Skip to main content

WAWEKEZAJI NA WATOA HUDUMA ZA MITANDAO WATAKIWA KUBORESHA INTANETI






Na Mathias Canal, Katavi

Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Andrew Kundo (Mb) amewaomba wawekezaji na watoa Huduma za Mitandao ya mawasiliano kote Nchini kuhakikisha wanafanya tathmini ya mahitaji husika ya sasa katika maeneo ambayo minara inazidiwa.

Amewataka wawekezaji hao kuhakikisha kuwa wanayaboresha mawasiliano hayo, uwezo wake au kujenga minara mipya ili kuweza kusaidia katika maeneo husika.

Ameyasema hayo katika mwendelezo wa ziara zake za kukagua Miradi iliyopo chini ya Wizara ya Mawasilisiano na Taknolojia ya Habari akiwa katika eneo inapojengwa Bandari ya Karema iliyopo Mwambao wa Ziwa Tanganyika Mkoani Katavi ili kujionea uhalisia wa namna ya kuunganisha na kuimarisha mawasiliano katika ukanda wa ziwa Tanganyika.

Hata hivyo amewataka wawekezaji na watoa Huduma kuboresha maeneo ambayo yanatoa huduma ya mawasiliano ya simu pekee kuhakikisha wanaboresha huduma hiyo kutoka 2G hadi 3G ili watanzania wote waweze kutumia huduma ya Intaneti kwa kuwa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya Mwaka 2020-2025 inaelekeza kuhakikisha huduma ya Intaneti inapatikana kwa Asilimia 80%.

Mhandisi Kundo amesema serikali imejipanga kuangalia namna gani inavuta Mkonge wa Taifa kufika katika eneo la Bandari ya Karema ili kuhakikisha shughuli za Kitehama ikiwemo uwezo wa upatikanaji mtandao (Internet) kwa urahisi.

Kuhusu Changamoto ya Redio na Televisheni kutokuwa na usikivu wa kutosha katika maeneo ya Karema na Mishamo Naibu Waziri Mhandisi Kundo amesema wameshafanya mazungumzo na Shirika la Habari Tanzania (TBC) kuhakikisha kwamba uboreshaji wa Miundombinu ya TBC unarekebishwa ili kupata taarifa za kutosha na kuelimika kupitia Mawasiliano ya Redio.

Kadhalika, Naibu Waziri  Mhandisi Andrew Kundo (Mb) amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe Juma Homera kwa usimamizi madhubuti wa kuimarisha masuala ya Ulinzi na Usalama ukilinganisha na miaka ya nyuma.

MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...