Skip to main content

KATAVI YAZIDI KUMUENZI HAYATI MAGUFULI NA AGIZO LA NYAMA PORI







Na Swaum Katambo-Katavi

Mkoa wa Katavi leo Aprili 14, 2020 umetimiza agizo la aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt John Pombe Magufuli  alipokuwa ziarani Mkoani Katavi mnamo Octoba 10, 2019 ambapo aliagiza uanzishwaji wa mabucha ya nyamapori nchini.

Akizindua Bucha hilo la nyamapori Mkuu wa Mkoa wa Katavi Juma Homera ametumia fursa hiyo kuwaasa wananchi kutojihusisha na matukio ya ujangili kwani kufanya hivyo ni kinyume cha sheria huku akitaja bei elekezi ya nyama hizo kuwa ni shilingi 8000 kwa kilo moja.

Kwa upande wake meneja wa Pori la Akiba (TAWA) Mkoa wa Rukwa Baraka Balagaye amesema wako tayari kushirikiana na wananchi watakaohitaji kufunga mabucha ya nyamapori ikiwa ni pamoja na kutoa miongozo isiyo na masharti magumu.

Hata hivyo Mmiliki wa Bucha lililozinduliwa Ndugu Vedasto Magaba ameishukuru Serikali na Taasisi mbalimbali kwa ajili ya kufanikisha adhma ya kufungua Bucha la nyamapori ikiwa ni Bucha la kwanza kwa Mkoa wa Katavi tangu tamko la Hayati Dkt Magufuli alipoelekeza kuanzishwa kwa mabucha hayo nchini huku akielezea changamoto ya upatikanaji wa wanyamapori kutokana na kipindi cha mvua za Masika wanyama kuwa mbali zaidi na kutopatikana kwa urahisi hali inayopelekea kutumia gharama kubwa.

Kwa upande wao wananchi wamemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe Homera kwa kusimamia uanzishwaji wa Bucha la nyamapori huku wakiomba huduma hiyo kuwa endelevu kadhalika na wahusika kupunguza bei kutoka ya shilingi 8000 hadi shilingi 7000 kwa siku za mbeleni ili kukidhi mahitaji ya wananchi wa hali ya chini.

MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja