Skip to main content

RC HOMERA ATOA MAAGIZO KWA MA' DC NA DED KATAVI, WAKISHINDWA WAJIELEZE

Na, Swaum Katambo-Katavi

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Juma Homera ametoa siku 7 kwa wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri za Tanganyika,Nsimbo na Mlele kuwasilisha fedha za ujenzi wa Eneo la maonesho ya wakulima Nanenane lililopo Kata ya Kabungu Wilayani Tanganyika.

Maagizo hayo yametolewa leo Aprili 19,2021 katika kikao cha wadau wa Sekta ya Kilimo Mkoa wa Katavi kilichofanyika katika Ukumbi wa Idara ya Maji uliopo Manispaa ya Mpanda mara baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Afisa Kilimo wa Mkoa Faridu Mtiru alipokuwa akiwasilisha maadhimio yatokanayo katika kikao cha wadau wa Kilimo kilichoketi mnamo Desemba 16,2020.

Hata hivyo RC Homera amewaambia Wakuu wa Wilaya pamoja na Wakurugenzi endapo watashindwa kutekeleza agizo hilo waandike maelezo ya kushindwa kutekeleza huku akiwapongeza Manispaa ya Mpanda pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe ambao wamekwisha wasilisha fedha zao.

Kadhalika katika kikao hicho kilichokutanisha wadau wa Sekta ya Kilimo Mkoa wa Katavi, kilipata kuzungumzia baadhi ya changamoto zinazowakabili wakulima zikiwemo ucheleweshwaji wa malipo ya wakulima katika vyama vya msingi pamoja na ununuzi wa mazao kwa bei ndogo ambapo 
Mhasibu wa Bodi ya Nafaka na Mazao mchanganyiko Mkoani Katavi Zawadi Mrisho amesema wanatarajia kununua Tani 1000 za mazao ya Alizeti,Karanga,Maharage,Mahindi na Mpunga kwa bei isiyowaumiza wakulima.

Kwa upande wake Mrajis Msaidizi Mkoa wa Katavi Ibrahim Kakozi amesema Mkoa unatarajia kukusanya Tani 6937 za Ufuta kupitia vyama vya Ushirika, jumla ya Vyama vya Ushirika 19 vitashiriki katika zoezi la ukusanyaji na uuzaji wa Ufuta ghafi kwa msimu wa Mwaka 2021/2022.

MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...