Skip to main content

RC HOMERA ATOA MAAGIZO KWA MA' DC NA DED KATAVI, WAKISHINDWA WAJIELEZE

Na, Swaum Katambo-Katavi

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Juma Homera ametoa siku 7 kwa wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri za Tanganyika,Nsimbo na Mlele kuwasilisha fedha za ujenzi wa Eneo la maonesho ya wakulima Nanenane lililopo Kata ya Kabungu Wilayani Tanganyika.

Maagizo hayo yametolewa leo Aprili 19,2021 katika kikao cha wadau wa Sekta ya Kilimo Mkoa wa Katavi kilichofanyika katika Ukumbi wa Idara ya Maji uliopo Manispaa ya Mpanda mara baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Afisa Kilimo wa Mkoa Faridu Mtiru alipokuwa akiwasilisha maadhimio yatokanayo katika kikao cha wadau wa Kilimo kilichoketi mnamo Desemba 16,2020.

Hata hivyo RC Homera amewaambia Wakuu wa Wilaya pamoja na Wakurugenzi endapo watashindwa kutekeleza agizo hilo waandike maelezo ya kushindwa kutekeleza huku akiwapongeza Manispaa ya Mpanda pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe ambao wamekwisha wasilisha fedha zao.

Kadhalika katika kikao hicho kilichokutanisha wadau wa Sekta ya Kilimo Mkoa wa Katavi, kilipata kuzungumzia baadhi ya changamoto zinazowakabili wakulima zikiwemo ucheleweshwaji wa malipo ya wakulima katika vyama vya msingi pamoja na ununuzi wa mazao kwa bei ndogo ambapo 
Mhasibu wa Bodi ya Nafaka na Mazao mchanganyiko Mkoani Katavi Zawadi Mrisho amesema wanatarajia kununua Tani 1000 za mazao ya Alizeti,Karanga,Maharage,Mahindi na Mpunga kwa bei isiyowaumiza wakulima.

Kwa upande wake Mrajis Msaidizi Mkoa wa Katavi Ibrahim Kakozi amesema Mkoa unatarajia kukusanya Tani 6937 za Ufuta kupitia vyama vya Ushirika, jumla ya Vyama vya Ushirika 19 vitashiriki katika zoezi la ukusanyaji na uuzaji wa Ufuta ghafi kwa msimu wa Mwaka 2021/2022.

MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja