Skip to main content

ABIRIA WAPONGEZA SAFARI ZA MABASI DAR-KATAVI

Abiria Mkoani Katavi wameishukuru Kampuni ya Mabasi Adventure Connection kwa kurudisha safari za mabasi kutoka Katavi kwenda Dar es Salaam ambapo zilisitishwa kwa kipindi cha miaka miwili mfululizo hivyo kupelekea kupata changamoto ya usafiri.

Wakizungumza na Site Tv abiria hao wamesema hapo awali kulikuwa na changamoto hasa kwa abiria wanaohitaji kwenda mikoa ya Dodoma, Morogoro,Pwani na Dar es Salaam kutokana na kutokuwepo kwa usafiri wa moja kwa moja hivyo kupelekea kulala Tabora jambo ambalo lilikuwa likiwagharimu muda na fedha nyingi zikiwemo za chakula na malazi.

Kwa upande wake Msimamizi wa Kampuni ya Mabasi ya Adventure Connection Tawi la Mpanda Nassor Ally amesema walisitisha safari hizo kwa kipindi cha miaka miwili kutokana na changamoto za uendeshaji pamoja na Miundombinu ya barabara kutokuwa rafiki lakini kwa sasa wamejidhatiti ili kuhakikisha changamoto walizokabiliana nazo hazijitokezi tena.

Kadhalika, amewaasa abiria kutodanganyika na wapiga debe wa stendi ambao huwadanganya hakuna usafiri wa moja kwa moja kwenda Dar kwa lengo la kuwatapeli.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Stendi ya Mizengo Pinda Katavi Edward Gelard amewashauri wawekezaji waongeze mabasi ya abiria mkoani hapa kwa kuwa abiria ni wengi na mabasi ni machache.

MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...