Skip to main content

MPIMBWE: VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA CHANZO CHA MIGOGORO YA ARDHI.




Mkuu wa Wilaya ya Mlele Filberto Sanga akizungumza wakati wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe Oktoba 27,2022.

Na Aidan Felson, Site Blog-Katavi.

********************************************

IMEBAINISHWA kuwa,Migororo ya Ardhi katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe Mkoani Katavi inazidi kuongezeka kila siku,huku chanzo cha migogoro hiyo kikitajwa ni viongozi.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Filberto Sanga,wakati wa kikao cha Baraza la madiwani la halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe lililofanyika Oktoba 27,2022 katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri.

Sanga amesema wapo baadhi ya viongozi wasio waadilifu wanatumia nafasi zao kuwachochea wananchi kuvamia maeneo ikiwemo viongozi hao kuwatapeli Wananchi kutoa maeneo yao kwa madai ni kwa ajili ya matumizi ya Kijiji wakati sio kweli.

Akitolea mfano moja ya mgororo,DC Sanga amesema "Kulikuwa na suala kule Ukimbwamizi,suala la mnara wa Voda,ule mgogoro ni ujanja tu. Wale viongozi wangu wanaelea,baada ya voda kufika Serikali ya Kijiji kutafuta eneo, viongozi wangu walienda kumshawishi Mama mmoja,tunaliomba hili eneo tulitumie kwa kazi za Kijiji"

"Yule Mama bila kujua,akaridhia akawapa,baada ya kuwapa muda haukupita 2019/20 Vodacom wakaenda pale kusimika mnara. Yule Mama akawaambia kumbe mlikuwa mnanizunguka mnajua hili? Basi naomba na Mimi nipate kidogo,wakasema hapana hatukupi wewe umeshalitoa hili eneo"

Kufuatia hali hiyo, Serikali imeamua mama huyo arudishiwe eneo lake na mkataba utenguliwe asaini mama huyo.

Katika hatua nyingine,amewataka viongozi wote Wilayani humo kufanya maandalizi ya utekelezaji wa miradi ya mazingira mapema kwa kuotesha vitalu ili ifikapo mwakani suala hilo litekelezwe kikamilifu kama yalivyo maagizo ya Rais Samia Suluhu Hassan.

Hata hivyo,Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe limewataka wananchi wote waliojenga eneo la mnada lililopo Kata ya Majimoto kubomoa haraka na kuondoka eneo hilo kabla Serikali haijaingilia kati.

"Halmashauri yetu kwa ujumla tuna changamoto kubwa sana ya migogoro ya Ardhi,na hususani kwenye maeneo ya Kasisi na pale kwenye eneo letu la Majimoto kwenye mnada,wananchi wanaendelea kuvamia"- Alisema Mwenyeketi wa Halmashauri hiyo,Sailas Irumba.

Aidha,amesisitiza elimu izidi kutolewa kwa Wananchi ili kunusuru hifadhi za Misitu.

MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja