Skip to main content

ABIRIA WAPONGEZA SAFARI ZA MABASI DAR-KATAVI

Abiria Mkoani Katavi wameishukuru Kampuni ya Mabasi Adventure Connection kwa kurudisha safari za mabasi kutoka Katavi kwenda Dar es Salaam ambapo zilisitishwa kwa kipindi cha miaka miwili mfululizo hivyo kupelekea kupata changamoto ya usafiri.

Wakizungumza na Site Tv abiria hao wamesema hapo awali kulikuwa na changamoto hasa kwa abiria wanaohitaji kwenda mikoa ya Dodoma, Morogoro,Pwani na Dar es Salaam kutokana na kutokuwepo kwa usafiri wa moja kwa moja hivyo kupelekea kulala Tabora jambo ambalo lilikuwa likiwagharimu muda na fedha nyingi zikiwemo za chakula na malazi.

Kwa upande wake Msimamizi wa Kampuni ya Mabasi ya Adventure Connection Tawi la Mpanda Nassor Ally amesema walisitisha safari hizo kwa kipindi cha miaka miwili kutokana na changamoto za uendeshaji pamoja na Miundombinu ya barabara kutokuwa rafiki lakini kwa sasa wamejidhatiti ili kuhakikisha changamoto walizokabiliana nazo hazijitokezi tena.

Kadhalika, amewaasa abiria kutodanganyika na wapiga debe wa stendi ambao huwadanganya hakuna usafiri wa moja kwa moja kwenda Dar kwa lengo la kuwatapeli.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Stendi ya Mizengo Pinda Katavi Edward Gelard amewashauri wawekezaji waongeze mabasi ya abiria mkoani hapa kwa kuwa abiria ni wengi na mabasi ni machache.

MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja