Skip to main content

FISH4ACP YAJA NA MPANGO WA UTUNZAJI WA FUKWE ZIWA TANGANYIKA


Na.Swaum Katambo,

Site Tv - Katavi.

Ikiwa ni Wiki ya kusafisha fukwe ulimwenguni kote,Watumiaji wa Ziwa Tanganyika katika Wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi wameombwa kuzingatia matumizi bora ya fukwe ili kuendelea kuwa na uhifadhi wa Mazingira katika fukwe hizo.

Akizungumza na chombo hiki Afisa Tarafa Kata ya Karema Mbonimpaye Ntiyonza Nkoronko amewaomba Watendaji wa Kata na Vijiji pamoja Wenyeviti wa Vitongoji kusimamia utunzaji bora wa fukwe pamoja na kuwa na Mpango Kazi wa kutembelea maeneo ya fukwe na kuhamasisha usafi wa mazingira.

"Hapa kuna watu wanaitwa BMU (Beach management unit) miongoni mwa Kazi walizonazo ni kusimamia hizi fukwe zisichafuliwe na matumizi bora ya fukwe hizi,ndio maana upande wa Karema wao ukikutwa unafua au unaoga ndani ya Ziwa ni faini,kama unataka kuoga chota maji kaogee nchi Kavu na kufua chota maji kafulie nchi kavu",Amesema Mbonimpaye.

Afisa Tarafa Kata ya Karema Mbonimpaye Ntiyonza Nkoronko

Afisa uvuvi kutoka Shirika la Chakula Duniani (FAO) na Mratibu wa Mradi wa Fish4ACP Hashim Muumin amesema wameamua kuungana na wengine ulimwenguni kusafisha Mwalo uliopo Kata ya Ikola Tarafa ya Karema pamoja na mazingira ya fukwe hizo ambazo  zimeelemewa sana na taka ngumu hasa plastiki zinazoingia katika maeneo ya uvuvi.

"Moja kati ya vitu ambavyo vinasabisha upungufu wa Samaki na matatizo katika maeneo yetu ya uvuvi ni hizi taka za plastiki,kwa sababu wakati mwingine zinazuia miale ya jua kuingia katika maji au vyanzo vya maji",Amesema Bw.Hashim.

Afisa uvuvi kutoka Shirika la Chakula Duniani (FAO) na Mratibu wa Mradi wa Fish4ACP Hashim Muumin.

Bw.Hashim ameongeza kuwa lengo la mradi huo ni kupunguza changamoto zilizopo, kuanzia kwa mvuvi hadi kwa mlaji katika Ziwa Tanganyika pamoja na kuutambulisha Mradi katika Mkoa wa Katavi.

Kwa Upande wake Afisa uvuvi katika Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika Donald Kusekwa amesema mradi wa Fish4ACP umesaidia kutoa hamasa kwa wananchi kusafisha maeneo ya fukwe hasa katika Mwalo wa Ikola ambapo hapo awali mazingira ya fukwe hayakuwa rafiki.

Nao baadhi ya wanachama wa BMU (Mpango wa usafi wa mazingira ya fukwe) wamesema hapo awali walikuwa wakisua sua kufanya usafi wa mazingira ya fukwe hizo hivyo mradi huo umewapa nguvu ya kuendelea kutekeleza majukumu yao kikamilifu.
Baadhi ya wana BMU wakiendelea na zoezi la kusafisha Fukwe katika Ziwa Tanganyika Mkoani Katavi.

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja