Skip to main content

ELIMU KWA JAMII JUU YA LISHE BORA YAHITAJIKA ILI KUPUNGUZA UTAPIAMLO (UDUMAVU).

Picha na Mtandao.

                **********************************************
                        Na Irene Temu,Katavi.

Ukosefu wa uhamasishaji kwa umma kuhusu huduma za lishe zinazopatikana kwa watoto chini ya umri wa miaka mitano na Mama wajawazito ndio tatizo kubwa la kuendelea kuwa  na utapiamlo.

Ambapo ukosefu wa lishe mchanganyiko na bora kwa kila kaya  kutokana na kipato kidogo katika familia huchangia  huku Elimu juu ya lishe ikihitajika.

Akizungumza na Mwandisi wa Habari hizi Afisa lishe Mkoa wa Katavi Asnath Mrema alisema kuwa Mwili kupokea virutubishi vya lazima Kama kalori,protini,mafuta,wanga,vitamini na madini uhaba au wingi wa vitu hivyo katika mwili husababisha utapiamlo.

Sambamba na kukosa chakula cha kutosha na mtoto kukaa na njaa ya muda mrefu au kushiba bila kujali uwiano wa virutubishi ndani ya chakula nayo Ni sababu mojawapo ya mtoto kupata utapiamlo

Aidha aliongeza kuwa   udumavu huweza kutokea kati ya siku moja tangu kutungwa mimba Hadi siku 1000 hivyo mama mjamzito anatakiwa kupata lishe Bora Ili kuweza kurutubisha Afya ya Mwili wake na kiumbe aliyeko tumboni.

Pia alisema kuwa kupitia Mpango wa Utekelezaji wa lishe ya kitaifa wa Mwaka 2016-2021 Asilimia 31.5 ya Watoto chini ya Miaka Mitano wanaudumavu kutoka Asilimia 88  ya Mwaka 1999.

Hivyo aliitaka jamii kuboresha namna ya ulishaji wa Watoto wachanga na wadogo na kushauri pia kunyonyesha kunapunguza viwango vya utapiamlo na vifo kwa watoto.

Nae Daktari Erick Mwijage aliongeza kuwa maradhi ya kuambukiza kama homa ya matumbo,nimonia,malaria huongeza mahitaji ya lishe hivyo endapo mtoto atakosa huishia kupata utapiamlo.

"Endapo ukosefu wa lishe utatokea wakati wa ujauzito au kabla ya umri wa miaka miwili huenda ukasababisha matatizo ya kudumu katika ukuaji wa Mwili,akili,kimo cha chini,wembamba,viwango vya chini sana vya nguvu, miguu pamoja na tumbo kuvimba"alisema Daktari Erick

Pia alisema kuwa zipo aina mbili za ukosefu wa lishe ambapo alifafanua kwamba kuna ukosefu wa Lishe ya Protini ambayo huleta nguvu Mwilini na kusababisha Mtoto kuwa na unyafuzi.

Huku ukosefu wa lishe Bora ni Mtoto kukosa vyakula vyenye aina zote za virutubisho na Madini kama Ayodini na Vitamin A.

Hivyo jamii imetakiwa kizingatia chakula cha nyongeza kwa Watoto kati ya miezi 6 na miaka miwili huku kilimo kikiboreshwa kwa ajili ya kupata chakula cha kutosha Ili kupunguza umasikini na kuondoa uchafu katika mazingira yanayotuzunguka ili kupunguza magonjwa.

Sambamba na kuwawezesha wanawake kiuchumi kwani ndio nguzo kubwa katika kulea familia pamoja na Watoto.

MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...