Skip to main content

TAKUKURU YATOA WITO KWA JAMII KUKOPA KWENYE TAASISI ZA FEDHA ZINAZOTAMBULIKA





Na Swaum Katambo-Katavi

TAKUKURU Mkoani Katavi imeokoa na kurejesha fedha kiasi cha Shilingi Mil 10 kwa Mwalimu George Gabriel Kanyukamalunde ambaye ni  mstaafu aliyedhulumiwa fedha za mafao yake baada ya kukopa fedha kwa nyakati tofauti kutoka kwa mkopeshaji mmoja Mkoani hapa.

Akitoa taarifa mbele ya waandishi wa Habari Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Katavi Christopher Nakua amesema mnamo Disemba 3, 2020 walipokea taarifa kutoka kwa Bi. Catherine Mlenga ambaye ni mke wa Mwl Kanyukamalunde  juu ya madai hayo ambapo baada ya Mkopeshaji huyo kumkopesha mzee huyo alichukua Kadi yake ya Benki pamoja na namba za siri ambayo ndiyo iliyotumika kuchukulia fedha mara baada ya kiinua mgongo kutoka.

Ameongeza kuwa baada ya uchunguzi kukamilika mtuhumiwa alikiri makosa na kuahidi kumrejeshea mlalamikaji kiasi cha Shilingi Mil 20 ambapo ni tofauti ya fedha ambazo ilikuwa ni kama dhuluma kwa mlalamikaji kwani kiasi hicho cha fedha hakikuwa na maelezo ya kutosha kama ni riba au ni nini ambacho kilirejeshwa Februari 23, 2021.

“Mtuhumiwa alirejesha kiasi cha shilingi Mil 10 taslimu na kiasi kilichobaki cha shilingi Mil 10 atarejesha Aprili 30, 2021 ili kukamilisha kiasi cha shilingi Mil 20 alichomdhulumu Mwl Kanyukamalunde” Amekaririwa

Kwa upande wa wanafamilia ya Mwl Kanyukamalunde ambao ni Bi. Catherine Mlenga na mtoto wake Genuine Kanyukamalunde  wameishukuru TAKUKURU kwa kusaidia kupatiwa msaada huku wakisema pesa hizo zitakwenda kusaidia matibabu ya mzee wao kwani baada ya kudhulumiwa pesa zake alipata mshtuko na kumsababishia maradhi.

Katika hatua nyingie TAKUKURU Mkoa wa Katavi imemkamata Egid Damas Ntila ambaye ni Kaimu Katibu wa Serikali ya kitongoji cha Magula kilichopo Katika kijiji cha Mtisi, Kata ya Sitalike Wilayani Mpanda kwa kuomba Rushwa ya shilingi 300,000 na kupokea Rushwa ya shilingi 50,000 katika eneo la Soko Jipya la kitongoji cha Magula.

TAKUKURU Mkoa wa Katavi inatoa wito kwa wananchi kama kuna ulazima wa kukopa ni vizuri kwenda kukopa kwenye Taasisi za kifedha zilizo rasmi na zinazofuata sheria, taratibu na miongozo ya Benki Kuu ya Tanzania (BOT)

MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

WAJASIRIAMALI MPANDA WAILILIA SERIKALI KUCHELEWA UPATIKANAJI WA VITAMBULISHO

Na Swaumu Katambo, Katavi W afanyabiashara wadogo   katika stendi ya mabasi M izengo P inda wameiomba S erikali kuharakisha ugawaji wa vitambulisho ili kuep u kana na adha ya kulipa ushuru wa H almashauri ambao una   gharama  kubwa. W akizungumza na Site Tv  wajasiriamali M jini M panda wame i lalamikia H almashauri ya M anispaa ya M panda kuwatoza ushuru pasipo kuwa na utaratibu wowote . Mkurugenzi wa M anispaa ya M panda M ichael N zyungu amesema kuwa adha hiyo imetokana na kuchele we shwa kwa vitambulisho na amewataka wajasiriamali kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki. Vitambulisho vya ujasiriamali vilianzishwa na serikali maalumu kwa kuwasaidia wafanya   biashara wadogo kutoa huduma bila bugdha yoyote . MWISHO

Tufanye mabadiliko ya kina kwenye mfumo wa elimu -Mbunge Rose Tweve

KANISA KATOLIKI PAROKIA YA INYONGA LAFANYA MISA MAALUMU KUMUOMBEA DKT MAGUFULI, DC JAMILA ASISITIZA KUMUENZI KWA VITENDO

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akisisitiza jambo wakati  akizungumza kwenye Misa Maalumu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  ambaye pia ni  Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mlele  Mhe  Jamila Yusu ph akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kanisa katoliki Parokia ya inyonga mara baada ya kumalizika  Misa Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Kiongozi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga Padri  Maricelo Butoyi akiongoza Misa Maalumu ya  kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ya Kumuombea Hayati Dkt John Pombe Magufuli, tarehe 24 Machi 2021. Sehemu ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Inyonga wakifuatilia ibada Maalumu ...