Skip to main content

MWENGE WA UHURU WARIDHISHWA NA MIRADI MPANDA,WAKATAA MRADI MMOJA.

Na.Swaum Katambo

Mpanda - Katavi.

Ikiwa Ujumbe Mkuu wa mbio za Mwenge wa uhuru Kitaifa kwa mwaka huu 2021 unasema "Tehama ni Msingi wa Taifa endelevu itumie kwa usahihi na uwajibikaji",Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Luteni Josephine Mwambashi leo Sep 24 amezindua Shughuli za TEHAMA katika Shule ya Wasichana Mpanda iliyopo Mkoani Katavi.
Baadhi ya wanafunzi Shule ya Wasichana Mpanda.

Mwenge wa Uhuru pia umeweza kuzindua baadhi ya klabu mashuleni zikiwemo klabu ya Mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI katika shule ya Msingi Uruwila,Klabu ya Mapambano dhidi ya Rushwa Shule ya Sekondari Nsimbo,Klabu ya mapambano dhidi ya dawa za kulevya Shule ya Msingi Kashato na Klabu ya lishe wanafunzi wa Shule ya Msingi Katavi.

Hata hivyo mwenge wa Uhuru umeweka mawe ya Msingi katika Miradi miwili ambayo ni Kituo cha Mafuta (MSS) na Ujenzi wa Barabara ya Mkumbo mita 600 kwa kiwango cha Lami.

Kadhalika, Mwenge wa Uhuru umezindua vyumba viwili vya madarasa na ofisi moja shule ya Msingi Uruwila,Zahanati ya Shanwe huku Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa uhuru Luteni Mwambashi akimalizia kwa kugawa vyandarua kwa mama wajawazito katika Zahanati hiyo.

Miradi yote iliyozinduliwa na kuwekwa mawe ya Msingi imeonekana kufanya vizuri ukilinganisha na gharama zilizotumika, isipokuwa Mradi mmoja wa Tanki la kuhifadhia Maji Ikolongo namba mbili uliopo eneo la Mapinduzi Kata ya Ilembo ambao umegharimu Tsh.Bil 1.7 Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru amekataa kuuzindua kwa kile alichodai gharama za ujenzi kuwa kubwa ukilinganisha na mradi huo.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Luteni Josephine Mwambashi.


Hata hivyo kufuatia changamoto hiyo ya kukataliwa kwa Mradi wa Maji Ikolongo namba mbili,Mbunge wa Mpanda Mjini Sebastian Kapufi amewataka watumishi wanapopewa dhamana ya kusimamia Miradi kuwa waangalifu na kutofanya ubadhilifu wa mali yoyote ya umma.






Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...