Skip to main content

MIGOGORO YA ARDHI BADO KIZUNGUMKUTI KATAVI.

Bibi Godlia Maenge,Mtoa kero.


Mkuu wa Mkoa wa Ktavi,Mhe.Mwanamvua Mrindoko akitoa maelekezo.

Na Mwandishi Wetu,Mpanda-Katavi.

Licha ya Serikali kuweka mifumo mizuri ya upimaji Ardhi,bado migogoro ya Ardhi ni tatizo katika Jamii hivyo ipo haja kwa Viongozi na Wataalam kutoka maofisini kukutana na Wananchi ikibidi kutenga Siku za kusikiliza kero mara kwa mara na kuzitatua kabla Mwananchi hajafanya uwekezaji na kumsababishia hasara.

Hilo linadhihirika katika Kikao cha Kwanza cha Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi.Mwanamvua Mrindoko cha kusikiliza kero,kilichofanyika Agosti 4,2021 Ofisini kwake ambapo Asilimia kubwa ya waliowasilisha kero zao ilikuwa ni masuala ya Ardhi.

Akiwasilisha kero yake kwa Mkuu wa Mkoa,Bibi  Godlia Constantino Maenge Mkazi wa Kichangani Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi amewalalamikia Mabwana Ardhi kuchukua eneo lake analoishi na kumpa Mtu mwingine huku wakimataka ahame eneo hilo kwa kile alichoelezwa ni eneo la wazi.

"Mabwana Ardhi kwenye eneo langu ninapoishi Kichangani,walilichukua wakampa Mtu mwingine Kiwanja nyuma yangu,baada ya hapo ndiyo nikaanza kulalamika juu ya huyo Baba waliempa Kiwanja tukikuja kusimama kwa Mkuu wa Mkoa wakamwambia hatuwezi tukamtoa Mkolechi (Mzee) pale tulipomkuta"-Bi.Maenge

Kutokana na kilio hicho,Mkuu wa Mkoa ametoa Siku Saba kwa Idara ya Ardhi Manispaa ya Mpanda kumtafuta huyo aliyepimiwa karibu na Bibi huyo ili ikiwezekana atafutiwe eneo lingine na alipwe fidia ampishe Bibi aendelee kuishi kwenye eneo ambalo amedai hawezi kulihama kwani ameshaliozea.

Hata hivyo,RC Mrindoko amesema anaweka utaratibu wa kila Mwezi kusikiliza Kero za Wananchi.

MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...