Skip to main content

WADAU WATOA MAONI MAREKEBISHO YA KANUNI ZA SHERIA YA EPOCA.


Naibu Katibu Mkuu wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Jim Yonazi akifungua Mkutano
wa wadau wa huduma za mawasiliano ili kutoa maoni kwenye rasimu ya maboresho ya kanuni 4
za Sheria ya Udhibiti wa Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta jijini Dodoma.


Mwakilishi kutoka Baraza la Habari Tanzania (MCT) na Umoja wa Haki za Kupata Taarifa
(CORI) akizungumza kwenye Mkutano wa wadau wa huduma za mawasiliano ili kutoa maoni
kwenye rasimu ya maboresho ya kanuni 4 za Sheria ya Udhibiti wa Mawasiliano ya Kielektroniki
na Posta jijini Dodoma.


Mkuu wa Kitengo cha Ufuatiliaji wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt. Philip
Filikunjombe akizungumza kwenye Mkutano wa wadau wa huduma za mawasiliano ili kutoa
maoni kwenye rasimu ya maboresho ya kanuni 4 za Sheria ya Udhibiti wa Mawasiliano ya
Kielektroniki na Posta jijini Dodoma.





Baadhi ya wadau wa huduma za mawasiliano wakifuatilia mkutano uliowakutanisha wadau hao
kwa ajili ya kutoa maoni kwenye rasimu ya maboresho ya kanuni 4 za Sheria ya Udhibiti wa
Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta jijini Dodoma.

                                 **************************************

                               Na Faraja Mpina na Colnelia Munyi, DODOMA

Serikali imewakutanisha wadau wa Sekta ya Mawasiliano na Habari kujadili na kutoa maoni kwenye rasimu ya marekebisho ya kanuni nne za Sheria ya Kielektroniki na Posta (EPOCA). Kanuni hizo ni kanuni za leseni, kanuni za maudhui mtandaoni, kanuni za miundombinu ya utangazaji kidijitali na kanuni za maudhui ya redio na runinga.

Akifungua kikao hicho kilichofanyika jijini Dodoma Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Jim Yonazi amesema kuwa Serikali imeona umuhimu wa kuwaita wadau hao ili kupata maoni yao kwasababu wao ndio watekelezaji wa kanuni hizo

Dkt. Yonazi amezungumza na wadau hao na kuwaeleza kuwa matamanio ya Serikali ni kuboresha mazingira ya watoa huduma za mawasiliano na habari nchini ili wananchi waweze kunufaika na kufaidi bidhaa na huduma bora za mawasiliano.

Ameongeza kuwa hadhira hiyo imekutana kwa ajili ya kufanya maboresho ya kanuni hizo kwa kutoa maoni yao katika maeneo ambayo yamefanyiwa mapitio hivyo ushirikiano wao na mchango wao unahitajika ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Naye Mkuu wa Kitengo cha Ufuatiliaji wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt. Philip Filikunjombe amesema kuwa maboresho ambayo wadau wanatolea maoni yanaenda kuleta mabadiliko katika Sekta ya Mawasiliano na Habari kwa kutenganisha kati ya watoa huduma za maudhui mtandaoni kama chombo cha habari na wale wanaotoa maudhui ambayo hayahusiani na vyombo vya habari

Amesema kuwa maboresho hayo yataenda kutatua sintofahamu ya nani anatakiwa kupatiwa leseni ya kuweka maudhui mtandaoni pamoja na kushusha ada ya leseni hizo kwa mwaka ambapo maombi ya leseni kwenye rasimu ya hiyo imeshuka kutoka shilingi laki moja hadi 50,000/= na ada ya leseni kwa mwaka imeshuka kutoka shilingi milioni moja hadi shilingi laki 5 kwa mwaka.

Aidha amezungumzia kanuni zilizopo kwa sasa zinawataka watoa huduma wa redio na runinga kuomba leseni ya kutaka maudhui yaleyale kuonekana mtandaoni lakini rasimu hiyo ya maboresho ya kanuni hawatatakiwa kuomba leseni tena ili vipindi vyao kuonekana kupitia mtandao.

Dkt. Filikunjombe amezungumzia maboresho ya kanuni hizo kuwa yanaenda kupunguza ada ya leseni ya kurusha matangazo ya redio na runinga kwa asilimia 30 na kuruhusu vituo vya redio na runinga kujiunga na vituo vingine kurusha maudhui yao bila kupata kibali kutoka TCRA isipokuwa watatakiwa kupeleka mpangilio wa vipindi unaoonesha kuwa atajiunga na kituo kingine.

Amesema kuwa maboresho hayo yanaenda kuhakikisha ving’amuzi vyote vinaonesha chaneli za bure bila kujali ni king’amuzi cha kulipia au la ili kuongeza wigo wa wananchi kupata taarifa.

Maboresho mengine yaliyofanyika ni katika vipengele vya matangazo ya mubashara na kuruhusu runinga za kulipia kuchukua matangazo na kubadili leseni ya redio na runinga za jamii kutoka leseni kubwa kwenda kuwekwa kwenye kundi la leseni ndogo.

Aidha, wadau mbalimbali walitoa maoni kuhusu rasimu ya kanuni hizo kwa makundi wakiwemo wadau kutoka Umoja wa Haki ya Kupata Taarifa (CORI), Baraza la Habari Tanzania (MCT), MISA Tanzania, Umoja wa Makampuni ya Simu Tanzania (TAMNOA),Wamiliki wa Vyombo vya Habari (MOAT), Wamiliki wa Ving’amuzi na Jukwaa la Wahariri Tanzania

Kanuni nne zilizofanyiwa maboresho ni miongoni mwa kanuni 22 za mawasiliano na utangazaji zinazosimamiwa na TCRA ambapo kanuni 18 zipo chini ya Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na kanuni 4 zipo chini ya Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini

Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...