Skip to main content

DC TANGANYIKA AWAOMBA WANANCHI KUCHUKUA HATUA KUJILINDA NA EBOLA KAMA WANANVYO JILINDA NA CORONA




Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Mbwana Saleh Mhando akizungumza na waadishi wa habari ofisini kwake huku akihimiza wananchi kujikinga na ugonjwa wa COVID 19 pamoja na EBOLA.

Na George Mwigulu,Tanganyika.
Wananchi wa  Wilaya ya  Tanganyika Mkoani Katavi wametakiwa kuendelea kuchukua hatua madhubuti za kupambana na kujikinga na ugonjwa wa COVID 19 pamoja na Ebola wawapo sehemu za mikusanyiko hususani minadani.
Hayo aliyasema Mkuu wa wilaya ya hiyo Mbwana Saleh Mhando wakati akizungumza na Wanahabari ofisi kwake katika kata ya Ifukutwa ambapo aliwataka wakazi hao kuwa waangalifu pamoja na  kuchukua tahadhari kubwa wakati huu ugonjwa wa corona unapoendelea kuenea hapa nchini.
Mkuu wa wilaya hiyo alieleza kuwa kutokana na wilaya ya Tanganyika kupakana na nchi ya DRC Congo ambayo imeshuhudiwa pia na  maambukizi ya COVID 19 pamoja na ugonjwa wa Ebola.Hatua madhubuti zinatakiwa kuchukuliwa na wananchi za kujikinga pasipo kuiachia jukumu hilo pekee serikali yao.
Mhando amefafanua kuwa hadi sasa kunawageni pekee watatu kutoka nchi ya DRC Congo ambao wote kwa pamoja wamehifadhiwa kwenye kituo cha Afya Karema kwa uagalizi wa kitabibu (Karatini)wa siku kumi na nne.
Philipo Mihayo ambaye ni Afisa Mazingira na Msimamizi wa kituo cha ukaguzi wa wageni wanao ingia kutoka Mkoa wa Kigoma na maeneo ya Mwambao wa Ziwa Tanganyika amewataka wasafiri kuendelea kuchukua hatua za kujikinga wawapo safarini  ikiwa pamoja na kunawa mikono na kutogusana.
Pamoja na hayo Philipo amewapongeza wasafiri wote kwa kuwa na hamasa ya kujilinda kwa kunawa mikono kwa maji safi na sabuni bila kushurutishwa kwa mguvu katika maeneo yote yaliyotengwa kwa ukaguzi.
Elias Athony ambaye ni msafiri kutoka Mkoa wa Kigoma kwenda Mpanda aliyeshuka kwenye kizuizi cha  Kabungu kutii agizo la serikali la  kunawa mikono na kupimwa joto lake la mwili ameishukuru serikali ya wilaya ya Tanganyika kwa namna walivyojipanga kudhibiti COVID 19.
Vile vile Elias ameiomba serikali kuzidi kuchukua hatua zaidi za kuwaelimisha wananchi madhara yatokanayo na COVID 19 jinsi ambavyo janga hilo la dunia linaweza kuathiri uchumi wao na taifa kwa ujumla.
Esther Charles ambaye naye ni msafiri aliye tii agizo la serikali alisema kuwa watu wasijisahau kujilinda na magonjwa mengine ambayo ni hatari zaidi kama vile UKIMWI na EBOLA kwani kupambana pekee na COVID 19 hakutasaidia kama kuna vifo vitazidi kushuhudiwa vya magonjwa hayo.
Aidha ameiomba serikali kutumia njia hiyo hiyo ambayo wanaitumia kuhamasisha wananchi kujilinda na COVID 19 pia waitumie katika kuelimisha wananchi kujilinda na magonjwa mengine.

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...