Skip to main content

APATWA NA MAUTI KWA KUPIGWA NA RADI AKIENDESHA PIKIPIKI BARABARANI.



 Na Mwandishi Wetu.

         Katavi.


MTU  mmoja   Mkazi wa Mtaa wa Mpanda Hotel  katika Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi aliyejulikana kwa jina la  Paulo  Chundu  amekufa hapo hapo baada ya kupigwa na radi akiwa anaaendesha pikipiki wakati akitokea kwenye shamba la mpunga .

 Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Benjamin  Kuzaga aliwaambia wandishi wa habari kuwa tukio la kifo cha marehemu huyo  lilitokea hapo juzi majira ya saa 12  jioni katika eneo la  Kalilankuluku Tarafa ya Kabungu Wilaya ya Tanganyika .

 Kuzaga alieleza kuwa kabla ya tukio hilo marehemu huyo alikuwa ameaga nyumbani kwake kuwa anapeleka chakula  kwenye shamba lake la mpunga kwa ajiri ya chakula  cha vibarua waliokuwa wakifanya kazi kwenye shamba hilo .

 Baada ya kuwa ameaga nyumbani kwake marehemu huyo alipakia chakula hicho kwenye pikipiki  yake na kuelekea kwenye shamba hilo la mbuga ya mpunga lililoko katika Kijiji cha Ikaka na alifika salama  kwenye shamba hilo .

 Kamanda Kuzaga alieleza kuwa baada ya kuwa amefikisha chakula hicho na kukagua hali ya maendeleo ya mbuga hiyo ya mpunga  marehemu aliwaaga   vibarua waliokuwa wakifanya kazi na kuanza safari yake ya kurejea  nyumbani kwake katika Mtaa wa Mpanda Hotel.

 Wakati akiwa anaondoka kulikuwa na dalili za mvua  kutaka kunyesha hata hivyo hari hiyo haikumfanya ashindwe kuendelea na safari yake ndipo wakati alikuwa amefika kwenye eneo la Kalilankulukulu alipigwa na radi wakati akiwa anaendesha pikipiki na kufa hapo hapo .

Alisema baada ya kuwa amepigwa na radi hiyo hadi kufa wananchi waliokuwa wanapita kwenye eneo hilo la barabara hiyo inayotoka Mpanda Mjini  kwenda Tarafa ya Karema waliuona mwili huu wa marehemu ukiwa kati kati ya barabara huku pikipiki yake ikiwa ipo pembeni yake .

 Wananchi hao waliweza kutowa taarifa kwa jeshi la Polisi ambao  walifika kwenye eneo hilo na kisha waliuchukuwa mwili wa marehemu na kuupeleka kwenye chumba cha kuhifadhi maiti katika Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Katavi .

   Kamanda Kuzaga alisema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali hiyo na baada ya uchunguzi utakabidhiwa kwa ndugu zake kwa ajiri ya mazishi aliwaondoa  mashaka ndugu wa marehemu   kuwa  kifo hicho kimetokana na radi ya mpango wa Mungu na wala wasifikilie tofauti na hivyo .

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja