Skip to main content

UDESO KUTOKOMEZA UKATILI WA KIJINSIA,MIMBA NA NDOA ZA UTOTONI


Mkurugenzi wa asasi ya Usevya Development Society (UDESO) Eden Wayimba
Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe Godfrid Nkuba 

Wazazi na walezi Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe Mkoani Katavi wameombwa kushirikiana na vyombo vya sheria katika kufichua matukio ya ubakaji na unyanyasaji wa kijinsia pindi yanapotokea katika jamii ili kutokomeza vitendo hivyo.


Hayo yamejiri katika hafla ya uzinduzi wa Mradi wa kushiriki kutokomeza na kupinga Ukatili na Unyanyasaji wa Kijinsia,Mimba na Ndoa za Utotoni ulioandaliwa na Taasisi ya Usevya Development Society (UDESO) kwa Ufadhili wa Taasisi ya Women Fund Tanania (WFT) na kufanyika katika Ukumbi wa Kapalale uliopo Halmashauri hiyo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya wadau wamesema kuwa wanakutana na changamoto pale wanapobaini vitendo hivyo ambapo wazazi na walezi hushirikiana na mhalifu kuficha uovu uliotokea.

"Levo yangu ni kumpelekea Mtendaji wa Kata ambae ni bosi wangu,lakini kesi ile ukipeleka pale inavurugwa vurugwa tuu bila sababu yoyote sijui kama inaenda Polisi,mimi nitaendelea kumfuatilia mtoto mpaka ntaitwa mnoko,naomba tujifuze watoto wana faida sana badae",amesema Patrick Nzowa Mkuu wa Shule ya Sekondari Usevya.

"Kazi yetu baada ya kuletewa taarifa ni kwenda kumkamata mhalifu,baada ya kumkamata familia au mzazi wanakwenda kuelewana na mhalifu,kesi ikishafika mahakamani mtoto anafundishwa kusema nililazimishwa nimtaje fulani,mwisho wa siku ushahidi unapotea",amesema Daniel Richard Mtendaji Kijiji cha Kibaoni.

Nae Damary Thomas ambae ni Mjumbe wa Bodi ya UDESO amesema kumekuwa na kasumba ya watu kuchukua mabinti wadogo wenye umri wa kusoma na kuwafanyisha kazi za majumbani hivyo kuishauri Serikali kwa kushirikiana na wananchi kufichua wanao watumikisha watoto.

Mila Potofu za pamoja na lugha za "Mchumba mchumba" pia zimetajwa na Jerome Mwakalemba kuwa sehemu ya chanzo cha matukio ya ubakaji na unyanyasaji wa Kijinsia katika Halmashauri hiyo.

Mkurugenzi wa asasi ya Usevya Development Society (UDESO) Eden Wayimba amesema lengo la mradi huo ni kutokomeza tatizo la Mimba za Utotoni na Ukatili wa Kijinsia uliokithiri katika Mkoa wa Katavi hivyo wanaamini kampeni hiyo itapunguza tatizo kwa kiasi kikubwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe Godfrid Nkuba amesema wao kama Serikali kwa kushirikiana na wananchi pamoja na taasisi hiyo wanaamini watakwenda kutokomeza na kupinga Ukatili na Unyanyasaji wa Kijinsia,Mimba na Ndoa za Utotoni katika Halmashauri hiyo kwani wamekuwa wakifanya hivyo katika utoaji wa Elimu hadi kwa Waendesha Pikipiki maarufu Bodaboda ambao pia wanatajwa kuwa sehemu ya chanzo cha Mimba za Utotoni.

Mimba 2965 sawa na 27% zilibainika katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe kwa Mwaka 2019/20 na Mimba 2628 sawa na 23% kwa Mwaka 2020/21.

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja