Skip to main content

MIRADI MIKUBWA ITAKAYOTEMBELEWA NA WAZIRI MKUU KATIKA ZIARA MKOANI KATAVI AGOSTI 25-27.

Eneo la Karema unapojengwa Mradi wa Bandari.

Kiwanda cha Kuchakata Pamba (NGS) kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Mrindoko akizungumza na Waandishi wa Habari Ofisini kwake kuhusu ujio wa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

                        *******************************
                                    Na Mwandishi Wetu,Site Blog.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa anatarajia kufanya ziara ya Siku Tatu Mkoani Katavi ambapo atatembelea,kukagua na kuzindua Miradi mbalimbali ikiwemo Bandari ya Karema sanjari na kutembelea na kuzindua Kiwanda cha Kuchakata Pamba kilichopo Halmashauri ya Wilaya Tanganyika.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Ofisini kwake leo Agosti 23,2021 Mkuu wa Mkoa huo Bi.Mwanamvua Mrindoko amesema ziara hiyo ya Waziri Mkuu itaanza Tarehe 25-27 Agosti Mwaka huu ambapo amewaomba Wananchi kujitokeza katika maeneo yao kumlaki kwa kumshangilia Barabarani huku tahadhari za kujikinga na Virusi vya Corona zikichukuliwa.

"Naomba kuchukua nafasi hii kuwafahamisha rasmi Wananchi wote wa Mkoa wa Katavi kwamba tutapokea ugeni huu Mkubwa wa Kitaifa kwa Tarehe nilizozitaja (25-27,8,2021). Maeneo ambayo atayatembelea na kazi kubwa atakazozifanya ni za kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo na Mradi wa kwanza atakao ukagua ni Mradi wa Bandari ya Karema"-Alisema Mkuu huyo wa Katavi.

Aidha,Waziri Mkuu anatarajiwa kukagua Kituo cha Afya cha Mishamo ambapo pia atazungumza na Viongozi wa eneo la Mishamo ambalo ni Makazi ya Wakimbizi na terehe 27 Waziri Mkuu atatembelea Mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa na kisha atakagua Ujenzi wa Barabara ya kutoka Mpanda kuelekea Tabora.



Mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi utakaotembelewa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa. 


Barabara ya kutoka Mpanda kuelekea Tabora itakayokaguliwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

"Tunawaomba Wananchi wapokee Taarifa za ujio huo na wawe katika maeneo yao kwa ajili ya kulaki ugeni huu kwa kushangilia kwa sababu hapatakuwa na Mikutano ya hadhara kutokana na hali ya uwepo wa Covid,lakini Wananchi wawe katika  maeneo ya Barabara ambazo atapita ili waweze kumlaki kwa kumshangilia na kumkaribisha na wakiwa wamechukua tahadhari za kujikinga na Ugonjwa wa UVIKO"-Alisema RC Mrindoko

Katika hatua nyingine,Mhe.Mrindoko amewataka Wananchi Mkoani humo kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya Ugonjwa wa Corona,na ametoa wito kwa wale ambao bado hawajachanja kufika katika Vituo vya Afya waweze kupatiwa Chamjo.

Kadhalika,amewaondoa wasiwasi Wananchi kuhusu Usalama wa Mkoa kwani hadi sasa hakuna matukio makubwa yanayotishia usalama.

MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...