa na hamasa ya kujilinda kwa kunawa mikono kwa maji safi na sabuni bila kushurutishwa kwa mguvu katika maeneo yote yaliyotengwa kwa ukaguzi.
Elias Athony ambaye ni msafiri kutoka Mkoa wa Kigoma kwenda Mpanda aliyeshuka kwenye kizuizi cha  Kabungu kutii agizo la serikali la  kunawa mikono na kupimwa joto lake la mwili ameishukuru serikali ya wilaya ya Tanganyika kwa namna walivyojipanga kudhibiti COVID 19.
Vile vile Elias ameiomba serikali kuzidi kuchukua hatua zaidi za kuwaelimisha wananchi madhara yatokanayo na COVID 19 jinsi ambavyo janga hilo la dunia linaweza kuathiri uchumi wao na taifa kwa ujumla.
Esther Charles ambaye naye ni msafiri aliye tii agizo la serikali alisema kuwa watu wasijisahau kujilinda na magonjwa mengine ambayo ni hatari zaidi kama vile UKIMWI na EBOLA kwani kupambana pekee na COVID 19 hakutasaidia kama kuna vifo vitazidi kushuhudiwa vya magonjwa hayo.
Aidha ameiomba serikali kutumia njia hiyo hiyo ambayo wanaitumia kuhamasisha wananchi kujilinda na COVID 19 pia waitumie katika kuelimisha wananchi kujilinda na magonjwa mengine.

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja