Skip to main content

RC IBUGE akagua mpaka wa Tanzania na Msumbiji kupitia Ziwa Nyasa.


Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Ruvuma na Kamati ya Ulinzi  na Usalama wilaya ya Nyasa,wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali ndani ya Mto Chiwindi ambao unagawa nchi ya Tanzania na Msumbiji kupitia wilaya ya Nyasa


Ni mmoja wa askari kutoka nchi ya Msumbiji akiwa  ng'ambo ya Mto Chiwindi ambako ni kijiji cha Shiwindi nchini Msumbiji akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge alipofanya ziara ya kutembelea mpaka wa Chiwindi unaotenganisha Tanzania na Msumbiji.


Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akizungumza na viongozi wa serikali katika ,kijiji cha Chiwindi Kata ya Chiwanda wilayani Nyasa,mpakani mwa Tanzania na nchi ya Msumbuji.


Na.Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amefanya ziara ya pili ya kukagua maeneo ya mipakani kwa kutembelea mpaka wa Chiwindi mwambao mwa ziwa Nyasa unaogawa Tanzania na nchi ya Msumbiji.

RC Ibuge katika ziara hiyo aliongozana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Ruvuma pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama wilaya ya Nyasa.

Akizungumza na viongozi na watendaji wa serikali katika kijiji cha Chiwindi,wilayani Nyasa,RC Ibuge ameagiza ulinzi na usalama katika eneo la mpaka kuimarishwa zaidi ili wananchi wanaoishi mpakani wasiwe na hofu bali waendelee kushiriki katika kazi za uzalishaji mali.

Hata hivyo amewataka wananchi wanaoishi mpakani kuwa walinzi wa kwanza na endapo wataona dalili za hatari wasipuuze, bali watoa taarifa haraka katika ngazi za juu ili hatua zichukuliwe haraka.

Ametoa rai kwa wananchi na wafanyabiashara wanaovuka mpaka kwenda Msumbiji kufuata maelekezo ya serikali,na hasa kutokana na kile ambacho kinaendelea katika nchi ya Msumbiji vikiwemo vitendo vya ugaidi ambapo amesisitiza kipaumbele cha kwanza kiwe ni maslahi ya Taifa.

Amewatahadharisha viongozi na watendaji waliopo mpakani wasiruhusu vitendo ambavyo vinahatarisha amani katika mipaka ya nchi ukiwemo mpaka wa Chiwindi ambako kuna mwingiliano wa wageni kutoka Msumbiji na kuingia Tanzania.

“Mipango ya serikali ni mikubwa,Rais wetu mama Samia Suluhu Hassan ana lengo la kuiendeleza nchi hii ipige hatua kubwa katika maendeleo’’,alisisitiza RC Ibuge.

Hata hivyo amesema bila amani na utulivu hakuna maendeleo,ambapo amewapongeza wananchi mwambao mwa ziwa kwa kufanya shughuli za kiuchumi ikiwemo kilimo cha zao la muhogo.

Hata hivyo amesema serikali kupitia ngazi ya wilaya ya Nyasa, inaandaa mpango kuviwezesha vikundi vidogo ili viweze kufanya kilimo cha ziada cha kuongeza kipato ambapo amesema wilaya ya Nyasa inafaa kwa kilimo cha michikichi ambacho kinazalisha mafuta ya kula ambayo yana soko kubwa hapa nchini.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Isabela Chilumba amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kwa ziara hiyo,ambayo amesema imeleta faraja kubwa kwa wananchi wa kijiji cha Chiwindi kilichopo mpakani mwa Tanzania na Msumbiji.

Hii ni ziara ya pili ya RC Ibuge kukagua maeneo ya mipaka katika Mkoa wa Ruvuma,ambapo katika ziara ya kwanza RC Ibuge alikagua mpaka wa Mkenda unaoigawa Tanzania na Msumbiji kupitia Mto Ruvuma wilaya ya Songea.

MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...