Skip to main content

Posts

Diwani na TARURA uso kwa uso,"Naomba Mwenyezi Mungu anipe roho ya kushuka"

Katavi: Diwani matatani kwa kumjeruhi Mkewe shingoni.

TANGANYIKA: WATU 32,000 WAPATA CHANJO YA UVIKO-19 NDANI YA SIKU SABA.

Sehemu ya Wananchi wa Luhafwe wakiwa wamejitokeza kupata chanjo ya UVIKO-19 leo Oktoba 31,2022. Mratibu wa chanjo Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika, Philip Mihayo. Zawadi Dakika,Afisa miradi kutoka Taasisi ya Benjamini Mkapa Shaban Juma,Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika. Dokta Alex Mrema,Mganga Mkuu Wilaya ya Tanganyika. Na Aidan Felson,Site Blog-Katavi. ****************************************** HALMASHAURI ya Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi kwa kushirikiana na Taasisi ya Benjamini Mkapa imefanikiwa ndani ya siku Saba kuwafikia na kuchanja Watu 32,000 wa chanjo ya kuzuia ugonjwa wa UVIKO-19 katika Halmashauri hiyo, kupitia kampeni ya uhamasishaji wa uchanjanji nyumba kwa nyumba ya siku Tisa. Akizungumza na waandishi wa habari katika eneo la Kijiji cha Luhafwe sehemu iliyotengwa maalum kwa ajili ya utoaji chanjo,Mratibu wa chanjo Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika, Philip Mihayo amesema idadi hiyo imefikiwa kutokana na hamasa na mbinu shirikishi iliyotumika...

VIONGOZI WA WAFANYAKAZI WATAKIWA KUNOLEWA CHUONI MBEYA.

Na  Castus Bhusolo,Site Blog-Mbeya . ********************************* VIONGOZI wa vyama vya Wafanyakazi nchini wameombwa kuleta wafanyakazi wao katika chuo cha wafanyakazi OTU kilichoko mkoani Mbeya ili kupewa elimu itakayowasaidia kuondokana na migogoro ndani ya Vyama. Ameyasema hayo Rais wa shirikisho la Vyama vya wafanyakazi nchini TUCTA Tumain Nyamhokya wakati akifunga mafunzo maalumu yaliyotolewa kwa wafanyakazi. "Nawashukuru sana kwa ushirikiano wenu katika semina hii, Mmejifunza muundo wa vyama vyetu vya wafanyakazi, chati ya uongozi katika vyama vyetu lakini pia mmejifunza majukumu yenu kama wajumbe wa kamati tendaji ya Taifa ya chama cha wafanyakazi TALWGU ninaamini elimu hii mtaitumia vyema kwa manufaa ya chama na wafanyakazi kwa ujumla" "Chuo hiki cha wafanyakazi Mbeya kilichangiwa na wafanyakazi wote nchi nzima wako waliokatwa kwenye mishahara yao na chuo hiki kikajengwa kimejengwa mwaka 1974-1975, 1976 kikaanza kutoa mafunzo nitoe wito kwa waajiri na vion...

Katavi: Mwenyekiti Mtaa wa Shanwe adaiwa kupigwa Risasi,Diwani na Viongo...

Viongozi pasua kichwa migogoro ya Ardhi//Watu wauziwa eneo la VETA,Mkuu ...

MPIMBWE: VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA CHANZO CHA MIGOGORO YA ARDHI.

Mkuu wa Wilaya ya Mlele Filberto Sanga akizungumza wakati wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe Oktoba 27,2022. Na Aidan Felson, Site Blog-Katavi. ******************************************** IMEBAINISHWA kuwa,Migororo ya Ardhi katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe Mkoani Katavi inazidi kuongezeka kila siku,huku chanzo cha migogoro hiyo kikitajwa ni viongozi. Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Filberto Sanga,wakati wa kikao cha Baraza la madiwani la halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe lililofanyika Oktoba 27,2022 katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri. Sanga amesema wapo baadhi ya viongozi wasio waadilifu wanatumia nafasi zao kuwachochea wananchi kuvamia maeneo ikiwemo viongozi hao kuwatapeli Wananchi kutoa maeneo yao kwa madai ni kwa ajili ya matumizi ya Kijiji wakati sio kweli. Akitolea mfano moja ya mgororo,DC Sanga amesema "Kulikuwa na suala kule Ukimbwamizi,suala la mnara wa Voda,ule mgogoro ni ujanja tu. Wale viongozi wangu wanaelea,baada ya ...