Skip to main content

VIONGOZI WA WAFANYAKAZI WATAKIWA KUNOLEWA CHUONI MBEYA.



Na Castus Bhusolo,Site Blog-Mbeya.

*********************************

VIONGOZI wa vyama vya Wafanyakazi nchini wameombwa kuleta wafanyakazi wao katika chuo cha wafanyakazi OTU kilichoko mkoani Mbeya ili kupewa elimu itakayowasaidia kuondokana na migogoro ndani ya Vyama.

Ameyasema hayo Rais wa shirikisho la Vyama vya wafanyakazi nchini TUCTA Tumain Nyamhokya wakati akifunga mafunzo maalumu yaliyotolewa kwa wafanyakazi.

"Nawashukuru sana kwa ushirikiano wenu katika semina hii, Mmejifunza muundo wa vyama vyetu vya wafanyakazi, chati ya uongozi katika vyama vyetu lakini pia mmejifunza majukumu yenu kama wajumbe wa kamati tendaji ya Taifa ya chama cha wafanyakazi TALWGU ninaamini elimu hii mtaitumia vyema kwa manufaa ya chama na wafanyakazi kwa ujumla"

"Chuo hiki cha wafanyakazi Mbeya kilichangiwa na wafanyakazi wote nchi nzima wako waliokatwa kwenye mishahara yao na chuo hiki kikajengwa kimejengwa mwaka 1974-1975, 1976 kikaanza kutoa mafunzo nitoe wito kwa waajiri na viongozi wa vyama waleteni wafanyakazi katika chuo hiki ili wapate elimu Stahiki"

Makam Mwenyekiti wa TALWGU, Ronward Mwasuya ameeleza mafunzo wanayopewa viongozi yanawanufaisha kwakuwa mbali na kutanua wigo wa fikra na maarifa inawasaidia pia kujua namna kuwasimamia wafanyakazi katika haki zao.

"Ili uwe kiongozi bora unatakiwa kujua ni nini ukifanye kwa wanachama wako kwahiyo viongozi wanapoletwa kupatiwa elimu inawasaidia na kuwalahisishia usimamizi na utendaji katika kazi zao"

Mjumbe wa kamati ya utendaji Taifa Rehema Omary Kabanda amesema baada ya mafunzo haya sasa yuko tayari kwenda kuwaelimisha wafanyakazi juu ya haki na wajibu wao wanaotakiwa kufanya ikiwemo wajibu wa kustaafu nankukumbushara baadhi ya taratibu na misingibya maadili katika kazi.

Akizungumzia ubora wa chuo cha wafanyakazi Mbeya Mkuu wa Chuo hicho Ezron Kaya amesema jitihada za kutoa elimu kwa viongozi wa wafanyakazi zinaendelea hawana mashaka kwakuwa chuo hicho ni cha muda mrefu na kimewanoa vionvozi wengi.

"Mimi niseme Waajiri wasione shaka kuwaleta wafanyakazi wao kupewa elimu,chuo hiki kimejitosheleza na gharama zake ni za kawaida mfano kwa mtu mmoja ni Laki5 wiki nzima au siku tano na hapo unahudumiwa kila kitu na elimu unayopata ni ya uhakika! Sasa kwanini viongozi wasije kunolewa hapa!!?"

MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...