Skip to main content

KATAVI YAZIDI KUMUENZI HAYATI MAGUFULI NA AGIZO LA NYAMA PORI







Na Swaum Katambo-Katavi

Mkoa wa Katavi leo Aprili 14, 2020 umetimiza agizo la aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt John Pombe Magufuli  alipokuwa ziarani Mkoani Katavi mnamo Octoba 10, 2019 ambapo aliagiza uanzishwaji wa mabucha ya nyamapori nchini.

Akizindua Bucha hilo la nyamapori Mkuu wa Mkoa wa Katavi Juma Homera ametumia fursa hiyo kuwaasa wananchi kutojihusisha na matukio ya ujangili kwani kufanya hivyo ni kinyume cha sheria huku akitaja bei elekezi ya nyama hizo kuwa ni shilingi 8000 kwa kilo moja.

Kwa upande wake meneja wa Pori la Akiba (TAWA) Mkoa wa Rukwa Baraka Balagaye amesema wako tayari kushirikiana na wananchi watakaohitaji kufunga mabucha ya nyamapori ikiwa ni pamoja na kutoa miongozo isiyo na masharti magumu.

Hata hivyo Mmiliki wa Bucha lililozinduliwa Ndugu Vedasto Magaba ameishukuru Serikali na Taasisi mbalimbali kwa ajili ya kufanikisha adhma ya kufungua Bucha la nyamapori ikiwa ni Bucha la kwanza kwa Mkoa wa Katavi tangu tamko la Hayati Dkt Magufuli alipoelekeza kuanzishwa kwa mabucha hayo nchini huku akielezea changamoto ya upatikanaji wa wanyamapori kutokana na kipindi cha mvua za Masika wanyama kuwa mbali zaidi na kutopatikana kwa urahisi hali inayopelekea kutumia gharama kubwa.

Kwa upande wao wananchi wamemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe Homera kwa kusimamia uanzishwaji wa Bucha la nyamapori huku wakiomba huduma hiyo kuwa endelevu kadhalika na wahusika kupunguza bei kutoka ya shilingi 8000 hadi shilingi 7000 kwa siku za mbeleni ili kukidhi mahitaji ya wananchi wa hali ya chini.

MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...