Skip to main content

WAHANGA WA VYETI "FEKI" WARUDISHIWA TABASAMU.


Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA) na Makam M/kiti wa TALWGU  Tumaini Nyamhokya.




Na Castus Bhusolo,Site Blog-Mbeya.

***************************************************************

KUFUATIA taarifa ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na wenye Ulemavu, Joyce Ndalichako ya kuutaarifu UMMA kwamba Rais Samia Suluhu Hassan ameridhia maombi ya viongozi kuwalipa wale wafanyakazi waliopata shida ya vyeti Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA),Tumaini Nyamhokya amewaongoza wafanyakazi wengine kumpongeza Rais Samia kwa moyo wake wa kuwajali na kuwafuta machozi wafanyakazi walioondolewa kwenye mfumo wa ajira kwasababu ya changamoto ya Vyeti.


Nyamhokya ambaye pia ni Makam M/kiti wa TALWGU amesema wafanyakazi hao Walitoka ghafla lakini sasa wanakwenda kulipwa Stahiki zao kila mmoja kwa kadri ya kiwango alichoweka.

"Ni ukweli wa wazi kuwa waliumia kwakuwa hawa wenzetu walizoea makazinii hawakujua kama kuna siku wataondolewa kwenye mfumo walizoea malezi ya serikali nasi kama Viongozi tumehangaika  kuwasaidia na kuwasemea tangu tulipoingia madarakani mwaka 2016 lakini sasa leo wanaenda kupata faraja walioweka asilimia 5 watalipwa asilimia tano na walioweka asilimia 10 watalipwa hiyohiyo.

Aidha Nyamhokya ameongeza kuwa "Wakati ule waliondolewa wengi, wenzetu wenye elimu ya darasa la saba walirejeshwa lakini hawa waliokuwa na shida ya vyeti hawakurejeshwa kazini na hawakuwahi kulipwa chochote lakini siku ya leo (jana) naamini taarifa hii itarejesha tabasamu lao lililopotea muda mrefu.

Elizabeth Kalinga ambaye ni mmoja wa waathirika, amesema wakati anakumbwa na mkasa huo alikuwa Mtendaji wa Kata Iwambi kwa zaidi ya miaka 15 na wakati anapokea taarifa ya kusitishwa kazi alikuwa anaumwa.

"Wakati nakumbwa na hili nilikuwa nimeomba kustaafu maana umri ulikuwa unafika, mwezi wa pili niliomba na mwezi wa tatu nikakubaliwa na mchakato wote ulikamilika na fedha ziliingia lakini nilipozifuata nikaambiwa zimezuiliwa," alisema Elizabeth.

Tumaini Mbonamasabo ambaye ni Afisa TEHAMA halimashauri wilaya ya Babati amesema Serikali inekuwa ikifanya kazi kwa ukaribu na viongozi wa wafanyakazi kama utoaji elimu juu ya uadilifu na uwajibikaji katika kazi hivyo kitendo alichokifanya Rais Samia cha kuridhia kuwapatia Mafao wafanyakazi hao ni kudhihirisha ubinadamu na utu alionao.

Changamoto hii ya kubaini Vyeti feki na wale wenye elimu isiyokidhi viwango kwa wafanyakazi ilianza mwaka 2016 ambapo mpaka kufika sasa ni miaka saba wako waliorejeshwa kazini na wako walioondolewa mpaka kufika sasa.

MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja