Skip to main content

TANESCO RUVUMA YASAMBAZA UMEME VIJIJI 119.

 
Jengo la TANESCO Mkoa wa Ruvuma


Baadhi ya watumishi wa TANESCO wakiongozwa na Meneja wa TANESCO Mkoa wa Ruvuma Florence Mwakasege walipotembelea ofisi ndogo ya TANESCO Madaba wilayani Songea.


Kituo cha kupozea umeme wa gridi kilichopo Unangwa mjini Songea.

Na,Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma.

SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) mkoani Ruvuma kupitia Wakala wa Umeme Vijijini (REA) limefanikiwa kusambaza umeme katika vijiji 119 kati ya lengo la kusambaza umeme vijiji 161.

Meneja wa TANESCO Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Florence Mwakasege amesema mradi huo umetekelezwa kupitia REA awamu ya tatu mzunguko wa kwanza ukihusisha pia ujenzi wa njia mbili za umeme wenye urefu wa Kilometa 106 kuelekea kituo cha kufua umeme wa maji Nakatuta Mto Ruvuma.

Amezitaja gharama za mradi huo kuwa ni zaidi ya shilingi bilioni 43 na kwamba vijiji ambavyo bado havijasambaziwa umeme utekelezaji wake upo katika hatua mbalimbali.

Mhandisi Mwakasege amesema tayari wateja 5,902 wa awali wameunganishiwa kati ya lengo la kuunganishiwa wateja 6,178 mradi huo utakapokamilika kwa asilimia 100

Amesema Mkoa wa Ruvuma una jumla ya vijiji 551,kati ya hivyo vijiji vyenye umeme ni 295,vijiji visivyo na umeme vilivyoomba kupitia REA awamu ya tatu mzunguko wa pili 256 na vijiji vitakavyokuwa na umeme baada ya miradi inayoendelea kukamilika ni 295.

Hata hivyo amesisitiza kuwa hadi kufikia Desemba 2022 vijiji vyote ambavyo havijapatiwa umeme katika Mkoa wa Ruvuma vinatarajiwa kumfikiwa na umeme.

Kuhusu upatikanaji wa umeme mkoani Ruvuma,Mhandisi Mwakasege amesema upatikanaji wa umeme ni wa kuridhisha baada ya Mkoa kuunganishwa na Grid ya Taifa katika Wilaya za Songea,Namtumbo,Mbinga,Nyasa na Tunduru.

“Mkoa wa Ruvuma pia unapata umeme kutoka kwa wawekezaji binafsi wa Kampuni za Tulila na Andoya ambao wana uwezo wa kufua umeme megawati 5.5 na kuingiza kwenye Grid ya Taifa’’,alisema Mwakasege.

Amewataja wateja waliounganishiwa umeme katika kipindi cha Julai 2020 hadi Machi 2021 kuwa ni 7,411 ukilinganisha na lengo la mwaka la kuunganisha wateja 6,000 sawa na asilimia 123.

MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...