Skip to main content

FISH4ACP YAJA NA MPANGO WA UTUNZAJI WA FUKWE ZIWA TANGANYIKA


Na.Swaum Katambo,

Site Tv - Katavi.

Ikiwa ni Wiki ya kusafisha fukwe ulimwenguni kote,Watumiaji wa Ziwa Tanganyika katika Wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi wameombwa kuzingatia matumizi bora ya fukwe ili kuendelea kuwa na uhifadhi wa Mazingira katika fukwe hizo.

Akizungumza na chombo hiki Afisa Tarafa Kata ya Karema Mbonimpaye Ntiyonza Nkoronko amewaomba Watendaji wa Kata na Vijiji pamoja Wenyeviti wa Vitongoji kusimamia utunzaji bora wa fukwe pamoja na kuwa na Mpango Kazi wa kutembelea maeneo ya fukwe na kuhamasisha usafi wa mazingira.

"Hapa kuna watu wanaitwa BMU (Beach management unit) miongoni mwa Kazi walizonazo ni kusimamia hizi fukwe zisichafuliwe na matumizi bora ya fukwe hizi,ndio maana upande wa Karema wao ukikutwa unafua au unaoga ndani ya Ziwa ni faini,kama unataka kuoga chota maji kaogee nchi Kavu na kufua chota maji kafulie nchi kavu",Amesema Mbonimpaye.

Afisa Tarafa Kata ya Karema Mbonimpaye Ntiyonza Nkoronko

Afisa uvuvi kutoka Shirika la Chakula Duniani (FAO) na Mratibu wa Mradi wa Fish4ACP Hashim Muumin amesema wameamua kuungana na wengine ulimwenguni kusafisha Mwalo uliopo Kata ya Ikola Tarafa ya Karema pamoja na mazingira ya fukwe hizo ambazo  zimeelemewa sana na taka ngumu hasa plastiki zinazoingia katika maeneo ya uvuvi.

"Moja kati ya vitu ambavyo vinasabisha upungufu wa Samaki na matatizo katika maeneo yetu ya uvuvi ni hizi taka za plastiki,kwa sababu wakati mwingine zinazuia miale ya jua kuingia katika maji au vyanzo vya maji",Amesema Bw.Hashim.

Afisa uvuvi kutoka Shirika la Chakula Duniani (FAO) na Mratibu wa Mradi wa Fish4ACP Hashim Muumin.

Bw.Hashim ameongeza kuwa lengo la mradi huo ni kupunguza changamoto zilizopo, kuanzia kwa mvuvi hadi kwa mlaji katika Ziwa Tanganyika pamoja na kuutambulisha Mradi katika Mkoa wa Katavi.

Kwa Upande wake Afisa uvuvi katika Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika Donald Kusekwa amesema mradi wa Fish4ACP umesaidia kutoa hamasa kwa wananchi kusafisha maeneo ya fukwe hasa katika Mwalo wa Ikola ambapo hapo awali mazingira ya fukwe hayakuwa rafiki.

Nao baadhi ya wanachama wa BMU (Mpango wa usafi wa mazingira ya fukwe) wamesema hapo awali walikuwa wakisua sua kufanya usafi wa mazingira ya fukwe hizo hivyo mradi huo umewapa nguvu ya kuendelea kutekeleza majukumu yao kikamilifu.
Baadhi ya wana BMU wakiendelea na zoezi la kusafisha Fukwe katika Ziwa Tanganyika Mkoani Katavi.

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...