Skip to main content

Wazee wa Mkoa wa Ruvuma waunda Baraza la Wazee.

Wawakilishi wa wazee wa Mkoa wa Ruvuma kutoka wilaya  zote tano wakiwa katika kikao maalum cha kuunda Baraza la wazee wa Mkoa pamoja na kuchagua viongozi watakaoongoza Baraza hilo ngazi ya Mkoa wa Ruvuma.


Mwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma ambaye pia ni Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimali watu akifungua kikao maalum cha uundaji wa Baraza la wazee Mkoa wa Ruvuma na kufanya  uchaguzi wa kuwapata viongozi watakaoliongoza baraza hilo ngazi ya Mkoa.

Na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Wazee wa Mkoa wa Ruvuma wamefanya kikao maalum cha uundaji Baraza la Wazee la Mkoa kilichofanyika kwenye ukumbi wa mipango Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma mjini Songea.

Waliochaguliwa kuunda Baraza hilo kwenye uchaguzi ulishirikisha wawakilishi kutoka wilaya za Nyasa,Mbinga,Songea,Tunduru na Namtumbo ni pamoja na Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Mkoa amechaguliwa Elenzian Nyoni kutoka Manispaa ya Songea.

Wengine waliochaguliwa ni Lusiana Nduguru kutoka Halmashauri ya Mji wa Mbinga ambaye amechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti,Katibu ni Winfrid Mbilinyi kutoka Halmashauri ya Madaba na Naibu Katibu Philipo Katyale kutoka Halmashauri ya Songea.

Viongozi wengine waliochaguliwa kuunda Baraza la Wazee wa Mkoa ni Mtunza Hazina amechaguliwa Esta Nzuyu kutoka Halmashauri ya Mji wa Mbinga,Mwakilishi wa wanaume Yustin Mande kutoka Halmashauri ya Nyasa na Mwakilishi wa wanawake amechaguliwa Maria Luoga kutoka Manispaa ya Songea.

Akizungumza wakati anafungua kikao cha uchaguzi huo,mgeni rasmi Mwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma Bakari Ally Mketo amesema Taifa linawategemea sana wazee ambao ni hazina kubwa katika jamii.

“Taifa bila wazee halina dira,wala muelekeo,sehemu yeyote panapokosekana wazee,pana hatari ya kuangamia’’,alisisitiza Mketo.

Amesema vijana wana mengi ya kujifunza kutoka kwa wazee kwa sababu wazee wanafahamu siri kubwa na hekima ya kuwa kiongozi bora ambapo amesisitiza kuwa Taifa linawategemea wazee ndiyo maana yanaundwa mabaraza ya wazee katika ngazi mbalimbali.

Amesema serikali imetoa nguvu kubwa katika mabaraza ya wazee na kwamba busara ya wazee kwenye mabaraza hayo itasaidia kutafutia ufumbuzi changamoto mbalimbali zinazowakabili wazee.

MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...