Skip to main content

UJENZI WA MRADI SHIRIKISHI WA MIUNDOMBINU YA UMWAGILIAJI WAANZA KARAGWE



Na; Mwandishi Wetu– Kagera

Ukarabati wa Miundombinu ya Kilimo cha umwagiliaji Wilayani Karagwe Mkoani Kagera Umeanza Rasmi, kwa ujenzi wa Barabara katika skimu ya kilimo cha umwagiliaji Mwisa pamoja na mifereji ya kupitisha maji kuelekea mashambani.

Akizungumza wakati wa kupokea vifaa vya ujenzi Mhandisi wa Umwagiliaji, ambaye pia ni Meneja Maradi huo shirikikishi Bw. Adelialidy Mwesigwe, Amesema amepokea baadhi ya viaafa ambavyo vitaweza kutumika katika ujenzi pamoja na kusakafia mfereji wenye urefu wa mita mia saba hamsini (750), ambapo mpaka sasa mtaro wenye urefu wa mita mia tano na mbili (502) umeshachimbwa na barabara yenye urefu wa mita mia saba na sitini (760) inayokwenda sambamba na mtaro huo imekwisha andaliwa.

“Tutajenga vikinga maji tisa, (9)  kwenye awamu hii kutokana na kwamba skimu hii ina ukubwa wa eneo la Hekta mia tatu (300) ambalo linalimwa zao la mpunga na mazao mchanganyiko.” Alisema Mwesigwa.

Aliendelea kusema kuwa eneo ambalo lpo nje kidogo  wakulima wanalima bustani za mbogamboga, na Skimu ina idadi ya wakulima mia moja na sabini na tano (175).

Miradi hii shirikishi ya maendeleo ya serikali ya awamu ya tano katika sekta ya kilimo cha umwagiliaji inashirikisha wananchi wakazi wa eneo husika katika ujenzi na ukarabati wa miundombinu hiyo.

MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...