Skip to main content

MPANGO WA UBORESHAJI KILIMO CHA UMWAGILIAJI, KATAVI BADO CHANGAMOTO.




Mkulima Mdogo,Emmanuel Ramadhan.

Ramadhan Nyembe Mkulima Kijiji cha Majalila.

Baadhi ya Wakulima wakivuna Mpunga.





Magunia ya Mpunga.



PICHA  NA ZAINAB MTIMA,Site Tv

Na.Swaum Katambo,Tanganyika-Katavi.

Licha ya Serikali kuwekeza zaidi ya Bilioni 5 kwa ajili ya Skimu tatu za Umwagiliaji zilizopo Wilayani Mpanda ambazo ni Ugala,Mwamkulu na Uruila,Mkoa wa Katavi hauna Skimu iliyokamilika pamoja na kuwa Mpango wa Serikali wa Mwaka 2021/22 ni kuboresha Kilimo cha Umwagiliaji Nchini.

Hayo yanakuja mara baada ya Wakulima katika Kijiji cha Majalila Kata ya Tongwe Wilayani Tanganyika Mkoani Katavi kusikiliza Hotuba aliyoitoa Waziri wa Fedha na Mipango Mhe.Mwigulu Nchemba kuhusu Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2021/22 katika Sekta ya Kilimo kuwa Maeneo yatakayopewa msukumo ni pamoja na ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji.

"Kwa bajeti iliyosomwa inaonekana wakulima inatuinua,Serikali imetuangalia kwa macho mawili labda tusubiri utekelezaji kwa sababu yanayosemwa ni mazuri lakini kwenye utekelezaji sasa inaweza isifanye vizuri",Alisema Ramadhan Nyembe Mkulima Kijiji cha Majalila.

Nyembe ametolea mfano kwa Mkoa mzima wa Katavi kuwa una Skimu za Umwagiliaji tatu huku skimu hizo zikiwa hazijakamilika hivyo anaamini kuwa Serikali ikitilia mkazo katika Kilimo cha umwagiliaji na kuzikamilisha Skimu hizo wakulima watalima Kilimo chenye tija.

Kwa Mkoa wa Katavi Serikali ilitenga kiasi cha shilingi Bilioni 5.6 kwa Skimu tatu za Umwagiliaji ambapo Skimu ya  Ugalla ilitengewa Sh Bilioni 1.2, Skimu ya Umwagiliaji ya Mwamkulu ilitengewa Sh Bilioni 1.6 na Skimu ya Uruila ilitengewa sh Bilioni 1.8 lakini bado hazijakamilika.

Hata hivyo wakulima pia wameipongeza hatua ya Serikali kutaka kuimarisha mifumo ya upatikanaji wa pembejeo za kilimo ikiwemo zana za kilimo, mbegu bora za mazao, mbolea na viuatilifu. 

"Zamani tulikuwa tunanunuliana tuu una debe la Malamata (Mbegu ya kienyeji ya Mpunga) uniletee hapa,basi tunapanda tuu kienyeji..,lakini upatikanaji wa mbegu bora za mazao itakuwa na kipato kingi cha kutosha tofauti na tulivyozoea mwanzoni",Alisema Emmanuel Ramadhan Mkulima mdogo.

Aidha, wakulima katika Kijiji cha Majalila wameiomba Serikali kuwasogezea nyenzo au kuwapatia vifaa kwa ajili ya kuvunia mazao kwani wanapata Changamoto nyingi pindi unapofika msimu wa mavuno.

"Kama unavyoona hivi tunahangaika sana,lakini tungekuwa tunatumia mashine tungekuwa tumeshamaliza muda mrefu,tunaomba sana Serikali ituangalie hata kwa kutupa Mikopo ya Vitendea kazi tungeshukuru sana",Alisema  Nyembe.

Kwa Mujibu wa Waziri wa Fedha na Mipango Mhe.Mwigulu Nchemba wakati akiwasilisha Bungeni Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2021/22 amesema Serikali ina Mpango wa kuongeza matumizi ya teknolojia na mbinu za kilimo kinachohimili mabadiliko ya tabianchi,
kuongeza matumizi ya teknolojia bora katika uzalishaji wa mazao ili kuongeza uzalishaji na tija, kuimarisha vituo vya utafiti wa mbegu bora,vyuo vya mafunzo na vituo vya mafunzo ya wakulima na huduma za ugani. 

Kadhalika, Serikali inatarajia kuongeza thamani ya mazao ya kilimo na kuhakikisha upatikanaji wa masoko ya ndani na nje ya nchi,Vilevile itaendelea kuhamasisha uzalishaji wa mazao yakiwemo mazao ya kimkakati ya Mkonge, Chikichi, Tumbaku,Pareto,Korosho, Kahawa na Pamba. 

MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...