![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgOEWJqUF0b5Fz8TdoUlMOscMBcBaR64vtpGytW7c1-Y-L_5G_Bwj44sRKJoa6cUCUD2adVuPgoH0wQf_Zfoh4aB3rj4bnn3aVXmPIhCbL4Ta4AeDSXdGi28S5WScNDGeIfQ_FG47HIA6I/w640-h360/vlcsnap-2021-06-16-10h00m34s143.png)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhwKD_gYBB0b-yiHGC7PJRTOS2q8fVctQDP_dlJ9i6GEF51gYsV7TWeqwrFaT6HuyT0SrAP2QE3AHJaOJms3m8YJWOXeNzmmDUt1i-zqpGhefwQ6261FNf5vb8Mb4SkbnYxrIlRD4ITTcQ/w640-h360/vlcsnap-2021-06-16-09h59m14s52.png)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhV9qULo7qE6eZ2mruBz9SDIUsLh_F93c4ijSbCWNTfb6Kv_pyplZdxCd79_wsqS72C4Q7qKNCaXp_I1h1YKZio6LvYoqu1uuU4vbDEEK9HZDrhzj4ksostL2VsIKyU4OeB7bAMC2dYlVw/w640-h360/vlcsnap-2021-06-16-09h59m28s160.png)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgYfo4WsZmLgQJ_2-0zMhEgK-bp9QWHUvIPyIRvv9lyAq5Kv-4YEZxoL7uT4diAgoWqNXqHg-WV_sq95DtBJYzlhR04_Dqy8UjklFP1y-ePY06ipT-mnxhW_zsIsg0_hfUW_DBaPVYH1Vc/w640-h360/vlcsnap-2021-06-16-09h59m58s223.png)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiM4ORH1xbqX9pVUHTCFUnZ2CuZEQ23wZ5eC4GDWS7J0wZ6_OJRqQMcl3Z-8spyUSQmenqghD8NcGlm5_2yHZjT6pg6exaVOiICfTbEj3fJSiJrw7sLgHF27h-LCvP5P-4JgP3EplR7nq8/w640-h360/vlcsnap-2021-06-16-10h00m49s227.png)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhI__dcZAtGqdcF7fGA6XYqWyu_IZ2DbMDCqdq0AqAE5XphIeYPJ7v91gx0YqLX0rBdPgf75WMd2t-ipBgooKR9HPEwU2ffoQjSdyvacTuLK-kFUxH2Bmbkym01Y_7wjz8nMrgWKLVpdOw/w640-h360/vlcsnap-2021-06-16-10h01m47s59.png)
Na. Zainab Mtima,
Tanganyika-Katavi.
Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Bi. Mwanamvua Mrindoko ameagiza
Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU Mkoania humo, kufatilia fedha
zote za ushuru zilizotumiwa kinyume na utaratibu kabla ya fedha hizo
hazijaingizwa kwenye mfumo.
Mrindoko ametoa maagizo hayo katika mkutano wa
baraza la hoja la madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika ambapo amesema serikali haiwezi kuvumilia wizi
wa aina hiyo ya matumizi holela ya fedha za serikali ambazohazijaingizwa kwenye
akaunti ya Halmashauri.
Pia amemtaka mwenyekiti wa Halmshauri hiyo Bwana. Hamadi
Mapengo kuhakikisha anasimamia hoja zote 35 zilizosalia kati ya hoja 55 zilizotolewa na mdhibiti na mkaguzi wa nje
wa hesabu za serikali CAG kwa mwaka 2019-2020 zinafungwa haraka iwezekanavyo.
Miongoni mwa hoja hizo ni pamoja na madeni ya
halmashauri pamoja na matumizi mabaya ya fedha za ushuru.
Sambamba na hilo Mrindoko amesema suala ya hoja
kujirudia kila mwaka ni uzembe na
kutowajibika kwa watumishi ipasavyo.
Kwa upande wake mkaguzi wa nje wa hesabu za
serikali mkoa, Mohamed Msangi amesema hoja zilizojibiwa ni asilimia 36 pekee,
huku asilimia 64 ya hoja zikiwa bado hazijapata majibu, huku fedha za serikali
zikionekana kutumiwa ndivyo sivyo.
Katika hatua nyingine Mrindoko amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri
hiyo kwa kushirikiana na Katibu Tawala wa Wilaya kuhakikisha wanasimamia suala
la watumishi hewa ili kuepuka mianya ya malipo hewa kwa watumishi ambao tayari
wamehamishwa.
MWISHO.
Comments
Post a Comment