Skip to main content

Fedha za Ushuru Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika kuchunguzwa.







Mkaguzi wa nje wa hesabu za Serikali Mkoa wa Katavi,Mohamed Msangi akieleza jambo katika Mkutano wa Baraza la hoja la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika.


Na. Zainab Mtima,

Tanganyika-Katavi.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Bi. Mwanamvua Mrindoko ameagiza Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU Mkoania humo, kufatilia fedha zote za ushuru zilizotumiwa kinyume na utaratibu kabla ya fedha hizo hazijaingizwa kwenye mfumo.

Mrindoko ametoa maagizo hayo katika mkutano wa baraza la hoja la madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika ambapo amesema serikali haiwezi kuvumilia wizi wa aina hiyo ya matumizi holela ya fedha za serikali ambazohazijaingizwa kwenye akaunti ya Halmashauri.

Pia amemtaka mwenyekiti wa Halmshauri hiyo Bwana. Hamadi Mapengo kuhakikisha anasimamia hoja zote 35 zilizosalia kati ya hoja 55 zilizotolewa na mdhibiti na mkaguzi wa nje wa hesabu za serikali CAG kwa mwaka 2019-2020 zinafungwa haraka iwezekanavyo.

Miongoni mwa hoja hizo ni pamoja na madeni ya halmashauri pamoja na matumizi mabaya ya fedha za ushuru.

Sambamba na hilo Mrindoko amesema suala ya hoja kujirudia kila mwaka ni uzembe na kutowajibika kwa watumishi ipasavyo.

Kwa upande wake mkaguzi wa nje wa hesabu za serikali mkoa, Mohamed Msangi amesema hoja zilizojibiwa ni asilimia 36 pekee, huku asilimia 64 ya hoja zikiwa bado hazijapata majibu, huku fedha za serikali zikionekana kutumiwa ndivyo sivyo.

Katika hatua nyingine Mrindoko amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kwa kushirikiana na Katibu Tawala wa Wilaya kuhakikisha wanasimamia suala la watumishi hewa ili kuepuka mianya ya malipo hewa kwa watumishi ambao tayari wamehamishwa.

MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...