Skip to main content

WAWEKEZAJI NA WATOA HUDUMA ZA MITANDAO WATAKIWA KUBORESHA INTANETI






Na Mathias Canal, Katavi

Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Andrew Kundo (Mb) amewaomba wawekezaji na watoa Huduma za Mitandao ya mawasiliano kote Nchini kuhakikisha wanafanya tathmini ya mahitaji husika ya sasa katika maeneo ambayo minara inazidiwa.

Amewataka wawekezaji hao kuhakikisha kuwa wanayaboresha mawasiliano hayo, uwezo wake au kujenga minara mipya ili kuweza kusaidia katika maeneo husika.

Ameyasema hayo katika mwendelezo wa ziara zake za kukagua Miradi iliyopo chini ya Wizara ya Mawasilisiano na Taknolojia ya Habari akiwa katika eneo inapojengwa Bandari ya Karema iliyopo Mwambao wa Ziwa Tanganyika Mkoani Katavi ili kujionea uhalisia wa namna ya kuunganisha na kuimarisha mawasiliano katika ukanda wa ziwa Tanganyika.

Hata hivyo amewataka wawekezaji na watoa Huduma kuboresha maeneo ambayo yanatoa huduma ya mawasiliano ya simu pekee kuhakikisha wanaboresha huduma hiyo kutoka 2G hadi 3G ili watanzania wote waweze kutumia huduma ya Intaneti kwa kuwa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya Mwaka 2020-2025 inaelekeza kuhakikisha huduma ya Intaneti inapatikana kwa Asilimia 80%.

Mhandisi Kundo amesema serikali imejipanga kuangalia namna gani inavuta Mkonge wa Taifa kufika katika eneo la Bandari ya Karema ili kuhakikisha shughuli za Kitehama ikiwemo uwezo wa upatikanaji mtandao (Internet) kwa urahisi.

Kuhusu Changamoto ya Redio na Televisheni kutokuwa na usikivu wa kutosha katika maeneo ya Karema na Mishamo Naibu Waziri Mhandisi Kundo amesema wameshafanya mazungumzo na Shirika la Habari Tanzania (TBC) kuhakikisha kwamba uboreshaji wa Miundombinu ya TBC unarekebishwa ili kupata taarifa za kutosha na kuelimika kupitia Mawasiliano ya Redio.

Kadhalika, Naibu Waziri  Mhandisi Andrew Kundo (Mb) amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe Juma Homera kwa usimamizi madhubuti wa kuimarisha masuala ya Ulinzi na Usalama ukilinganisha na miaka ya nyuma.

MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja