Skip to main content

MWENGE WA UHURU WARIDHISHWA NA MIRADI MPANDA,WAKATAA MRADI MMOJA.

Na.Swaum Katambo

Mpanda - Katavi.

Ikiwa Ujumbe Mkuu wa mbio za Mwenge wa uhuru Kitaifa kwa mwaka huu 2021 unasema "Tehama ni Msingi wa Taifa endelevu itumie kwa usahihi na uwajibikaji",Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Luteni Josephine Mwambashi leo Sep 24 amezindua Shughuli za TEHAMA katika Shule ya Wasichana Mpanda iliyopo Mkoani Katavi.
Baadhi ya wanafunzi Shule ya Wasichana Mpanda.

Mwenge wa Uhuru pia umeweza kuzindua baadhi ya klabu mashuleni zikiwemo klabu ya Mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI katika shule ya Msingi Uruwila,Klabu ya Mapambano dhidi ya Rushwa Shule ya Sekondari Nsimbo,Klabu ya mapambano dhidi ya dawa za kulevya Shule ya Msingi Kashato na Klabu ya lishe wanafunzi wa Shule ya Msingi Katavi.

Hata hivyo mwenge wa Uhuru umeweka mawe ya Msingi katika Miradi miwili ambayo ni Kituo cha Mafuta (MSS) na Ujenzi wa Barabara ya Mkumbo mita 600 kwa kiwango cha Lami.

Kadhalika, Mwenge wa Uhuru umezindua vyumba viwili vya madarasa na ofisi moja shule ya Msingi Uruwila,Zahanati ya Shanwe huku Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa uhuru Luteni Mwambashi akimalizia kwa kugawa vyandarua kwa mama wajawazito katika Zahanati hiyo.

Miradi yote iliyozinduliwa na kuwekwa mawe ya Msingi imeonekana kufanya vizuri ukilinganisha na gharama zilizotumika, isipokuwa Mradi mmoja wa Tanki la kuhifadhia Maji Ikolongo namba mbili uliopo eneo la Mapinduzi Kata ya Ilembo ambao umegharimu Tsh.Bil 1.7 Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru amekataa kuuzindua kwa kile alichodai gharama za ujenzi kuwa kubwa ukilinganisha na mradi huo.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Luteni Josephine Mwambashi.


Hata hivyo kufuatia changamoto hiyo ya kukataliwa kwa Mradi wa Maji Ikolongo namba mbili,Mbunge wa Mpanda Mjini Sebastian Kapufi amewataka watumishi wanapopewa dhamana ya kusimamia Miradi kuwa waangalifu na kutofanya ubadhilifu wa mali yoyote ya umma.






Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja