Skip to main content

MNADA WA PAMBA TANGANYIKA,WAKULIMA KICHEKO.


Pichani ni Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika,Salehe Mhando (aliyevaa Suti) akiwa na baadhi ya Wakulima wa Pamba katika tukio la uzinduzi wa Soko la Pamba katika Kijiji cha Sibwesa.





Mnunuzi wa Pamba kutoka Kampuni ya NGS Investment Co.Ltd Njalu Daudi Silanga.


Pichani ni Sephania Waya kutoka Idara ya Kilimo Wilayani Tanganyika.


Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika,Salehe Mhando akizungumza jambo na Wakulima pamoja na Wanunuzi wa Pamba.


Na.Swaum Katambo

Tanganyika-Katavi.

Wakulima wa Pamba Wilayani Tanganyika Mkoani Katavi wameipongeza Serikali kwa usimamizi mzuri wa ununuzi wa Pamba kwa bei elekezi ya Sh.1050 ukilinganisha na mwaka jana ambapo waliuza kwa Sh.810.

Wakizungumza katika tukio la uzinduzi wa Soko la Pamba uliofanyika Jana Juni 15,2021 katika Kijiji cha Sibwesa Wilayani humo,Wakulima wamesema kuwa mwaka huu wamepata manufaa ukilinganisha na gharama za uandaaji wa mashamba,ununuzi wa mbegu pamoja na palizi.

"Mwaka wa kwanza wakati wanzindua Pamba walikuwa wananunua kwa bei ya sh 1200 lakini kwenye malipo wananchi walidhurumika,hiyo ilipelekea kwenda kupungua kwa uzalishaji wa zao la Pamba"Alisema Kusekwa Mathias

Hata hivyo pamoja na unafuu wa kuongezeka kwa Bei elekezi ya mwaka huu Wakulima pia wameiomba Serikali kuangalia tena suala la bei ya Pamba kwani gharama za Uzalishaji ni kubwa hivyo faida wanayoipata ni ndogo.

Nae Mnunuzi wa Pamba kutoka Kampuni ya NGS Investment Co.Ltd Njalu Daudi Silanga amesema pamoja na kuwa wao ni wanunuzi wa Pamba lakini wataendelea kufanya kazi kwa ukaribu na Makarani ili kujua nini kinaendelea kwenye maeneo yao na kusema kuwa kazi hiyo si ya Serikali pekee.

"Kama kununua Pamba hakuna anayenizidi hapa,nimeanza kununua Pamba kwa Sandarusi,na mtu anaposema kwamba amekula shoti sio amekula shoti amebeba zile hela",alisema Njalu Silanga Mnunuzi wa Pamba.

Kwa upande wake Sephania Waya kutoka Idara ya Kilimo ambaye ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Halimashauri ya Wilaya ya Tanganyika amesema kwa Msimu wa Kilimo 2020/21 zilijitokeza changamoto mbalimbali ikiwemo Wakulima wengi kutokuwa na Elimu ya Kanuni za Kilimo bora cha Pamba na Matumizi sahihi ya Viuatilifu na Vinyunyizi hivyo ili kukabiliana na changamoto hiyo wamepanga kutoa Elimu ya utambuzi,uthibiti wa wadudu waharibifu na matumizi sahihi ya Viuatilifu na Vinyunyizi kwa wakulima kupitia Mikutano ya Wakulima na Redio za Kijamii.

Nae Mgeni rasmi katika tukio hilo Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Salehe Mhando amesema hatarajii kusikia mkulima hata mmoja analalamika kutolipwa pesa yake hivyo ametoa maagizo kwa Afisa Kilimo,watendaji na Maafisa Tarafa,wenyeviti,Madiwani na Bodi za Amcos kwa Wilaya nzima.

"Makarani najua Mikataba yenu haitazidi zaidi ya Miezi miwili sitatarajia kumuona Karani baada ya Miezi hii miwili anamiliki Gari..,ameenda kununua  kundi la Ng'ombe,taarifa hizo zilikuwa zinafanyika hapa ninazo"-Alisema DC Mhando

MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...