Skip to main content

MPIMBWE: VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA CHANZO CHA MIGOGORO YA ARDHI.




Mkuu wa Wilaya ya Mlele Filberto Sanga akizungumza wakati wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe Oktoba 27,2022.

Na Aidan Felson, Site Blog-Katavi.

********************************************

IMEBAINISHWA kuwa,Migororo ya Ardhi katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe Mkoani Katavi inazidi kuongezeka kila siku,huku chanzo cha migogoro hiyo kikitajwa ni viongozi.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Filberto Sanga,wakati wa kikao cha Baraza la madiwani la halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe lililofanyika Oktoba 27,2022 katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri.

Sanga amesema wapo baadhi ya viongozi wasio waadilifu wanatumia nafasi zao kuwachochea wananchi kuvamia maeneo ikiwemo viongozi hao kuwatapeli Wananchi kutoa maeneo yao kwa madai ni kwa ajili ya matumizi ya Kijiji wakati sio kweli.

Akitolea mfano moja ya mgororo,DC Sanga amesema "Kulikuwa na suala kule Ukimbwamizi,suala la mnara wa Voda,ule mgogoro ni ujanja tu. Wale viongozi wangu wanaelea,baada ya voda kufika Serikali ya Kijiji kutafuta eneo, viongozi wangu walienda kumshawishi Mama mmoja,tunaliomba hili eneo tulitumie kwa kazi za Kijiji"

"Yule Mama bila kujua,akaridhia akawapa,baada ya kuwapa muda haukupita 2019/20 Vodacom wakaenda pale kusimika mnara. Yule Mama akawaambia kumbe mlikuwa mnanizunguka mnajua hili? Basi naomba na Mimi nipate kidogo,wakasema hapana hatukupi wewe umeshalitoa hili eneo"

Kufuatia hali hiyo, Serikali imeamua mama huyo arudishiwe eneo lake na mkataba utenguliwe asaini mama huyo.

Katika hatua nyingine,amewataka viongozi wote Wilayani humo kufanya maandalizi ya utekelezaji wa miradi ya mazingira mapema kwa kuotesha vitalu ili ifikapo mwakani suala hilo litekelezwe kikamilifu kama yalivyo maagizo ya Rais Samia Suluhu Hassan.

Hata hivyo,Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe limewataka wananchi wote waliojenga eneo la mnada lililopo Kata ya Majimoto kubomoa haraka na kuondoka eneo hilo kabla Serikali haijaingilia kati.

"Halmashauri yetu kwa ujumla tuna changamoto kubwa sana ya migogoro ya Ardhi,na hususani kwenye maeneo ya Kasisi na pale kwenye eneo letu la Majimoto kwenye mnada,wananchi wanaendelea kuvamia"- Alisema Mwenyeketi wa Halmashauri hiyo,Sailas Irumba.

Aidha,amesisitiza elimu izidi kutolewa kwa Wananchi ili kunusuru hifadhi za Misitu.

MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...