Skip to main content

APATWA NA MAUTI KWA KUPIGWA NA RADI AKIENDESHA PIKIPIKI BARABARANI.



 Na Mwandishi Wetu.

         Katavi.


MTU  mmoja   Mkazi wa Mtaa wa Mpanda Hotel  katika Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi aliyejulikana kwa jina la  Paulo  Chundu  amekufa hapo hapo baada ya kupigwa na radi akiwa anaaendesha pikipiki wakati akitokea kwenye shamba la mpunga .

 Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Benjamin  Kuzaga aliwaambia wandishi wa habari kuwa tukio la kifo cha marehemu huyo  lilitokea hapo juzi majira ya saa 12  jioni katika eneo la  Kalilankuluku Tarafa ya Kabungu Wilaya ya Tanganyika .

 Kuzaga alieleza kuwa kabla ya tukio hilo marehemu huyo alikuwa ameaga nyumbani kwake kuwa anapeleka chakula  kwenye shamba lake la mpunga kwa ajiri ya chakula  cha vibarua waliokuwa wakifanya kazi kwenye shamba hilo .

 Baada ya kuwa ameaga nyumbani kwake marehemu huyo alipakia chakula hicho kwenye pikipiki  yake na kuelekea kwenye shamba hilo la mbuga ya mpunga lililoko katika Kijiji cha Ikaka na alifika salama  kwenye shamba hilo .

 Kamanda Kuzaga alieleza kuwa baada ya kuwa amefikisha chakula hicho na kukagua hali ya maendeleo ya mbuga hiyo ya mpunga  marehemu aliwaaga   vibarua waliokuwa wakifanya kazi na kuanza safari yake ya kurejea  nyumbani kwake katika Mtaa wa Mpanda Hotel.

 Wakati akiwa anaondoka kulikuwa na dalili za mvua  kutaka kunyesha hata hivyo hari hiyo haikumfanya ashindwe kuendelea na safari yake ndipo wakati alikuwa amefika kwenye eneo la Kalilankulukulu alipigwa na radi wakati akiwa anaendesha pikipiki na kufa hapo hapo .

Alisema baada ya kuwa amepigwa na radi hiyo hadi kufa wananchi waliokuwa wanapita kwenye eneo hilo la barabara hiyo inayotoka Mpanda Mjini  kwenda Tarafa ya Karema waliuona mwili huu wa marehemu ukiwa kati kati ya barabara huku pikipiki yake ikiwa ipo pembeni yake .

 Wananchi hao waliweza kutowa taarifa kwa jeshi la Polisi ambao  walifika kwenye eneo hilo na kisha waliuchukuwa mwili wa marehemu na kuupeleka kwenye chumba cha kuhifadhi maiti katika Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Katavi .

   Kamanda Kuzaga alisema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali hiyo na baada ya uchunguzi utakabidhiwa kwa ndugu zake kwa ajiri ya mazishi aliwaondoa  mashaka ndugu wa marehemu   kuwa  kifo hicho kimetokana na radi ya mpango wa Mungu na wala wasifikilie tofauti na hivyo .

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...