Skip to main content

Wakulima Morogoro wanufaika na Mradi wa zao la Mpunga.


Picha ikionesha Mfereji mkuu unaoepeleka maji mashambani katika skimu ya Msolwa Ujamaa.


Sehemu ya Miundombinu katika skimu ya Kilimo cha Umwagiliaji Msolwa ujamaa Kilosa mkoani Morogoro.


Picha Ikionesha Ghala la kuifadhia mazao katika skimu ya kilimo cha Umwagiliaji Njage katika Halmashauri ya Mlimba.


Bi. Wadara Kitada Afisa Kilimo katika Halmashauri ya Mlimba Mkoani Morogoro akizungumza katika skimu ya Njage wakati wa ziara ya kikazi katika miradi ya kuongeza uzalishaji wa zao la mpunga.

Na. Mwandhishi Wetu-Morogoro.

Wakulima katika skimu za kilimo cha umwagiliaji Mvumi, Msolwa Ujamaa na Njage zilizopo katika Wilaya ya Kilosa, Kilombero na Halmashauri ya Mlimba Mkoani Morogoro, zimenufaika na ukamilishwaji wa ujenzi wa skimu za kilimo cha umwagiliaji zilizopo chini ya mradi wa kuongeza uzalishaji wa zao la mpunga uliyofadhiliwa na Bank ya Dunia.

Wakiongea katika nyakati tofauti baadhi ya wakulima katika skimu hizo,walisema hali ya kilimo katika skimu hizo haikuwa rafiki kabla ya kuwepo kwa ujenzi wa miundombinu hiyo ambapo kwa sasa, hali ya kilimo ni nzuri kwani kuna uhakika wa kupata wastani wa mavuno ya gunia 20 mpaka 30 kwa heka kutokana na uhakika na matumizi sahihi ya maji katika misimu tofauti ya kilimo.

Bi Mwanaisha Kaluwa mkulima katika Skimu aya Mvumi Wilayani kilosa amesema “Naishukuru Serikali kwa kushirikiana na Bank ya Dunia kwa kutuletea mradi wenye manufaa kwetu sisi wakulima lakini Ombi langu ni kwamba Serikali itutaftie masoko ya uhakika kwani kwa sasa tunauza kupitia madalali ambao wanatuumiza sana , hawatumii vifungashio halali wanafunga kwa ktumia umbesa, tunaomba sana Serikali isimamie mpunga uuzwe kwa kutumia mizani.” Alisema Bi. Mwanaisha.

Afisa kilimo wa Halmashauri ya Mlimba Bi Wadara Kidata, akiongelea skimu ya kilimo cha umwagiliaji Njage alisema kabla ya mradi skimu ilikuwa na changamoto ya maji ambayo kwa sasa wanapata maji kwa wakati barabara ni nzuri ambazo zinarahisisha mazao kufika ghalani na kwa wanunuzi kwa wakati na gharama nafuu.

Kwa upande wake mwakilishi wa Mhandisi wa mkoa wa Umwagiliaji Morogoro Njanji Mlole, alisema kabla ya kukabidhi mradi huo ambao upo katika muda wa matazamio, mapungufu machache yaliyojitokeza ikiwa ni pamoja na kurekebisha mabanio na kuinua sehemu ya vipange vya barabara za skimu na kubadilisha ma karavati katika skimu ya Njage Mlimba, pamoja na kuingiza mfumo wa maji safi katika vyoo yatarekebishwa katika kipindi hicho kwa mujibu wa mkataba.

MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...