Skip to main content

MIGOGORO YA ARDHI BADO KIZUNGUMKUTI KATAVI.

Bibi Godlia Maenge,Mtoa kero.


Mkuu wa Mkoa wa Ktavi,Mhe.Mwanamvua Mrindoko akitoa maelekezo.

Na Mwandishi Wetu,Mpanda-Katavi.

Licha ya Serikali kuweka mifumo mizuri ya upimaji Ardhi,bado migogoro ya Ardhi ni tatizo katika Jamii hivyo ipo haja kwa Viongozi na Wataalam kutoka maofisini kukutana na Wananchi ikibidi kutenga Siku za kusikiliza kero mara kwa mara na kuzitatua kabla Mwananchi hajafanya uwekezaji na kumsababishia hasara.

Hilo linadhihirika katika Kikao cha Kwanza cha Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi.Mwanamvua Mrindoko cha kusikiliza kero,kilichofanyika Agosti 4,2021 Ofisini kwake ambapo Asilimia kubwa ya waliowasilisha kero zao ilikuwa ni masuala ya Ardhi.

Akiwasilisha kero yake kwa Mkuu wa Mkoa,Bibi  Godlia Constantino Maenge Mkazi wa Kichangani Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi amewalalamikia Mabwana Ardhi kuchukua eneo lake analoishi na kumpa Mtu mwingine huku wakimataka ahame eneo hilo kwa kile alichoelezwa ni eneo la wazi.

"Mabwana Ardhi kwenye eneo langu ninapoishi Kichangani,walilichukua wakampa Mtu mwingine Kiwanja nyuma yangu,baada ya hapo ndiyo nikaanza kulalamika juu ya huyo Baba waliempa Kiwanja tukikuja kusimama kwa Mkuu wa Mkoa wakamwambia hatuwezi tukamtoa Mkolechi (Mzee) pale tulipomkuta"-Bi.Maenge

Kutokana na kilio hicho,Mkuu wa Mkoa ametoa Siku Saba kwa Idara ya Ardhi Manispaa ya Mpanda kumtafuta huyo aliyepimiwa karibu na Bibi huyo ili ikiwezekana atafutiwe eneo lingine na alipwe fidia ampishe Bibi aendelee kuishi kwenye eneo ambalo amedai hawezi kulihama kwani ameshaliozea.

Hata hivyo,RC Mrindoko amesema anaweka utaratibu wa kila Mwezi kusikiliza Kero za Wananchi.

MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja