Skip to main content

UJENZI WA MRADI SHIRIKISHI WA MIUNDOMBINU YA UMWAGILIAJI WAANZA KARAGWE



Na; Mwandishi Wetu– Kagera

Ukarabati wa Miundombinu ya Kilimo cha umwagiliaji Wilayani Karagwe Mkoani Kagera Umeanza Rasmi, kwa ujenzi wa Barabara katika skimu ya kilimo cha umwagiliaji Mwisa pamoja na mifereji ya kupitisha maji kuelekea mashambani.

Akizungumza wakati wa kupokea vifaa vya ujenzi Mhandisi wa Umwagiliaji, ambaye pia ni Meneja Maradi huo shirikikishi Bw. Adelialidy Mwesigwe, Amesema amepokea baadhi ya viaafa ambavyo vitaweza kutumika katika ujenzi pamoja na kusakafia mfereji wenye urefu wa mita mia saba hamsini (750), ambapo mpaka sasa mtaro wenye urefu wa mita mia tano na mbili (502) umeshachimbwa na barabara yenye urefu wa mita mia saba na sitini (760) inayokwenda sambamba na mtaro huo imekwisha andaliwa.

“Tutajenga vikinga maji tisa, (9)  kwenye awamu hii kutokana na kwamba skimu hii ina ukubwa wa eneo la Hekta mia tatu (300) ambalo linalimwa zao la mpunga na mazao mchanganyiko.” Alisema Mwesigwa.

Aliendelea kusema kuwa eneo ambalo lpo nje kidogo  wakulima wanalima bustani za mbogamboga, na Skimu ina idadi ya wakulima mia moja na sabini na tano (175).

Miradi hii shirikishi ya maendeleo ya serikali ya awamu ya tano katika sekta ya kilimo cha umwagiliaji inashirikisha wananchi wakazi wa eneo husika katika ujenzi na ukarabati wa miundombinu hiyo.

MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Katavi akibidhiwa Ofisi,aelezwa Miradi ya kusimamia.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi,Mwanamvua Hoza Mrindoko wa kwanza Kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera wakati wa makabidhiano ya Ofisi. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani. Wakuu wa Wilaya,Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Rachel Kasanda. Na Mwandishi Wetu,Site Tv Mapema leo Mei 25,2021 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko,amekabidhiwa Ofisi na aliye kuwa Mkuu wa Mkoa huo Juma Zuberi Homera aliye hamishiwa Mkoani Mbeya kuwa Mkuu wa Mkoa. Katika makabidhiano hayo,Homera amemtajia Mkuu wa Mkoa wa Katavi miradi ambayo inatakiwa kusimamiwa hadi ikamilike ni pamoja na Bandari ya Karema,Hosipitali ya Rufaa Mkoa,Kiwanda cha Nguo,Jengo la Utawala pamoja na Umeme wa Gridi ya Taifa. Aidha,amesema Katavi ni Nyumbani hivyo atatoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku akiwakaribisha Viongozi na Wananchi kwa ujumla katika Mkoa wa Mbeya. "Kuna hili la Gridi ya Taifa ambalo linaendelea,kuna Kiwan...

Tabasamu hili kwa Wanafunzi,Nuru imewaka Juu yao/Mwekezaji afanya Jambo ...

Ajira Mpya Wakaribishwa Mlele, Full Kula Bata/Makubwa yaja